Nataka kuanza biashara ya kuleta mtindi Dar kutoka nyanda za juu kusini

ipyax

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
4,247
Reaction score
6,578
Kama heading inavyo sema ,katika harakati zangu za kusaka pesa nimepata wazo la kufanya hii biashara. Huku niliko maziwa yanapatikana kwa wingi sana kwa bei ya chini,mpango wangu ni kununua maziwa fresh na kuyagandisha mwenyewe kisha kusafirisha mpaka dar.

Ningependa kupata maoni na ushauri kutoka kwenu kuhusu changamoto, vikwazo,fursa nk kwenye hii kazi. Target yangu ni angalau kuleta Lita 200 kila wiki sokoni kwa kuanzia huku nikitegemea demand kuongezeka mpaka angalau Lita 1000 kwa wiki.

Mchango wenu na ushauri utapokelewa kwa mikono miwili.
 
Hata mimi nakuunga mkono kwenye izo arakati ila vipi utafanya packaging mwenyewe au utachukuwa viwandani. Mi nipo dar ila nafanya arakati zangu iringa najuwa ASas nafanya packeg vizuri unawez ukaanz nao
 
Hata mimi nakuunga mkono kwenye izo arakati ila vipi utafanya packaging mwenyewe au utachukuwa viwandani. Mi nipo dar ila nafanya arakati zangu iringa najuwa ASas nafanya packeg vizuri unawez ukaanz nao
Kufanya packaging ya kisasa ni gharama lakini pia yahitajika vibali toka tfda,osha,tra nk. Mwanzo nitafanya kwenye dumu za lita 5 mpaka biashara itakapo kua ndipo nitaongeza aina tofauti za vifungashio.
 
Kufanya packaging ya kisasa ni gharama lakini pia yahitajika vibali toka tfda,osha,tra nk. Mwanzo nitafanya kwenye dumu za lita 5 mpaka biashara itakapo kua ndipo nitaongeza aina tofauti za vifungashio.
Haina shida kiongoz mungu hatakuongoza ni pm kama hautojali tushare idea mi mwenyewe na wazo lakuchukuwa samaki wabichi toka mtera kuleta hapa dar
 
hahahahahaha hapo bado hujakutana na vikwazo vya maagent wa malaika mkuu, TRA,TRAFFIC POLICE,ROAD BLOCKS,MABWANA/MABIBI AFYA
 
Haina shida kiongoz mungu hatakuongoza ni pm kama hautojali tushare idea mi mwenyewe na wazo lakuchukuwa samaki wabichi toka mtera kuleta hapa dar
Pamoja mkuu,nitumia no yako pm ntakutafuta tufanye kushare mawazo na changamoto.
 
hahahahahaha hapo bado hujakutana na vikwazo vya maagent wa malaika mkuu, TRA,TRAFFIC POLICE,ROAD BLOCKS,MABWANA/MABIBI AFYA
Tukiogopa vikwazo na changamoto basi tutabaki na umaskini wetu mpaka kufa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…