Nataka kufanya biashara ya kusupply mchele mashuleni na vyuoni

Mkuu Lazima Uwe Na Mtaji Mkubwa Sana
Serikali Huchelewa Sana Kulipa Wazabuni
Sasa Unaweza Kufanya Supply January
Ukalipwa January Nyingine


Kwasasa Nadhani Tender Ndiyo Inaamua
Enzi Za Nyuma Ungekwenda Chuo/Shule Yoyote
vipi kwa upande wa shule binafsi? bila shaka wao hawachelewi kulipa hela

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baba utafilisika bure kama huna mtaji. Kama umesoma sekondari nadhani utakuwa umeshawahi sikia Mzabuni Kagoma baada kuleta chakula sababu hajalipwa.
 
Hii biashara ni nzuri na inalipa vizuri sana. Ila kupata hizi tender sio kitu rahisi, lazima ujidhatiti haswa, ikiwezekana hata ukubali kula na wenye mamlaka....maana
wengi wao huwa na tamaa tamaa nyingi, kukupa tender anaona kama utapata sana.

Kwa kuanza nakushauri, anza kwa kutembelea private schools. Maana ndio soko bora lililobakia kwa biashara hiyo, kwa sababu sio wacheleweshaji wa malipo kabisa. Wapo wanaolipa kwa trip, week na kwa mwezi.....ni maelewano yenu tu.

Angalizo.

1: Hakikisha una mtaji wa kutosha.
2: Uwe na store.
3: Huo mchele ni vema ukachukua kwa wingi kutoka kwa wakulima na wala sio kwa walanguzi masokoni.(kuna maana kubwa kwenye hili).
4: Pia uwe na usafiri like kirukuu, pikipiki au bajaji utakayoitumia kufanya supply yako.
5: Mwisho, make sure unakuwa na vitabu vizuri vya deliver notes na invoice, kwa ajili ya uendeshaji wa biashara yako.

I wish you all the best ndugu.
Welcome.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
barikiwa kwa kumjenga mdogo wetu.
 
Soko lipo,cha muhimu ni mtaji wako na uvumilivu wa kusubiria kulipwa.Kama una uwezo wa kulisha mwaka mzima,na kusubiria malipo baada ya miaka miwili bila kuathirika kiuchumi,nakushauri uende shule yoyote ile ukatangaze nia;natumaini utapata.
 
Kuna shangazi yangu alaikuwa anapeleka matunda shule fulani hapa Arusha amebidi aache........kikubwa kuwa na mtaji mrefu alafu iyo ela usiitegemee ukishapeleka maana sio ya kuipigia mahesabu kabla ujaishika mkononi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…