Natafuta fremu ya biashara maeneo ya Mbezi Louis na jirani

Natafuta fremu ya biashara maeneo ya Mbezi Louis na jirani

kibebi

Senior Member
Joined
Feb 22, 2013
Posts
111
Reaction score
267
Hello!

Heri ya mwaka Mpya. Nilipata changamoto nikapotea kidogo Ila nimerudi (wakulungwa wanaelewa nimepotea wapi).

Back to business.

Ninaomba mnisaiaide kupata eneo zuri la biashara ya mahitaji ya nyumbani (unga, mchele, maharagwe, sukari, chumvi, diapers, mafuta na mahitaji mengine mengi ya nyumbani). Napendelea kuuza reja reja...

Eneo hilo niweze pia kuwa nauza fresh juice na maziwa kwa kuwasambazia watu waliopo eneo hilo na jirani na duka (kwa hiyo uwepo wa vijiwe na mzunguko wa watu ni muhimu).

Nitatoa kifuta jasho kwa atakayenielekeza chimbo La kueleweka nisije kata mtaji wangu.

Eneo napendelea liwe mitaa ya Mbezi ya Kimara, mitaa ya Kimara, pia Goba japo Goba sio kipaumbele.

Nasisitiza kutoa chochote kwa atakayenipa ushirikiano wa eneo zuri na ikiwezekana frem kabisa.

Asanteni kwa ushirikiano.
 
Kabla sijaenda kwa dalali nataka nipate maoni ya wapi nielekee...
Nimekuwa muoga Sana nisije Zika mtaji. HeLa saa hivi ni ngumu
Nasisitiza kutoa chochote kwa atakayenipa ushirikiano wa eneo zuri na ikiwezekana frem kabisa. Hapo lazima mtu kati ahusike mkuu.
Ila JF ni kubwa unaweza kupata mmiliki wa flem na mkayajenga.
All the best 🙏
 
Nasisitiza kutoa chochote kwa atakayenipa ushirikiano wa eneo zuri na ikiwezekana frem kabisa. Hapo lazima mtu kati ahusike mkuu.
Ila JF ni kubwa unaweza kupata mmiliki wa flem na mkayajenga.
All the best [emoji120]
Asante Sana
Nitampa chochote kitu atakayenipatia password
 
hapo pagumu maana kila palipochangamka hizo biashara zipo na hiyo ya duka inakata sana mitaji ya watu kwasababu ya gharama za fremu kuwa juu
 
hapo pagumu maana kila palipochangamka hizo biashara zipo na hiyo ya duka inakata sana mitaji ya watu kwasababu ya gharama za fremu kuwa juu
Ushauri wako pls
Nini kingine kifanyike?
 
Ushauri wako pls
Nini kingine kifanyike?
Ki ukweli inategemea upo sehemu gani je unakaa kwako au umepanga? na passion yako ni nini? maana ukifanya kitu ambacho sio hobby yako basi utaishia kupoteza pesa tuu.
 
Hello!

Heri ya mwaka Mpya. Nilipata changamoto nikapotea kidogo Ila nimerudi (wakulungwa wanaelewa nimepotea wapi).

Back to business.

Ninaomba mnisaiaide kupata eneo zuri la biashara ya mahitaji ya nyumbani (unga, mchele, maharagwe, sukari, chumvi, diapers, mafuta na mahitaji mengine mengi ya nyumbani). Napendelea kuuza reja reja...

Eneo hilo niweze pia kuwa nauza fresh juice na maziwa kwa kuwasambazia watu waliopo eneo hilo na jirani na duka (kwa hiyo uwepo wa vijiwe na mzunguko wa watu ni muhimu).

Nitatoa kifuta jasho kwa atakayenielekeza chimbo La kueleweka nisije kata mtaji wangu.

Eneo napendelea liwe mitaa ya Mbezi ya Kimara, mitaa ya Kimara, pia Goba japo Goba sio kipaumbele.

Nasisitiza kutoa chochote kwa atakayenipa ushirikiano wa eneo zuri na ikiwezekana frem kabisa.

Asanteni kwa ushirikiano.
Kumbe ulirudi

 
Back
Top Bottom