Nataka kuacha kazi nisimamie biashara yangu lakini naogopa-naomba ushauri

Nataka kuacha kazi nisimamie biashara yangu lakini naogopa-naomba ushauri

FADHILIEJ

Senior Member
Joined
Nov 5, 2010
Posts
132
Reaction score
18
Wana JF nimekuwa muajiriwa kwenye NGO Moja kwa takriban miaka kumi.
Imefika wakati nataka kuacha ili nipate muda wa kutosha kusimamia biashara yangu japo ni ndogo.
Kinachonisumbua ni hofu ya kuacha kazi.naombeni nishaurini nitumie mbinu gani?
 
Tatizo unang'atwa na hofu. Angalia kama mapato ya biashara yako in terms of net profit kwa mwezi ni zaidi net salary yako. kwa mwezi. Cha pili angalia opportunity cost. Uko huru zaidi upande gani. Pia angalia uendelevu wa biashara yako kwa miaka 5 ijayo kama itakuwepo. Angalia una ujuzi gani na hiyo biashara pamoja na washindani wako ktk soko. Last but not least angalia uthubutu wako katika kujiajiri-entrepreneural ability. Hii ni rasilimali muhimu sana. Baada ya hapo kata shauri
 
miaka kumi unafanyaa nini yotee kwanza umechelewa na bado una nafasi mkuu kamua kivyako
tuko nyuma yako
 
Haupo tayari, endelea na kibarua chako hapo NGO mkuu usitafute presha bure. In short you are not a 'business-type' guy, you are a 'salary-type' guy
 
pamoja na ushauri wa mkuu hapo chini kama biashara yako ina wateja wa uhakika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo na na kama inaweza kupanuka kama ikinderezwa bora kusimamia biashara.
lakini pia ni ukuweka detail za kutosha hapa, utopata ushauri wa maana au kukusaidia


Tatizo unang'atwa na hofu. Angalia kama mapato ya biashara yako in terms of net profit kwa mwezi ni zaidi net salary yako. kwa mwezi. Cha pili angalia opportunity cost. Uko huru zaidi upande gani. Pia angalia uendelevu wa biashara yako kwa miaka 5 ijayo kama itakuwepo. Angalia una ujuzi gani na hiyo biashara pamoja na washindani wako ktk soko. Last but not least angalia uthubutu wako katika kujiajiri-entrepreneural ability. Hii ni rasilimali muhimu sana. Baada ya hapo kata shauri
 
Wasiwasi ni akili mpendwa.
Ni vema ukaangalia faida unazopata kibaruani kwako na biashara pia. Uhakika ni muhimu juu ya mwendelezo wa biashara yenyewe isije kuwa ni ya msimu tu.
Endelea kutumia kazi kama dhamana kama haikubani sana katika shughuli zako binafsi. Ukipata faida kotekote huoni kuwa inalipa zaidi?
 
Kuna Professor wangu mmoja amenifundisha enterpreneurship and Innovation alituambia darasani hivi. Alifanya kazi makampuni makubwa mf IBM nk. akwa anasema niligundua siwezi kuwa President akaacha, akaend akampuni nyingine vilevile akaacha kwa sababu hiyohiyo. Alipokuwa na umri wa miaka 37 akaamua kuacha kazi zote akaanza shughulizake binafsi. Na toka wakati huo hajawahi kuludi nyuma. NA sasa biashara zake zina mtaji wa Dola Ml.3 za kimarekani. almost 4.5 billion kwa hela za madafu.

Sasa basi angalia Business Plan yako for the next 3 to 5 years. Tengeneza Income Statement Projection for that period.. na kwa kuwa umekuwa nayo tayari haitakusumbua kujua Annual Revenue generation na expenses zake. Pili angalia Balance Sheet yako inasemaji in terms of equity( chako ni kiasi gani na Benki ama business patner wako) Alafu mwisho Cash flow kwa kipindi chote cha miaka utayoamua.

Hii itakusaidia kujua ni faida kiasi gani unapata kwa mwaka, hata kwa mwezi. Then hapo utakuwa na uhakika wa kujua kuwa biashara itaendelea ama lah.. Kinachoshinda wengi ni kutosimama kwa misingi ya biashara aliyoweka mwenyewe.

