Kirikou Wa Kwanza
JF-Expert Member
- May 24, 2013
- 3,564
- 1,991
Mimi ni Kijana, nina miaka 23; nataka kurudia form4. Wadau mnanishauri vipi?
Si ukasomee ualimu tu.
Hebu nipe matokeo yako ya mwanzo kwanza ndo nikushauri.
Kwa karne hii m2 wangu umr umekwenda tafuta hata njia nyingine kulko kuyarudia matapish yako
Rudia!
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
kama maisha yako yapo safi rudia ila kama ndo pamoja kwenye dimbwi la umasikini tafuta sehemu nyingine.UMASIKINI UNAFUPISHA MAISHA.
Kiufupi nina dv four ya 29
Kwa kukusoma haraka haraka lengo lako wewe ni kusoma form v (nimekosea mkuu?kama nimekosea niambie), hizo maksi zako ndio zimegota hapo kikubwa ni kuangalia vyuo vinavyotoa Certificate ya fani ambayo unataka uje uwe kwa level ya juu siku za usoni kwani ukirudia form 4 mfano ukichemsha zaidi ya hapo itakuaje plus muda uliopoteza. Tafuta chuo piga certificate kisha nenda Diploma baada ya hapo ukiwa vizuri utaendelea na masomo ya juu maana muda huo unaorudia form 4 tayari unakuwa umepata certificate, (assuming kama kwa kurudia kwako umefaulu maana yake tena muda ambao unasoma kidato cha 5 na 6 ndio muda ungetumia kwa kusoma Diploma ila wewe unakuwa na benefit ya tayari una fani yako). Elimu sio lazima ufike form 5 na 6 kuna mazingira kama ikigoma unatakiwa uwe na plan B na ndio maana vikawepo vyuo vya kada mbalimbali kikubwa ni wewe kujirekebisha uingiapo chuo ili makosa uliyoyafanya secondari yasijirudie
Mkuu Mwamini Yesu kwan anaweza yote. So ukirudia utafanya vizur zaidi.
Kiufupi nina dv four ya 29
Kwa kukusoma haraka haraka lengo lako wewe ni kusoma form v (nimekosea mkuu?kama nimekosea niambie), hizo maksi zako ndio zimegota hapo kikubwa ni kuangalia vyuo vinavyotoa Certificate ya fani ambayo unataka uje uwe kwa level ya juu siku za usoni kwani ukirudia form 4 mfano ukichemsha zaidi ya hapo itakuaje plus muda uliopoteza. Tafuta chuo piga certificate kisha nenda Diploma baada ya hapo ukiwa vizuri utaendelea na masomo ya juu maana muda huo unaorudia form 4 tayari unakuwa umepata certificate, (assuming kama kwa kurudia kwako umefaulu maana yake tena muda ambao unasoma kidato cha 5 na 6 ndio muda ungetumia kwa kusoma Diploma ila wewe unakuwa na benefit ya tayari una fani yako). Elimu sio lazima ufike form 5 na 6 kuna mazingira kama ikigoma unatakiwa uwe na plan B na ndio maana vikawepo vyuo vya kada mbalimbali kikubwa ni wewe kujirekebisha uingiapo chuo ili makosa uliyoyafanya secondari yasijirudie
Mimi ni Kijana, nina miaka 23; nataka kurudia form4. Wadau mnanishauri vipi?
Usipojirekebisha uandishi wako hasa kama ulivyoandika heading utarudia hadi ukome na matokeo yataendelea kubaki mabaya...