Natafuta mshirika katika biashara - Nina Milioni 2 kama mtaji

Sudi jr

Senior Member
Joined
Aug 4, 2017
Posts
134
Reaction score
179
Habari ndugu zangu,

Natafuta mtu wa kushirikiana nae katika biashara ambayo tutaamua kwa pamoja kama washirika kufanya, binafsi nina mawazo ya biashara kadhaa na nina mtaji wa million 2 ila naitaji paternership.

Sifa za mimi;
-Wa kiume
-Elimu yangu ni shahada ya kwanza (BA.Ed)
-Sio mvivu wa kazi na najituma hasa
-Naishi Kibaha
-Mwaminifu sana, ila (sio mtu wa maneno mengi)

Sifa za mshiriki
-Awe mwaminifu sana
-Mchapa kazi kweli ikibidi hata usiku
-Awe anapatikana wakati wote wa majukumu
-Mkazi wa Dar es Salaam au Kibaha
-Awe na mtaji sio chini ya million 1.5.
-Jinsia yoyote ila mimi ni wa kiume, kama akiwa wa kiume itapendeza zaidi

Kama upo interested na wazo hili naomba tufanya mawasiliano PM then tutashare contact.
Ndugu zangu katika ujenzi wa nchi.
 
Nimeiona hii thread nimekimbia mbio kuangalia ni mshirika yupi anahitajika. Naona hapa tatizo siyo mshirika -- tatizo kubwa hapa ni huo mtaji. Mshirika anaweza kuwa na vigezo karibia vyote, lakini akaangukia pua kwenye mtaji. Vuta subira washirika watakuja mkuu, kila la heri.
 
Niko Dar, naomba uni PM wazo ulilo nalo na fursa uliyoiona hapo kibaha tuyajenge...
 
sema wazo kwanza ulilo nalo ili tujue kama tunakupigia tuna anzia wapi
 
Food and drinks, (cartering)
Yaani kutengeneza, packaging, kuuza, na kusambazaa vyakula na vinywaji ambavyo vinatokana na matunda, pamoja na asali.
 
Niko Dar, naomba uni PM wazo ulilo nalo na fursa uliyoiona hapo kibaha tuyajenge...
Food and drinks, (cartering)
Yaani kutengeneza, packaging, kuuza, na kusambazaa vyakula na vinywaji ambavyo vinatokana na matunda, pamoja na asali.
 
[emoji121]
MKUU,

HII CHANCE NAIHITAJI SANA,
ILA MTAJI WANGU NI LAKI NNE.

HIVYO NI-PM TUANZE MICHAKATO FASTA,
HUKO MBELENI MTAJI UKIKUA TUTASAWAZISHA TU USIHOFU.
 
Karibu mm nipo DSM mm mtaji wangu ni ardhi, km ipo fresh nicheck
 
Food and drinks, (cartering)
Yaani kutengeneza, packaging, kuuza, na kusambazaa vyakula na vinywaji ambavyo vinatokana na matunda, pamoja na asali.
Hii biashara ya chakula huwa haidanganyi..na profit margin yake ni kubwa, cha kuzingatia ni location,ubora wa chakula (hapa hata kama location si nzuri), na bei (hasa usawa huu wa magu)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…