UKiweza kuwa na business plan nzuri na ukaisimamia basi hutokuwa na hofu ya kuacha hiyo kazi unayofanya

Option nyingine unaweza endelea na kazi yako lakini ukai monitor kwa results produced kwa uliowaajiiri but business plan ni muhimu mkuu.

All the best
 
niliwahi kusoma katuni kwenye newsweek zamani kidogo. kanuni ya kwanza ya kujitegemea kwenye soko huria ni kuruka toka kwenye ndege angani ukiwa na parachuti. lazima uiache ndege (sehemu salama) kwanza. halafu ukishaanza kudondoka ndo unafungua hilo parachuti lililoko mgongoni kwako. kwanza huna uhakika kama litafunguka. lakini pia huna uhakika litakapofunguka litakupeleka mpaka wapi. kwa hiyo hofu ya yote hayo lazima uwe nayo kabla ya kuacha kazi ujitegemee. na katika kuweka mambo sawa ndo maana unashauriwa kutazama mambo mengi kwa marefu na mapana. ila kikubwa sana cha kutambua ni kuwa huwezi kuwa tajiri kwa kuajiriwa...haipo. ukitaka kuwa tajiri lazima ujiajiri!
 
Nashukuru kwa mawazo yote mazuri,
nimepaata idea mpya kwamba labda nichukue likizo isiyo na malipo kwa miezi mitatu plus annual leave nisome ramani na kuondoa hofu,kikieleweka basi niachie ngazi,

mnasemaje?
 
fanya vyote mpaka hapo ajira itakapokoma, sababu biznes yako imetokana na ajira, ukiacha ajira bizness ina bankrupt sure nakueleza. Continue doing reseach on that.
 
Nashukuru kwa mawazo yote mazuri,
nimepaata idea mpya kwamba labda nichukue likizo isiyo na malipo kwa miezi mitatu plus annual leave nisome ramani na kuondoa hofu,kikieleweka basi niachie ngazi,

mnasemaje?

Hii ndiyo naona ni sawa maana inaonekana hujawi kutokuwa muajiriwa kabisa, pia angalia uwezekanao wa kutotumia mshahara wako kabisa kwa miezi sita ukitegemea hiyo biahsara tu, I mean iwe inajizungusha yenyewe na kuweza kukupa mahitaji yako na faida kiasi, ili ukiacha usiwe na hofu. hat ahiyvo muda huo ni mfupi na inaweza kukupa picha nzuri au mbaya kwa iyo angalia other factors ambazo zimechangia kwa kipindi utakapokuwa unafanya evaluation mfano kupanda na kushuka shilingi etc.
 
Angalia kipato kama biashara yako inaingiza faida kiasi sawa na mshahara wako unaweza kuacha na kujiunga na biashara yako kama unaweza kuishi bila kuchukua mshahara wako zaidi ya miezi 6 unaweza kuacha kazi vinginevyo endelea na kazi ukiacha utajuta.
 
Wasiwasi ni akili mpendwa.
Ni vema ukaangalia faida unazopata kibaruani kwako na biashara pia. Uhakika ni muhimu juu ya mwendelezo wa biashara yenyewe isije kuwa ni ya msimu tu.
Endelea kutumia kazi kama dhamana kama haikubani sana katika shughuli zako binafsi. Ukipata faida kotekote huoni kuwa inalipa zaidi?

"Uoga wako ndio umaskini wako!!" - Kanyagio (JF Senior Expert Member)
 
mwisho wa siku lazima urudi kujiaajiri ....hata pensheni huisha kama hujajiandaa...... tafakari chukua hatua mapema

be strong and decide
 
Haupo tayari, endelea na kibarua chako hapo NGO mkuu usitafute presha bure. In short you are not a 'business-type' guy, you are a 'salary-type' guy

mkuu umenena. Huyu jamaa bado kwenye kujiajiri. Nadhani endelea na kazi yako na tafuta muda wa kujifunza zaidi kuhusu hiyo biashara mpaka hapo utakaporidhika kwamba hiyo biashara inaripa. Binafsi nilijitoa muhanga nikaacha kibaru na kujikita kwenye kikampuni changu.sasa si haba nimetoka kwenye sole proprietor naelekea kuwa limited
 
