Nataka kuwashitaki PPF, naombeni mawazo na muongozo mzuri.

Nataka kuwashitaki PPF, naombeni mawazo na muongozo mzuri.

Bunny Wailer

Member
Joined
Oct 29, 2017
Posts
11
Reaction score
11
Habari wana jamvi...!!
Nina tatizo na ningeomba nipate ushauri wenu ikibidi muongozo wa namna gani nifanye ili kupata ufumbuzi na haki zangu. Ni hivi, miezi sita sasa nimepoteza ajira kwa kufukuzwa na mwajiri wangu. Baada ya kupoteza ajira, nilienda ofisi za watu wa ppf kufuatilia mafao yangu. Lakini walichonambia ni kwamba, wamesitisha utoaji mafao mpaka wapate maelekezo toka serikalini, hiyo ilikuwa mwezi wa tano. Nikajipa moyo nikiamini maelekezo ya serikalini yatatoka ili nipate mafao yangu kutoka ppf. Kwa kipindi ambacho nilikuwa nikisubiri maelekezo ya serikalini kwa watu wa ppf ambayo ndiyo yangekuwa kama tiketi ya mimi kupata mafao, nilikuwa kutafuta ajira huku na huko, ila kwa kweli ajira zimekuwa ngumu sana kupatikana. Miezi miwili baadaye nikaenda tena ppf kutaka kujua, na majibu yalikuwa yaleyale kwamba wanasubiri maelekezo toka serikalini. Lakini nilipodadisi sana kwa maswali, niliambiwa na yule mhudumu kuwa, mafao yanatolewa kwa waliopunguzwa makazini/redundancy. Nilipouliza kama wanatoa kwa waliopunguzwa kazini, iweje waliofukuzwa wasipewe, yule mhudumu alinijibu vizuri kabisa kuwa maswali kama hayo hata wao huwa wanajiuliza na huwa hawapati majibu.

Wana jamvi, tangu kupoteza ajira nimekuwa na maisha ya shida sana, mambo yangu mengi yamevurugika, sina pa kushika, sina mjomba wala shangazi wa kunisaidia. Ninavyoishi Mungu pekee ndiye anajua. Nyumba niliyokuwa naishi ni ya kupanga, ilinibidi niondoke baada ya kodi kuisha. Nimekuwa naishi kwa kaka yangu ambaye nyumba yake nayo ilibomolewa huko Mbezi, hivyo naye anaishi kwenye nyumba ya mkwe wake. Mimi amenipa hifadhi kwa muda na hata hivyo nyumba yenyewe ya mkwe wake haijaisha kiujenzi kwa hiyo ninalala sebuleni. Kwa sababu nyumba ina vyumba viwili cha kwake na mkewe na kimoja cha watoto wake wawili wa kike ambao ni wakubwa.

Wana jamvi, lengo langu lilikuwa nifanye biashara yangu mwenyewe kwa hela hiyo ya ppf, lakini imeshindikana kwa sababu pesa yangu imezuiwa na hawa ppf kwa maelezo kuwa wanasubiri maelekezo toka serikalini. Kaka yangu mwenyewe hali yake kiuchumu si nzuri, kwa hiyo si rahisi kunipa mtaji. Kutokana na kuwaeleza watu tatizo langu, kuna mtu amenishauri niende mahakamani kuwashitaki ppf ili wanipe mafao yangu. Mtu huyo amenambia, msingi wa kesi yangu upo kwenye 'ubaguzi' kwamba; ppf wanatoa mafao kwa watu waliopunguzwa kazini ila wanabagua waliofukuzwa kazini, ilihali hakuna sheria ya namna hiyo. Amenieleza kuwa, hakuna sheria inayosema kuwa waliopunguzwa/redundancy watapewa mafao na ambao wamefukuzwa hawatapewa mafao. Sasa shida yangu ni moja hapa, kama naenda mahakamani hela yangu yenyewe ni hiyo milioni mbili na kama laki mbili, je, mwanasheria nitamlipa nini?

Naombeni ushauri ndugu zangu.
 
Mkuu Bunny Wailer pole sana kwa kadhia iliyokukumba. Mifuko hii ya kijamii imewekwa kwa misingi ya kisheria na shughuli zake zinatekelezwa kwa mujibu wa sheria husika. Mafao kwa mchangiaji (mwajiriwa) ni haki ya msingi kwa mujibu wa sheria mama ya mifuko hii. Haki hii ya msingi hutolewa kwa kuhusisha mnufaikaji (mwanachama) na mwajiri ambaye pia ni mchangiaji. Katika kufanikisha hili, ni wajibu wa pande zote tatu (mfuko, mwanachama na mwajiri) kutimiza matakwa na taratibu zilizowekwa. Pamoja na taratibu zingine, mwajiri anao wajibu wa kudhibitisha kuwa mwanachama wa mfuko anayo stahiki ya kulipwa kutokana na michango yake kwenye mfuko.

