Nataka kuwa wakala wa LUKU (TANESCO)

Nataka kuwa wakala wa LUKU (TANESCO)

Joined
Jan 6, 2015
Posts
7
Reaction score
0
Habari za muda huu! kwa heshima na taadhima napenda kuleta wazo langu mezani ili nipate ufumbuzi au uwelewa wa kutosha kabla ya kutenda (survey).

Mimi ni mwajiriwa ktk sekta binafsi nna wazo la kufungua ofisi ya uuzaji wa lishe (nafaka) na kuwa wakala wa uuzaji wa luku kupitia mashine za tanesco wenyewe na sio max malipo n.k kwani naamini mashine hizo huwa network inasumbua sana.

Kuhusu lishe(nafaka kwa ujumla wake) elimu nimepata tayari ya kutosha kunifanya nianze kutenda.
Ningependa kujua taratibu za kufata kuwa wakala wa luku tanesco, gharama za msingi elekezi. Naomba muongozo!
 
Wadau naomba muongozo wenu kwani nataraji wiki ijayo mungu akijaalia uhai na afya niwe wakala wa luku tanesco. Msaada tafadhali njia za kufata, msingi na mengineo
 
Habari za muda huu! kwa heshima na taadhima napenda kuleta wazo langu mezani ili nipate ufumbuzi au uwelewa wa kutosha kabla ya kutenda (survey).
Mimi ni mwajiriwa ktk sekta binafsi nna wazo la kufungua ofis ya uuzaji wa lishe (nafaka) na kuwa wakala wa uuzaji wa luku kupitia mashine za tanesco wenyewe na sio max malipo n.k kwani naamini mashine hizo huwa network inasumbua sana.
kuhusu lishe(nafaka kwa ujumla wake) elimu nimepata tayari ya kutosha kunifanya nianze kutenda.
Ningependa kujua taratibu za kufata kuwa wakala wa luku tanesco, gharama za msingi elekezi. Naomba muongozo!
Mimi Nina uelewa kiasi kwa sababu wife wangu aliajiriwa kwenye ofisi Kama hyo mkoani.
Alichoniambia ni kwamba kila mwaka huwa wanatangaza hiyo tender halaf watu wanaandika maombi ya kuomba hiyo nafasi.
Lakini wakati huo unaomba masharti yao uwe na ofisi/fremu ya kueleweka na yenye A/C ndani kwa sababu ya kupoza hizo mashine zao.
Halafu sharti lingine uwe na pesa isiyopungua milioni 5,hyo ni cash ambayo utaanza nayo mauzo.
Sasa Cha msingi nenda kwenye ofisi ya Tanesco ya mkoa uliopo ili ujue Kama mwaka huu wameshatangaza hiyo tenda au bado.
Ingawa Kuna ugumu kidogo kwenye kuipata coz hizo nafasi unagombania na wahindi so bila kujuana Kuna kasheshe.
Hata Mimi kiukweli nimeipenda hii biashara mwaka wowote nikijipanga nitafuatilia kwa mkoani Nina uhakika inalipa sana ila sina uhakika kwa sehem Kama Dar es salaam Kama bado inalipa maana watu wengi wananunua umeme kwa kutumia simu zao,mpesa/tigopesa.
 
Mkoa gani mkuu?
Habari za muda huu! kwa heshima na taadhima napenda kuleta wazo langu mezani ili nipate ufumbuzi au uwelewa wa kutosha kabla ya kutenda (survey).
Mimi ni mwajiriwa ktk sekta binafsi nna wazo la kufungua ofis ya uuzaji wa lishe (nafaka) na kuwa wakala wa uuzaji wa luku kupitia mashine za tanesco wenyewe na sio max malipo n.k kwani naamini mashine hizo huwa network inasumbua sana.
kuhusu lishe(nafaka kwa ujumla wake) elimu nimepata tayari ya kutosha kunifanya nianze kutenda.
Ningependa kujua taratibu za kufata kuwa wakala wa luku tanesco, gharama za msingi elekezi. Naomba muongozo!
 
Back
Top Bottom