Nataka kuuliza imekuwaje kuwaje mpaka wakoloni walituacha huru?

Nataka kuuliza imekuwaje kuwaje mpaka wakoloni walituacha huru?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Ngoja In Shaa Allah niingie Maktaba:

1566502768214.png

Uingereza ilikuwa ikitawala Tanganyika chini ya kifungu 76 na 77 cha Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Kama mamlaka tawala Uingereza ilitarajiwa kuanzisha na kuendeleza maendeleo ya siasa, uchumi na ya kijamii ya Tanganyika hadi kufikia wakati ambao watu wake wangekuwa tayari kujitawala. Lakini Waingereza walifanya khiyana na hawakutimiza ahadi hiyo. Walijihusisha na kulinda maslahi yao wenyewe ya kikoloni na yale ya watu weupe wachache na wakaendelea kuwapuuza Waafrika waliokuwa wengi na wenye nchi.

Ili Waafrika waweze kuikabili hali hii ilikuwa muhimu wawe wamoja kupambana na ukoloni na kwa ajili hii mwaka wa 1929 wakaunda African Association kwa nia ya kuwaleta Waafrika pamoja. Katika waasisi hawa kutoka Gerezani walikuwa Kleist Sykes (Katibu Muasisi) na Ibrahim Hamisi wote wakiishi Kipata Street. Lakini harakati khasa zilipamba moto baada ya Vita Kuu ya Pili pale mwaka wa 1950 vijana walipoamua kupindua uongozi wa TAA ambao Rais alikuwa Mwalimu Thomas Plantan akiishi Mtaa wa Masasi Mission Kota na Katibu Clement Mtamila akiishi Kipata. Walioongoza mapinduzi haya walikuwa Abdul Sykes na Hamza Mwapachu. Katika uchaguzi uliofuatia baada ya mapinduzi haya pale Makao Makuu ya TAA New Street Dr. Vedasto Kyaruzi akachaguliwa Rais na Abdul Sykes Katibu.

Mwaka huo TAA ikaunda TAA Political Subcommittee ambayo wajumbe wake walikuwa Dr. Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Steven Mhando, Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na Said Chaurembo. Kamati hii hadidu zake za rejea ilikuwa kushughulika na mambo yote ya siasa ndani ya TAA. Kwa msaada wa Earle Seaton ambae alikuwa rafiki yake Abdul huyu alikuwa mwanasheria kutoka kisiwa cha Bermuda TAA walianza kufanya mawasiliano na UNO kwa nia ya kutaka UNO iharakishe kupitia Kamati ya Udhamini wa Makoloni mchakato ambao utawaweka Waafrika wa Tanganyika katika hali ya kupewa uhuru wao. Hii Political Subcommittee ikapeleka kwa Gavana Twinig mapendekezo yake ya hali ya siasa Tanganyika na jinsi wananchi wanavyotaka nchi yao itawaliwe kufikia kupewa uhuru wake mwaka wa 1963.

Lakini viongozi hawa wa TAA walikuwa wanajua kuwa haiwezekani kudai uhuru chini ya TAA na ili kudai uhuru ni lazima wawe na chama cha siasa. Mazungumzo ya fikra hii yalianza mwaka wa 1951 kufanyika baina ya Abdul Sykes na Chief Kidaha Mwakaia wa Siha ambae alikuwa mjumbe wa LEGCO ikitegemewa Chief Kidaha ataingia TAA atachaguliwa Rais na TANU itaundwa kwenye Mkutano wa Mwaka wa TAA. Haya mazungumzo hayakufanikiwa.