Sasa basi, kama ulivyogusia, serikali ni mdau mkubwa katiaka mifukao hii ya kijamii, PPF ikiwa ni mojawapo, kwa sababu ndie mchangiaji mkubwa. Serikali inachangia kiasi maalumu kwa kila mwajiriwa wake anayestahili mafao ya uzeeni (pensheni). Hii ipo kisheria. Katika utaratibu wa ulipaji wa mafao, ukiachilia mbali mashariti ya umri na kiwango cha kuchangia ili uwe na stahiki yako ya mafao, sharti mojawapo ni mwajiri kuidhinisha ulipwaji wa stahiki zako. Mchakato wa mwajiri kuidhinisha stahiki zako unategemea na aina ya mafao unayostahili, kiwango cha mafao unayostahili na wakati unaodai stahiki zako za mafao.

Katika mchakato huu, mstaafu hatawekwa fungu moja na anayehitaji kujitoa katia fao. Aliyestaafu kwa hiari au kujiuzuru katika ajira pia mchakato wake utatofautiana na aliyestaafu kwa mujibu wa sheria (kufikia kikomo cha umri) au aliyeachishwa kazi kwa mujibu wa sheria. Michakato hii inahusisha kanuni za utumishi.

Suala la kuwashtaki PPF wala lisichukue wasiwasi mkubwa kwako. Usifikirie kuhusu gharama, maana haki yako ni haki yako pasipo kujali gharama. Cha msingi hapa ni kuangalia unamshtaki nani. Kama utaamua kushtaki, hakuna shaka katika shauri lako lazima umjumuishe mwajiri wako (hujaelezea ni yupi, bila shaka ni shirika la umma, na katika mazingira mengine itabidi umjumuishe Mwanasheria Mkuu wa serikali). Kwa hiyo katika shauri lako unaweza jikuta inakuchukua zaidi ya miezi mitatu ili mahakama/baraza lianze kusikiliza shauri lako. Gharama za shauri zisikutese katika mazingira ya sheria unao wasaa wa kulipwa mara tano ya hizo milioni mbili unazozihitaji. Zingatia mda.

Pia uwezekano upo kuwa shauri litakalifunguliwa dhidi ya PPF litapata vikwazo vya mapingamizi, kwa sababu tayari umekwisha fukuzwa kazini zaidi ya miezi sita iliyopita. Hata hivyo hii inayo tiba (remedy) yake kama ukipata wakili mzuri.

Ushauri: Hakikisha umetunza correspondence zote kati yako, mwajiri wako na PPF, toka barua ya kuajiriwa kwa msingi wa malipo ya uzeeni (pensheni) na barua ulizowapatia PPF na majibu yao. Correspondence hizi ndio utakuwa msingi wa madai ya stahiki zako.
 
Mkuu Bunny Wailer pole sana kwa kadhia iliyokukumba. Mifuko hii ya kijamii imewekwa kwa misingi ya kisheria na shughuli zake zinatekelezwa kwa mujibu wa sheria husika. Mafao kwa mchangiaji (mwajiriwa) ni haki ya msingi kwa mujibu wa sheria mama ya mifuko hii. Haki hii ya msingi hutolewa kwa kuhusisha mnufaikaji (mwanachama) na mwajiri ambaye pia ni mchangiaji. Katika kufanikisha hili, ni wajibu wa pande zote tatu (mfuko, mwanachama na mwajiri) kutimiza matakwa na taratibu zilizowekwa. Pamoja na taratibu zingine, mwajiri anao wajibu wa kudhibitisha kuwa mwanachama wa mfuko anayo stahiki ya kulipwa kutokana na michango yake kwenye mfuko.

Sasa basi, kama ulivyogusia, serikali ni mdau mkubwa katiaka mifukao hii ya kijamii, PPF ikiwa ni mojawapo, kwa sababu ndie mchangiaji mkubwa. Serikali inachangia kiasi maalumu kwa kila mwajiriwa wake anayestahili mafao ya uzeeni (pensheni). Hii ipo kisheria. Katika utaratibu wa ulipaji wa mafao, ukiachilia mbali mashariti ya umri na kiwango cha kuchangia ili uwe na stahiki yako ya mafao, sharti mojawapo ni mwajiri kuidhinisha ulipwaji wa stahiki zako. Mchakato wa mwajiri kuidhinisha stahiki zako unategemea na aina ya mafao unayostahili, kiwango cha mafao unayostahili na wakati unaodai stahiki zako za mafao.

