Natafuta miti ya matunda yafuatayo:

Natafuta miti ya matunda yafuatayo:

CHE GUEVARA-II

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2010
Posts
571
Reaction score
156
Ndugu wana JF, natumai hamjambo!
Naomba mnisaidie wapi naweza kupata miti ya matunda yafuatayo? Nahitaji angalau miti miwili katika kila aina.
Nahitaji mnisaidie kunielekeza nitakapozipata, contacts na if possible na bei zake:

(1)Zabibu (nyeusi na za kijani) - jumla miti minne
(2)Strawberry - miti miwili
(3)Zeituni - miti miwili
(4)Dates (tende) - miti miwili
(5)Apples (tufaa) - miti miwili
(6)Pears - miti miwili
(7)Pomegranate (komamanga) - miti miwili
(8)Mulberry (forosadi) - miti miwili
(9)Tangarine (chenza) - miti miwili
(10)Na miti ya matunda mengine mengi kadiri mtakavyoona yatanifaa, sana sana mimea inayostawi sehemu ya joto - nataka niipande Mtwara.

Nitashukuru.
 
Ngoja nami niisubiri maana mingine sijawahi hata kuiona maishani kama 'zeitoon'.
 
Straberry (mafurusadi) -

Miche mingi ya Matunda ipo sana Arusha na Lushoto sijui kwa hapa Dar.

Ngoja tusubiri
 
kama uko dar,nenda bonde la kawe kama unaelekea Tegeta(karibu na tangi bovu) yapo aina mbali mbali bei ni maelewano
 
kama upo dar nenda kurasini pale wapo radio utapata msaada zaidi
 
apple na pears kwa mTwara haitafaa. inahitaji sehemu za baridii. au kama unaitaka iwe kama mapambo tu!
 
Ndugu wana JF, natumai hamjambo!
Naomba mnisaidie wapi naweza kupata miti ya matunda yafuatayo? Nahitaji angalau miti miwili katika kila aina.
Nahitaji mnisaidie kunielekeza nitakapozipata, contacts na if possible na bei zake:

(1)Zabibu (nyeusi na za kijani) - jumla miti minne
Ukipata mtu kutoka Dodoma unaweza kuzipata. Ila zile seedless za kijani sidhani kama unaweza kuzipata hapa Tz

(2)Strawberry - miti miwili
Sidhani kama unaweza kuotesha strawberries Mtwara, ila nimeona zinauzwa Morogoro huwa zinatoka kule milimani juu ambako kuna baridi sana

(3)Zeituni - miti miwili
Unataka zeituni ipi, olives au ile yenye matunda ya manjano inayoitwa "Shajarati Fatma" kwa Zanzibar? Ikiwa ni hiyo ya pili basi ni rahisi kuatika mbegu na iko mingi katika maeneo ya pwani kama Tanga. Ama kwa olives huwa zinaota kwenye sehemu ya baridi na hasa maeneo ya Mediterranean sidhani kama unaweza kupata miti yake hapa Dar

(4)Dates (tende) - miti miwili
Chukua mbegu za tende mbili na uoteshe ni rahisi sana. Ukiona haioti jaribu kukwangua lile gamba la juu kwani baadhi ya mbegu hasa zile zenye gamba la nje gumu hulazimu kulikwangua au kuchemsha ili kuruhusu mche utoke.

(5)Apples (tufaa) - miti miwili
(6)Pears - miti miwili
Hii inahitaji baridi ili iweze kuzaa matunda. Miche yake utapata maeneo ya Iringa (Mufindi huko) au Lushoto Tanga

(7)Pomegranate (komamanga) - miti miwili
Hii unaweza kupata kwenye nursery za binafsi, au umuombe mwenye mti huo binafsi akuoteshee

(8)Mulberry (forosadi) - miti miwili
Hii miti ya porini kwa kwetu lakini unaweza kupata kwa watu binafsi

(9)Tangarine (chenza) - miti miwili
Michenza unaweza kupata kwenye nurseries nyingi lakini angalia unataka ya aina gani, ya mbegu au ambayo imefanyiwa budding? Ni vyema ukapata michenza ambayo imefanyiwa budding, yaani rootstock (kigogo) ni cha mlimau halafu imepandishiwa michenza. Hivyo utapata miche itayokuwa na ustahmilivu zaidi wa maradhi mbali mbali ya citrus.


(10)Na miti ya matunda mengine mengi kadiri mtakavyoona yatanifaa, sana sana mimea inayostawi sehemu ya joto - nataka niipande Mtwara.

Nitashukuru.

Che Guevara: Kuna miti uliyotaja ambayo sidhani kama itaweza kuzaa matunda katika hali ya joto kama hili, mfano strawberries. Jaribu kutembelea nursery ya SUA (horticulture) hapo zamani walikuwa wanauza miche aina tofauti tofauti.

Au, tafuta mtaalamu wa mambo ya nursery au mwenye nursery akuatikie miche unayotaka halafu utamlipa, kwani kuatika miche ya miti ina utaalamu wake.
 
Nawashukuru ninyi nyote mliochangia katika mada hii.
Nitafuata ushauri wenu!
Ngoja nijaribu tu na miti mingine hata kama ikitoa matunda mawili kwa mwaka poa tu (itakuwa sehemu ya mapambo pia).


''The revolution is not an apple that falls when it is ripe. You have to make it fall''
 
kwa kweli katika miti uliyouliza sijawahi sikia kama kuna miti ya zeituni hapa kwetu
 
Back
Top Bottom