Ndipo Hamza Mwapachu akaja na fikra ya kwa Abdul Sykes ya TAA kumtia Nyerere katika uongozi wa TAA New Street hii ilikuwa 1952 Nyerere alipotoka masomoni Uskochi na akaja Pugu kama mwalimu wa shule. Hadi kufikia mwaka wa 1953 mipango hii ikawa imekamilika pale Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe walipokwenda kwa Hamza Mwapachu Nansio, Ukerewe Abdul akitaka kupata kauli yake ya mwisho kutoka kwa Mwapachu kuhusu kumuingiza Nyerere kwenye nafasi ya urais wa TAA. Mwapachu alithibitisha kauli yake na katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 Ukumbi wa Arnautoglo Nyerere akagombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes na Nyerere akashinda. Mwaka wa 1954 katika Mkutano wa Mwaka wa TAA wajumbe 17 wa mkutano ule wakaunda TANU kama Hamza Mwapachu na Abdul Sykes walivyopanga.

TANU ikatangaza kuwa wameunda chama hicho kwa madhumuni ya kudai uhuru wa Tanganyika kiongozi wa harakati hizo akiwa Julius Nyerere. Mwaka wa 1955 Nyerere akaenda UNO kuhutubia Baraza la Udhamini akidai uchaguzi wa kura moja mtu mmoja katika LEGCO Baraza la Kutunga Sheria. Mwaka wa 1957 Nyerere akafanya safari ya pili UNO. Mwaka wa 1958 serikali ikaamua ufanyike uchaguzi ambao wajumbe watachaguliwa kwa rangi zao - Wazungu, Waasia na Waafrika. Uchaguzi ukafanyika na TANU ikashinda viti vyote. Mwaka wa 1960 Tanganyika ikapata madaraka na 1961 uhuru kamili.
 
sijawahi kuchoka kukusoma mzee wangu ila umeniacha na kiu mjukuu wako...
kikubwa ninacho jifunza ni kuwa ukolon bado upo ila upo ukoloni wenye jina jipya...na si mwingine ni "ukoloni mambo leo"
tunatawaliwa kifikra, uchumi na hata kimaendeleo na viashilia vinavyoashiria kuwa sisi ni watumwa vipo vingi vingene ukiandika utaanza kutafutwa na kubambikiwa kesi za uhaini...cha msingi ni kuendelea kuliziba hili bakuli lenye meno..
 
sijawahi kuchoka kukusoma mzee wangu ila umeniacha na kiu mjukuu wako...
kikubwa ninacho jifunza ni kuwa ukolon bado upo ila upo ukoloni wenye jina jipya...na si mwingine ni "ukoloni mambo leo"
tunatawaliwa kifikra, uchumi na hata kimaendeleo na viashilia vinavyoashiria kuwa sisi ni watumwa vipo vingi vingene ukiandika utaanza kutafutwa na kubambikiwa kesi za uhaini...cha msingi ni kuendelea kuliziba hili bakuli lenye meno..
Ukoloni hauto isha kamwe.Jitihada za kutafuta uhuru ni endelevu.Na kwa sasa tuna ukoloni wa aina mpya ambao hauna tofauti na ule wa wazungu
 
Pia inawapatia sifa baadhi ya watu wasizostahiki, badala ya lawama kiasi hiki.
Sajor...
Uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961 ulikuja na changamoto moto mpya za kuwa huru
na ikazuka hamu ya kutaka kujua nani na nani walikuwa waasisi wa harakati za kudai
uhuru na ni kundi lipi lililojitolea zaidi katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uasisi wa TANU ukawa ni ''the ultimate prize,'' yule jina lake au majina yao yatakachorwa
katika kikombe cha ushindi huu yatadumu daima katika historia ya Tanganyika.

Kuitafiti historia ya TANU si kazi kubwa hata kidogo.

Watafiti wote wanakubaliana kuwa TANU asili yake ni African Association na waasisi wake
wote wanafahamika vyema.

Mtafiti anaweza kuyapata majina haya katika: Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, katika kitabu alichohariri John Iliffe (Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, uk. 95-114.

Haya majina yamo katika mswada alioacha Kleist Sykes katibu muasisi wa African Association ambao aliandika kabla hajafariki mwaka wa 1949 na mjukuu wake Aisha ''Daisy' Sykes' akiwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki, Dar es Salaam mwaka wa 1968 akawasilisha kama seminar paper na iko katika Maktaba ya Chuo Kikuu Dar es Salaam sehemu iitwaya East Africana.