Katika mchakato huu, mstaafu hatawekwa fungu moja na anayehitaji kujitoa katia fao. Aliyestaafu kwa hiari au kujiuzuru katika ajira pia mchakato wake utatofautiana na aliyestaafu kwa mujibu wa sheria (kufikia kikomo cha umri) au aliyeachishwa kazi kwa mujibu wa sheria. Michakato hii inahusisha kanuni za utumishi.

Suala la kuwashtaki PPF wala lisichukue wasiwasi mkubwa kwako. Usifikirie kuhusu gharama, maana haki yako ni haki yako pasipo kujali gharama. Cha msingi hapa ni kuangalia unamshtaki nani. Kama utaamua kushtaki, hakuna shaka katika shauri lako lazima umjumuishe mwajiri wako (hujaelezea ni yupi, bila shaka ni shirika la umma, na katika mazingira mengine itabidi umjumuishe Mwanasheria Mkuu wa serikali). Kwa hiyo katika shauri lako unaweza jikuta inakuchukua zaidi ya miezi mitatu ili mahakama/baraza lianze kusikiliza shauri lako. Gharama za shauri zisikutese katika mazingira ya sheria unao wasaa wa kulipwa mara tano ya hizo milioni mbili unazozihitaji. Zingatia mda.

Pia uwezekano upo kuwa shauri litakalifunguliwa dhidi ya PPF litapata vikwazo vya mapingamizi, kwa sababu tayari umekwisha fukuzwa kazini zaidi ya miezi sita iliyopita. Hata hivyo hii inayo tiba (remedy) yake kama ukipata wakili mzuri.

Ushauri: Hakikisha umetunza correspondence zote kati yako, mwajiri wako na PPF, toka barua ya kuajiriwa kwa msingi wa malipo ya uzeeni (pensheni) na barua ulizowapatia PPF na majibu yao. Correspondence hizi ndio utakuwa msingi wa madai ya stahiki zako.

Dragon, asante sana kwa majibu mazuri. Inawezekana sijaeleza kila kitu kutokana na hali niliyo nayo hivi sasa, hivyo ili nieleze kila kitu, kuna mazingira mtu anayetaka kujua zaidi toka kwangu, itamlazimu kuniuliza zaidi. Dragon, mimi sikuwa mwajira wa shirika la umma. Mimi nilikuwa mfanyakazi wa kampuni binafsi ya Wachina, kwa hiyo michango inayoonekana kwa PPF ni ile ya kwangu mimi na mwajiri ambaye ni kampuni niliyokuwa nafanyia kazi. Kinachoniuma zaidi ni ule ubaguzi unaofanywa na hawa ppf kwamba waliopunguzwa makazini wanapewa mafao yao ila wanaofukuzwa wananyimwa ilihali wote haki ni yetu na ilihali wote tumepoteza ajira.
 
Elewa kuwa wewe umeingia mkataba wa mafao yako na ppf mwajiri ni middle man tu. Kile ulichochangia ni haki yako unless otherwise kama kuna hasara umemtia mwajiri basi anatakiwa akate kutoka ktk mafao yako kwa reconciliation ya pamoja.
Zile ni pesa zako zinazokuwa compounded for several years sasa uhuni huo unafanywa na mwajiri aliyewainamisha hata hao ppf.
 
Mkuu Bunny Wailer pole sana kwa kadhia iliyokukumba. Mifuko hii ya kijamii imewekwa kwa misingi ya kisheria na shughuli zake zinatekelezwa kwa mujibu wa sheria husika. Mafao kwa mchangiaji (mwajiriwa) ni haki ya msingi kwa mujibu wa sheria mama ya mifuko hii. Haki hii ya msingi hutolewa kwa kuhusisha mnufaikaji (mwanachama) na mwajiri ambaye pia ni mchangiaji. Katika kufanikisha hili, ni wajibu wa pande zote tatu (mfuko, mwanachama na mwajiri) kutimiza matakwa na taratibu zilizowekwa. Pamoja na taratibu zingine, mwajiri anao wajibu wa kudhibitisha kuwa mwanachama wa mfuko anayo stahiki ya kulipwa kutokana na michango yake kwenye mfuko.

