Wapo viumbe hai (wanyama) walioumbwa kipekee na hawajamiiani kama njia ya kudumisha uzao. Wanyama (viumbe) wa namna hiyo hawakuumbwa jike na dume bali wameumbwa wa aina moja mwenye mbegu za kike na kiume. Sivyo walivyo tausi. Hawa wameumbwa dume na jike. Tausi dume kwa kiingereza anaitwa "Peacock" na tausi jike kiingereza anaitwa "Peafowl".
Tausi dume mara nyingi ndiye aliyekivutio kikubwa kwa wanadamu hasa kwa uwezo wake wa kutandaza manyoya yake ya mkia ambayo ni marefu na yana michoro ya rangi nzuri mno, nichoro ambayo binadamu wameiiga mara nyingi katika mavazi hasa ya akima dada/mama. Tausi huyu dume hutandaza manyoya yake kwa sababu kabla ya kupandana lazima tausi "wachezo ngoma", au kwa maneno mengi wanafanya vitendo ambavyo vimeitwa na wanadamu "Peacock mating dance", na shughuli hii hasa hufanywa na tausi dume kuwavutia/kuwaita majike ili wapandane. Tukio hili la dume kuwaita majike ili awapande kwa hakika ni kivutio kikubwa mno kwa wanadamu na kwa kweli uzuri na umuhimu wa kufuga tausi uko katika umbo analoonekana nalo tausi dume wakati huo. Hata lile umbo la tausi wakiwa katika tendo la kupandana ni kivutio kikubwa kwa watazamaji. Fuata link hiyo hapo chini uone tausi wakipandana.
Peacocks mating - YouTube