Bahati mbaya sasa baada ya uhuru kupatikana historia hii iliyoandikwa na Kleist Sykes katika
mswada wake na mjukuu wake Daisy akaja kuufikisha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara
ya Historia ikawa haipendezi kwa badhi ya viongozi wa TANU na sababu ni kuwa wao hawataweza kamwe kuwa washindi wa ile ''ultimate prize,'' ya kuwa waasisi wa harakati za uhuru kutoka African Association chama kilichokuja kuzaa TANU.

Hapa ndipo kwa ushawishi wa viongozi hawa ikawa historia ya uhuru wa Tanganyika inaanza mwaka wa 1954 ikijaribiwa kufutwa historia ya African Association.

Tusimame hapa kwa sasa...
Ultimate prize:
''...something very important or valuable that is difficult to achieve or obtain...''
 
Sajor...
Uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961 ulikuja na changamoto moto mpya za kuwa huru
na ikazuka hamu ya kutaka kujua nani na nani walikuwa waasisi wa harakati za kudai
uhuru na ni kundi lipi lililojitolea zaidi katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Uasisi wa TANU ukawa ni ''the ultimate prize,'' yule jina lake au majina yao yatakachorwa
katika kikombe cha ushindi huu yatadumu daima katika historia ya Tanganyika.
Kuitafiti historia ya TANU si kazi kubwa hata kidogo.
Watafiti wote wanakubaliana kuwa TANU asili yake ni African Association na waasisi wake
wote wanafahamika vyema.
Mtafiti anaweza kuyapata majina haya katika: Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, katika kitabu alichohariri John Iliffe (Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, uk. 95-114.
Haya majina yamo katika mswada alioacha Kleist Sykes katibu muasisi wa African Association ambao aliandika kabla hajafariki mwaka wa 1949 na mjukuu wake Aisha ''Daisy' Sykes' akiwa mwanafunzi Chuo Kikuu Cha Afrika ya Mashariki, Dar es Salaam mwaka wa 1968 akawasilisha kama seminar paper na iko katika Maktaba ya Chuo Kikuu Dar es Salaam sehemu iitwaya East Africana.
Bahati mbaya sasa baada ya uhuru kupatikana historia hii iliyoandikwa na Kleist Sykes katika
mswada wake na mjukuu wake Daisy akaja kuufikisha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara
ya Historia ikawa haipendezi kwa badhi ya viongozi wa TANU na sababu ni kuwa wao hawataweza kamwe kuwa washindi wa ile ''ultimate prize,'' ya kuwa waasisi wa harakati za uhuru kutoka African Association chama kilichokuja kuzaa TANU.
Hapa ndipo kwa ushawishi wa viongozi hawa ikawa historia ya uhuru wa Tanganyika inaanza mwaka wa 1954 ikijaribiwa kufutwa historia ya African Association.
Tusimame hapa kwa sasa...
Ultimate prize:
''...something very important or valuable that is difficult to achieve or obtain...''
Safi Sana,
vijana inabidi wajiongeze, watafiti na kusoma ilikuweza kupata ukweli na uhalisia wa taifa lao.

Manufaa na hasara za kumuondosha Muingereza.
 
Safi Sana,
vijana inabidi wajiongeze, watafiti na kusoma ilikuweza kupata ukweli na uhalisia wa taifa lao.

Manufaa na hasara za kumuondosha Muingereza.
Sajor...
Kwa miaka mingi historia hii ilipotea na ikawa hakuna anaeijua hata chembe yake
ingawa seminar paper ya Daisy ilikuwapo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam toka
mwaka wa 1968.

Mwaka jana katika kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha Abdul Sykes, Daisy aliandika
makala ya kumkumbuka baba yake.

Kuna vipande katika makala ile kwa hakika vinavutia sana.
Mfano hiki hapo chini:

''Lakini kile ambacho kimeathiri fikra zangu na kubakia na mimi katika kumbukumbu zangu ni kufika pale nyumbani kwa uongozi wa juu wa Waafrika kabla ya uhuru, machifu kutoka makabila mbalimbali ya Tanganyika na viongozi wa vyama vya wazalendo vilivyokuwa ndiyo vinainukia, viongozi wa vyama vya wafanyakazi na wafanyakazi Waafrika katika wa serikali ya kikoloni.