Sasa basi, kama ulivyogusia, serikali ni mdau mkubwa katiaka mifukao hii ya kijamii, PPF ikiwa ni mojawapo, kwa sababu ndie mchangiaji mkubwa. Serikali inachangia kiasi maalumu kwa kila mwajiriwa wake anayestahili mafao ya uzeeni (pensheni). Hii ipo kisheria. Katika utaratibu wa ulipaji wa mafao, ukiachilia mbali mashariti ya umri na kiwango cha kuchangia ili uwe na stahiki yako ya mafao, sharti mojawapo ni mwajiri kuidhinisha ulipwaji wa stahiki zako. Mchakato wa mwajiri kuidhinisha stahiki zako unategemea na aina ya mafao unayostahili, kiwango cha mafao unayostahili na wakati unaodai stahiki zako za mafao.

Katika mchakato huu, mstaafu hatawekwa fungu moja na anayehitaji kujitoa katia fao. Aliyestaafu kwa hiari au kujiuzuru katika ajira pia mchakato wake utatofautiana na aliyestaafu kwa mujibu wa sheria (kufikia kikomo cha umri) au aliyeachishwa kazi kwa mujibu wa sheria. Michakato hii inahusisha kanuni za utumishi.

Suala la kuwashtaki PPF wala lisichukue wasiwasi mkubwa kwako. Usifikirie kuhusu gharama, maana haki yako ni haki yako pasipo kujali gharama. Cha msingi hapa ni kuangalia unamshtaki nani. Kama utaamua kushtaki, hakuna shaka katika shauri lako lazima umjumuishe mwajiri wako (hujaelezea ni yupi, bila shaka ni shirika la umma, na katika mazingira mengine itabidi umjumuishe Mwanasheria Mkuu wa serikali). Kwa hiyo katika shauri lako unaweza jikuta inakuchukua zaidi ya miezi mitatu ili mahakama/baraza lianze kusikiliza shauri lako. Gharama za shauri zisikutese katika mazingira ya sheria unao wasaa wa kulipwa mara tano ya hizo milioni mbili unazozihitaji. Zingatia mda.

Pia uwezekano upo kuwa shauri litakalifunguliwa dhidi ya PPF litapata vikwazo vya mapingamizi, kwa sababu tayari umekwisha fukuzwa kazini zaidi ya miezi sita iliyopita. Hata hivyo hii inayo tiba (remedy) yake kama ukipata wakili mzuri.

Ushauri: Hakikisha umetunza correspondence zote kati yako, mwajiri wako na PPF, toka barua ya kuajiriwa kwa msingi wa malipo ya uzeeni (pensheni) na barua ulizowapatia PPF na majibu yao. Correspondence hizi ndio utakuwa msingi wa madai ya stahiki zako.

Bunny Wailer, pole sana, hata mimi ni mhanga wa hawa PPF. Nimepata wazo jipya na nguvu ya kujua namna gani napata stahiki zangu kwa kusoma maoni ya ndugu Dragon.
 
Mkuu, kabla hujachukua uamuzi wa kwenda court, nikuulize umefatilia vizuri benefits zinazotolewa na PPF na vigezo na masharti ya kupata mafao yako?,
PPF wana scheme 3, traditional, deposit administration na wote scheme, kila scheme ina vigezo vyake (soma uvijue wewe ulikuwa kwenye scheme gan),
Sasa kwenye mafao yanayotolewa na PPF kuna old age, survival benefits, maternity, gratuity, death, education na disability. Hawa jamaa hawana withdraw benefits kama walivyo NSSF na mifuko mingine, sasa kwa ishu yako ya kufukuzwa kazi kwenda kudai mafao yako itakubid hadi utimize miaka 55+ hapo ndo utaweza kudai mafao ambapo utapewa old age au gratuity inategemea na umechangia kwa muda gani.
Mim binafsi sikushauri uende court ila jaribu kupata mshauri mzuri mwenye uelewa na mifuko ya hifadhi ya jamaa especially PPF, huyo mhudumu alikuwa anakuletea bla bla nyingi ila ukweli ni huo PPF hawana fao la kujitoa ukiacha kazi subiri ufikie umri wa pension ambao ni miaka 55+
 
Mkuu Bunny Wailer pole sana kwa kadhia iliyokukumba. Mifuko hii ya kijamii imewekwa kwa misingi ya kisheria na shughuli zake zinatekelezwa kwa mujibu wa sheria husika. Mafao kwa mchangiaji (mwajiriwa) ni haki ya msingi kwa mujibu wa sheria mama ya mifuko hii. Haki hii ya msingi hutolewa kwa kuhusisha mnufaikaji (mwanachama) na mwajiri ambaye pia ni mchangiaji. Katika kufanikisha hili, ni wajibu wa pande zote tatu (mfuko, mwanachama na mwajiri) kutimiza matakwa na taratibu zilizowekwa. Pamoja na taratibu zingine, mwajiri anao wajibu wa kudhibitisha kuwa mwanachama wa mfuko anayo stahiki ya kulipwa kutokana na michango yake kwenye mfuko.