Nashukuru kwa mawazo yote mazuri,
nimepaata idea mpya kwamba labda nichukue likizo isiyo na malipo kwa miezi mitatu plus annual leave nisome ramani na kuondoa hofu,kikieleweka basi niachie ngazi,

mnasemaje?

mkuu ... kwenye ujasiriamali usithubutu kujaribisha au kufanya vitu mguu nje mwingine ndani .... fanya maamuzi ... after all kwenye ujasiriamali siyo siku zote mambo ni mazuri ..kuna up and downs ...
 
Biashara ni kitu kinachoweza kujiendesha chenyewe ndani ya mwaka mzima bila uwepo wako. Sasa nionavyo mimi hapo utakuwa umebadirisha ajira sio kusimamia biashara.
Usiache kazi.
 
Tumia hesabu ifuatayo:

Chukua mshahara wako kwa mwezi gawanya kwa 30 then utapata kiasi gani kwa siku, then ringanisha na pato lako la siku kwenye biashara yako.

Kama tofauti yake ni 5% plus or minus then upo safi, hakuna haja ya kuogopa.

Angalia product yako kama ina demand kubwa kwenye current na future market, if YES then mwaga manyanga kazini - chukua nusu NSSF yako baada ya miezi sita wekeza kwenye biashara.

Baada ya miaka 5 utakuwa mbali sana- Kama mkeo anafanya kazi we mwache aendelee huko usimwachishe.

Tatizo wengi ni woga wa kuacha kazi.
 
Kuna Professor wangu mmoja amenifundisha enterpreneurship and Innovation alituambia darasani hivi. Alifanya kazi makampuni makubwa mf IBM nk. akwa anasema niligundua siwezi kuwa President akaacha, akaend akampuni nyingine vilevile akaacha kwa sababu hiyohiyo. Alipokuwa na umri wa miaka 37 akaamua kuacha kazi zote akaanza shughulizake binafsi. Na toka wakati huo hajawahi kuludi nyuma. NA sasa biashara zake zina mtaji wa Dola Ml.3 za kimarekani. almost 4.5 billion kwa hela za madafu.

Sasa basi angalia Business Plan yako for the next 3 to 5 years. Tengeneza Income Statement Projection for that period.. na kwa kuwa umekuwa nayo tayari haitakusumbua kujua Annual Revenue generation na expenses zake. Pili angalia Balance Sheet yako inasemaji in terms of equity( chako ni kiasi gani na Benki ama business patner wako) Alafu mwisho Cash flow kwa kipindi chote cha miaka utayoamua.

Hii itakusaidia kujua ni faida kiasi gani unapata kwa mwaka, hata kwa mwezi. Then hapo utakuwa na uhakika wa kujua kuwa biashara itaendelea ama lah.. Kinachoshinda wengi ni kutosimama kwa misingi ya biashara aliyoweka mwenyewe.

UKiweza kuwa na business plan nzuri na ukaisimamia basi hutokuwa na hofu ya kuacha hiyo kazi unayofanya

Option nyingine unaweza endelea na kazi yako lakini ukai monitor kwa results produced kwa uliowaajiiri but business plan ni muhimu mkuu.

All the best

duh hapo kwenye blue ndiyo kikwazo, wengi wetu business plan zetu ni vichwani kwetu. mambo ya kuandika andika as if unaenda kuomba mkopo benki duh.
 
Mkuu niliacha kazi 7 years a go kusimamia biashara yangu na sikuwa na willing ya my wife and my mother, but I decided it. Ni ngumu kwa kiasi fulani kwani 3 months down the line mambo yaliharika sana baada ya kuugua na vijana niliowaajiri kunichakachua. Sikukata tamaa nilipigana kiume na ninavyo andika niko napambana na my wife ameamua kujoin the boat from last year. Hivyo karibu sana mzee uwanjani pambana na utafanikiwa. Kwa taarifa tu nilipoamua kuacha my gross salary it was aroung 6.7m
 
Back
Top Bottom