Kutokana na hadhi hii ya baba yangu na umaarufu wake na kule kupenda kukirimu watu, nikawa si mgeni kwa machifu mashuhuri na nikawa nawahudumia walipokuwa mara nyingi wakija nyumbani.

Wageni hawa mashuhuri waliokuwa wakija nyumbani ni pamoja na Mangi Mkuu Thomas Marealle, Machifu Abdiel Shangali, John Maruma kutoka Moshi, Adam Sapi Mkwawa kutoka Iringa, Kidaha Makwaia kutoka Usukuma, Abdallah Fundikira, Harun Msabila Lugusha kutoka Tabora, Humbi Ziota kutoka Nzega, Michael Lukumbuzya kutoka Ukerewe na Patrick Kunambi kutoka Morogoro na wengine wengi.

Hawa machifu kwa kawaida walikuwa wakija na wake zao, wanawake warembo ambao hawakuacha kunifanya mimi kuwashangalia. Nakumbuka katika machifu wale, alikuwapo chifu mmoja na wa pekee mwanamke - Mwami Theresa Ntare kutoka Kasulu Kibondo.

Katika hali kama hii iliyokuwa tabu kufahamika, tukiwa watoto tulipata kujua maisha ya jamii nyingine, lugha zao, utamaduni wa makabila mengi ya Tanganyika kabla ya watu wengi kutoka sehemu nyingine za pwani hawajajua chochote kuhusu watu hawa.

Nilibahatika kukutana na katika utoto wangu na lile tabaka la Waafrika waliokuwa watumishi wa serikali, kundi dogo makhsusi lililokuwa linakua na liliopembuka kwa elimu zao kutoka Chuo Cha Makerere, Uganda na vyuo vingine.

Hiki ndicho kilikuwa kizazi kipya cha Watanganyika wasomi waliohusika na kuasisi siasa fikra ya uhuru itakayopelekea Waafrika kujitawala - Hamza Mwapachu, Zuberi Mtemvu, Mzee John Rupia, Steven Mhando, Dunstan Omari, Dossa Aziz kwa kuwataja wachache. Kulikuwa pia na tabaka jingine la watu maarufu kutoka Zanzibar kama Ahmed Rashad Ali and Abdul Razak Abdul Wadud ambao walikuwa kama sehemu ya familia yetu.

Siwezi kumsahau Maloo, Mburushi kutoka Congo ya Mashariki ambae alikuwa anakaa nyumbani na baba kwa muda mrefu sana kiasi tuliamini ni mmoja katika familia ya Sykes.

Lakini aliyeshika nafasi ya juu kabisa katika fikra zangu nikiwa mtoto alikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na ni kupitia kwake ndipo tukapata kujua kwa mara ya kwanza kuwa kuna kabila linaitwa, ‘’Wazanaki.’’

Kila alipokuwa anakuja nyumbani kwetu kuja kwake kulikuwa jambo maalum kulikosababisha minong’ono watu wakizungumza kwa sauti za chini wakipeana taarifa kuwa, ‘’Nyerere anakuja au keshafika.”

Kwangu mimi hii ilikuwa ishara ya kutimiza kazi yangu kwani siku zote nilikuwa nikiambiwa kutengeneza kifungua kinywa cha chai na mayai kila alipokuja nyumbani akitokea Shule ya Mt. Francis,Pugu alipokuwa akisomesha.''


Katika makala hii ya kumbukumbu ya kifo cha baba yake, Daisy anaeleza anasema yeye jina lake ni Aisha lakini ilikuwa Julius Nyerere na Hamza Mwapachu ndiyo waliolifanya jina lake la utani ''Daisy,'' limgande kwani wao walikuwa wakifika nyumbani kwao walikuwa wakimwita kwa tashtiti, ''Daisy'', ''Daisy,'' kwa ''accent'' ya Waingereza.

