Natafuta mdhamini/mfadhili kwa masomo yangu

dolson masaki

Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
38
Reaction score
3
jamani naombeni nifanyeje nipata kurudi xkul nilihitimu kidato cha 4 2008 nikashindwa kuendelea kutokana na kukosa karo ya shule
 
naombeni msaada natokea familia maskini natafuta mfadhili niweze kurudi SHULE nitafanyeje?
 
mwanangu we tafuta pesa mwenyewe ujisomeshe nani atakudhamani acha usharobaro
 
uandishi wako unaonyesha kuwa kichwani hakuna shule.

Nini maana ya "xkul"

na wewe wakati wanaume wana-kuchakachua pale udom kabla huja-disko ndio ilikua akili.
 
Jaman kama huwezi kutoa ushauri bora uc comment kwani unanikatisha tamaa
 
Dogo,we endelea kusaka mshiko tu,achana na mambo ya shule,utapoteza muda bure.
 
Mkuu, Wadhamini ni vigumu kuwapata, jitahidi kutafuta ela kisha weka akiba ili uweze kudhamini.
 
Kama alivyosema Senetor, wewe sasa hivi tafuta pesa tu, kusoma kutakupotezea muda.
 
Naaomba uwe makini na ueleze kwa kina hilo suala lako. Unaposema unaomba ufadhili ili urudi shule haieleweki ni shule ya msingi, sekondari, chuo cha kawaida au chuo kikuu.Hata kiingereza ulichotumia kinatia shaka, bora ungetumia lugha ya kiswahili.
 
Jitahidi kueleza vizuri. Umeeleza kwa kifupi sana.
 
Kaka bora utafute noti maana hao wasomi wewe huwaoni huko mtaani hawana ishu?....ka vp kajifunze ufundi garage karo ni Tsh 0....
 
soma underground...then lipia private candidate kisha fanya mtihani......hussle free!
 
uandishi wako unaonyesha kuwa kichwani hakuna shule.

Nini maana ya "xkul"

watu wengine huwa wanajiaribia bila kujua. hapo hata huyo sponsor lazma ashtuke.
 
Hata kiingereza ulichotumia kinatia shaka, bora ungetumia lugha ya kiswahili.[/QUOTE]

Jamaa anatumia lugha hiyo ili ujue kuwa hasomi shule ya msingi bali yuko kwenye skuli kuanzia za kata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…