Nataka kuwa dalali, nifanyeje ili niwe maarufu?

Mjina Mrefu

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2016
Posts
3,045
Reaction score
3,389
Wakuu, nataka kuwa dalali wa nyumba, vyumba, viwanja, frame za biashara, apartments nk. Je nifanyeje ili niwe maarufu?

Nifanye ili wenye mali zao wawe wananipa mtonyo ili nipeleke wateja?
 
Jitangaze haswa na uwe mwaminifu,sio mtu anatafuta kitu na anakupa mahitaj yake wwe unampeleka kinyume kisa tu unataka hela yake,kua mkweli,usiruhusu tamaa ikutawale,mtu akikataa kitu usimlazimshe akupe usumbufu,,usiuze viwanja mara mbili mbili,ukiwa mwaminifu Mungu nae atakuinua..
 
Weka mabango na picha ya hicho unacho kifanyia ufalali,kuwa na simu inayopatikana muda wote uwe na dili za kweli sio utapeli shinda vijiweni,kuwa na maneno mengi kama mswahili,kuwa na simu ya smartphone kuwa mtanashati na msafi
 
Asante mkuu. Ushauri murua sana
 
Weka mabango na picha ya hicho unacho kifanyia ufalali,kuwa na simu inayopatikana muda wote uwe na dili za kweli sio utapeli shinda vijiweni,kuwa na maneno mengi kama mswahili,kuwa na simu ya smartphone kuwa mtanashati na msafi
Asante mkuu. Nitafanya hivyo
 
Weka mabango na picha ya hicho unacho kifanyia ufalali,kuwa na simu inayopatikana muda wote uwe na dili za kweli sio utapeli shinda vijiweni,kuwa na maneno mengi kama mswahili,kuwa na simu ya smartphone kuwa mtanashati na msafi
Huu ushauri mzuri zingatia boss, penyewe Pana nia Kuna njia...

Nikutakie kheri mkuu!
 
Kuna vyama vyao vya udalali, jiunge navyo.

Ili kujitofautisha nao tangaza kazi zako kwenye mitandao, uwe na PC na smartphone yenye kamera nzuri, usiweke chumvi sana, usimpe mtu matumaini tofauti.

Kuna mdau kazungumzia swala la kuwa hewani muda wote, hili ni la muhimu, ukiwa na marketing strategies nzuri hata madalali wenzako wanakuletea kazi mnagawana sawa sawa.

Na kwenye matangazo yako unaweza kufuta ile chaji ya uchakavu, ila tu mteja akawa anacover nauli za kwenda kwenye eneo husika.
 
Shukran mkuu nitautilia maanani huu ushauri
 
Usiache kuleta mrejesho mkuu, maana kwa hivi vyuma inaweza kuwa msaada tukipata ushauri kwa mtu aliye field.
Mimi ni mtu wa kutoa feedback always. Nitafanya hivyo ngoja niingie sokoni.

Alafu nilikua nawaza kufungua na frem ndogo kabisa kwa ajili ya iyo issue.

Yaani clients wawe wanakuja ofisini alafu nawapelekea one way
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…