Nimekuleta haya kujenga fikra zako uione siasa katika Dar es Salaam ya 1950s na ushawishi ambao Abdul Sykes aliokuwanao katika jamii ya Waafrika viongozi na ndani ya TAA wakati ule akiwa Kaimu Rais wa TAA na Secretary.

Bila mtu kuwa na background hii itakuwa tabu kuelewa na kuzingatia kwa nini huwezi kuandika historia ya TANU bila ya kumtaja Abdul Sykes wala huwezi kuandika historia ya Mwalimu Nyerere katika siasa na katika TANU bila ya kumtaja Abdul Sykes.

Ukiyajua haya mengine hayakupi tabu kuwa wazi kwako na kuyaelewa.
 
Sajor...
Kwa miaka mingi historia hii ilipotea na ikawa hakuna anaeijua hata chembe yake
ingawa seminar paper ya Daisy ilikuwapo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam toka
mwaka wa 1968.
Mwaka jana katika kuadhimisha miaka 50 ya kifo cha Abdul Sykes, Daisy aliandika
makala ya kumkumbuka baba yake.
Kuna vipande katika makala ile kwa hakika vinavutia sana.
Mfano hiki hapo chini:
''Lakini kile ambacho kimeathiri fikra zangu na kubakia na mimi katika kumbukumbu zangu ni kufika pale nyumbani kwa uongozi wa juu wa Waafrika kabla ya uhuru, machifu kutoka makabila mbalimbali ya Tanganyika na viongozi wa vyama vya wazalendo vilivyokuwa ndiyo vinainukia, viongozi wa vyama vya wafanyakazi na wafanyakazi Waafrika katika wa serikali ya kikoloni.
Kutokana na hadhi hii ya baba yangu na umaarufu wake na kule kupenda kukirimu watu, nikawa si mgeni kwa machifu mashuhuri na nikawa nawahudumia walipokuwa mara nyingi wakija nyumbani.
Wageni hawa mashuhuri waliokuwa wakija nyumbani ni pamoja na Mangi Mkuu Thomas Marealle, Machifu Abdiel Shangali, John Maruma kutoka Moshi, Adam Sapi Mkwawa kutoka Iringa, Kidaha Makwaia kutoka Usukuma, Abdallah Fundikira, Harun Msabila Lugusha kutoka Tabora, Humbi Ziota kutoka Nzega, Michael Lukumbuzya kutoka Ukerewe na Patrick Kunambi kutoka Morogoro na wengine wengi.
Hawa machifu kwa kawaida walikuwa wakija na wake zao, wanawake warembo ambao hawakuacha kunifanya mimi kuwashangalia. Nakumbuka katika machifu wale, alikuwapo chifu mmoja na wa pekee mwanamke - Mwami Theresa Ntare kutoka Kasulu Kibondo.
Katika hali kama hii iliyokuwa tabu kufahamika, tukiwa watoto tulipata kujua maisha ya jamii nyingine, lugha zao, utamaduni wa makabila mengi ya Tanganyika kabla ya watu wengi kutoka sehemu nyingine za pwani hawajajua chochote kuhusu watu hawa.
Nilibahatika kukutana na katika utoto wangu na lile tabaka la Waafrika waliokuwa watumishi wa serikali, kundi dogo makhsusi lililokuwa linakua na liliopembuka kwa elimu zao kutoka Chuo Cha Makerere, Uganda na vyuo vingine.
Hiki ndicho kilikuwa kizazi kipya cha Watanganyika wasomi waliohusika na kuasisi siasa fikra ya uhuru itakayopelekea Waafrika kujitawala - Hamza Mwapachu, Zuberi Mtemvu, Mzee John Rupia, Steven Mhando, Dunstan Omari, Dossa Aziz kwa kuwataja wachache. Kulikuwa pia na tabaka jingine la watu maarufu kutoka Zanzibar kama Ahmed Rashad Ali and Abdul Razak Abdul Wadud ambao walikuwa kama sehemu ya familia yetu.
Siwezi kumsahau Maloo, Mburushi kutoka Congo ya Mashariki ambae alikuwa anakaa nyumbani na baba kwa muda mrefu sana kiasi tuliamini ni mmoja katika familia ya Sykes.
Lakini aliyeshika nafasi ya juu kabisa katika fikra zangu nikiwa mtoto alikuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na ni kupitia kwake ndipo tukapata kujua kwa mara ya kwanza kuwa kuna kabila linaitwa, ‘’Wazanaki.’’
Kila alipokuwa anakuja nyumbani kwetu kuja kwake kulikuwa jambo maalum kulikosababisha minong’ono watu wakizungumza kwa sauti za chini wakipeana taarifa kuwa, ‘’Nyerere anakuja au keshafika.”
Kwangu mimi hii ilikuwa ishara ya kutimiza kazi yangu kwani siku zote nilikuwa nikiambiwa kutengeneza kifungua kinywa cha chai na mayai kila alipokuja nyumbani akitokea Shule ya Mt. Francis,Pugu alipokuwa akisomesha.''

