Natafuta mke, awe mlevi (apende pombe)

Kheri Hansen

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2018
Posts
1,025
Reaction score
1,238
Hodi humu,

Ndugu zangu, mimi sasa ni rasmi nataka kuoa, nimeangalia sifa ambazo wanaume wenzangu huainisha, naona zimejaa unafiki; unakuta anasema nataka mke wa kuoa awe hivi, awe na kazi, sijui amesoma...kwakweli mimi naomba niseme tu ukweli, kama ni mawe mnipige.

Mimi nataka kuoa, sifa zote za kuwa mume wa mtu nimeshajiandaa, ninazo (makazi, ajira, upendo, kuwa tayari kulea, nk). sasa mbali na kwamba mwanamke ninayemhitaji na yeye awe na sifa k.v. upendo, kujiheshimu, n.k. Mimi nataka pia awe mlevi, yaani apende pombe, huyo naona tutaendana na tutakuwa marafiki wakubwa.

Nitampenda, nitamlinda, nitamhudumia, tukienda kulewa wote ntahakikisha silewi sana ili wote tusipotee njia ya kurudi nyumbani, pia mmoja awahi kuamka kuandaa supu ya kutoa hangover.

Kwa anayemjua dada aliyetayari kuolewa kwa ndoa halali, na anapenda pombe, please niPM.
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] nimeipenda hii...unafiki kando
 
Na ukimpata uturejeshee ripoti
 
Bora umejifungukia mapema
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…