Katika makala hii ya kumbukumbu ya kifo cha baba yake, Daisy anaeleza anasema yeye jina lake ni Aisha lakini ilikuwa Julius Nyerere na Hamza Mwapachu ndiyo waliolifanya jina lake la utani ''Daisy,'' limgande kwani wao walikuwa wakifika nyumbani kwao walikuwa wakimwita kwa tashtiti, ''Daisy'', ''Daisy,'' kwa ''accent'' ya Waingereza.
Nimekuleta haya kujenga fikra zako uione siasa katika Dar es Salaam ya 1950s na ushawishi ambao Abdul Sykes aliokuwanao katika jamii ya Waafrika viongozi na ndani ya TAA wakati ule akiwa Kaimu Rais wa TAA na Secretary.
Bila mtu kuwa na background hii itakuwa tabu kuelewa na kuzingatia kwa nini huwezi kuandika historia ya TANU bila ya kumtaja Abdul Sykes wala huwezi kuandika historia ya Mwalimu Nyerere katika siasa na katika TANU bila ya kumtaja Abdul Sykes.
Ukiyajua haya mengine hayakupi tabu kuwa wazi kwako na kuyaelewa.
Hakika kuna mengi yamejificha, yamefichwa na kufichika.
 
Here we go again...
Nanren,
Nina umri wa miaka 10 au 11 kila Jumamosi mchana kulikuwa
na kipindi TBC kinaitwa, ''Chipukizi Club,'' ambacho vijana wa hapa
mjini walikuwa wanapiga muziki wa Kizungu - Beatles, Elvis, Cliff
Richard...


Signature tune yake ilikuwa na lyrics...''Here we go loobeloo...''

Kipindi hiki kilipendwa sana na vijana...


1566643870542.png

Chipukizi hao hapo juu
 
Raha siyo raha?
Maalim Faiza,
Historia hii haiishi utamu...

Kama kuna ihsani kubwa iliyofanyiwa historia hii ni kule kujaribu kuifuta.
Baada ya kuwa imekuwa haifahamiki kwa miaka ghafla ikaja kuandikwa.

Kishindo chake ndicho hiki.

Kubaki na ile ya zamani haiwezekani na kukubali hii inawataabisha lakini
akili ni akili inapoona ukweli unaitambua kuwa hii ni kweli.
 
Hakika kuna mengi yamejificha, yamefichwa na kufichika.
Sajor...
Wananiuliza, ''Mohamed did you really know these people?''
''Do you doubt me?''

''Not at all its the way you talk about them the story is so thrilling...''

''I used to see them every day not that I knew at that time it would
come a day I will write about them...''

Maswali na maswali na maswali...

Wananiuliza kama kweli hawa watu mimi nikiwajua na nawajibu,

''Sana kwani hamuniamini?''
''Hapana hiki kisa kinavutia sana.''

''Nikiwaona siku zote ingawa sikutambua kwa wakati ule kama
nitakuja kuandika historia zao.''
 
Back
Top Bottom