Sasa basi, kama ulivyogusia, serikali ni mdau mkubwa katiaka mifukao hii ya kijamii, PPF ikiwa ni mojawapo, kwa sababu ndie mchangiaji mkubwa. Serikali inachangia kiasi maalumu kwa kila mwajiriwa wake anayestahili mafao ya uzeeni (pensheni). Hii ipo kisheria. Katika utaratibu wa ulipaji wa mafao, ukiachilia mbali mashariti ya umri na kiwango cha kuchangia ili uwe na stahiki yako ya mafao, sharti mojawapo ni mwajiri kuidhinisha ulipwaji wa stahiki zako. Mchakato wa mwajiri kuidhinisha stahiki zako unategemea na aina ya mafao unayostahili, kiwango cha mafao unayostahili na wakati unaodai stahiki zako za mafao.

Katika mchakato huu, mstaafu hatawekwa fungu moja na anayehitaji kujitoa katia fao. Aliyestaafu kwa hiari au kujiuzuru katika ajira pia mchakato wake utatofautiana na aliyestaafu kwa mujibu wa sheria (kufikia kikomo cha umri) au aliyeachishwa kazi kwa mujibu wa sheria. Michakato hii inahusisha kanuni za utumishi.

Suala la kuwashtaki PPF wala lisichukue wasiwasi mkubwa kwako. Usifikirie kuhusu gharama, maana haki yako ni haki yako pasipo kujali gharama. Cha msingi hapa ni kuangalia unamshtaki nani. Kama utaamua kushtaki, hakuna shaka katika shauri lako lazima umjumuishe mwajiri wako (hujaelezea ni yupi, bila shaka ni shirika la umma, na katika mazingira mengine itabidi umjumuishe Mwanasheria Mkuu wa serikali). Kwa hiyo katika shauri lako unaweza jikuta inakuchukua zaidi ya miezi mitatu ili mahakama/baraza lianze kusikiliza shauri lako. Gharama za shauri zisikutese katika mazingira ya sheria unao wasaa wa kulipwa mara tano ya hizo milioni mbili unazozihitaji. Zingatia mda.

Pia uwezekano upo kuwa shauri litakalifunguliwa dhidi ya PPF litapata vikwazo vya mapingamizi, kwa sababu tayari umekwisha fukuzwa kazini zaidi ya miezi sita iliyopita. Hata hivyo hii inayo tiba (remedy) yake kama ukipata wakili mzuri.

Ushauri: Hakikisha umetunza correspondence zote kati yako, mwajiri wako na PPF, toka barua ya kuajiriwa kwa msingi wa malipo ya uzeeni (pensheni) na barua ulizowapatia PPF na majibu yao. Correspondence hizi ndio utakuwa msingi wa madai ya stahiki zako.

Dragon, hata mimi ni moja ya wahanga wa hili la PPF. Kuna kitu umegusia kuhusu uwezekano wa pingamizi kwa upande wa PPF dhidi ya mshitaki kwamba imepita miezi sita, japo umemtoa waiwasi kuwa kuna namna ingine ambayo anaweza kusaidiwa kama sijakosea. Mimi binafsi, nina siku 124 tangu niachishwe kazi, siku 124 ni sawa na miezi 3 na siku kama 14 hivi. Je, kwa upande wangu kuhusiana na siku hizo bado siwezi kupata pingamizi pale nitakapoamua kutafuta msaada kisheria? Je, linapokuja suala la kuhesabu siku, vipi siku za weekend nazo zinahesabika kimahakama au zinaondolewa. Au niweke hivi, linapokuja suala la kuhesabu siku, je, kimahakama, siku zinahesabikaje mfano hizo siku zangu 124 tangu nifukuzwe kazi?

Kuhusu correspondence, binafsi nimetumia njia ya email kwa watu wa PPF ili kupata ufafanuzi juu ya mafao yangu na walinijibu, je, email kimahakama zinakubalika kama sehemu ya ushahidi iwapo zitakuwa printed? SSRA ambao ndiyo walezi niliwaandikia malalamiko yangu kwa njia ya posta, wao hadi naandika hivi sijapata majibu yao. Na ni barua ya tangu mwezi Oktoba tarehe 5, 2017. Je, kwa hili nafanyaje, maana nachokiona hapa hata hawa watu wa SSRA, nao kuna umuhimu wa kuwahusisha juu ya hili kutokan na wao kuwa waangalizi/wadhibiti/na wasimamizi wa hii mifuko.

Naomba ufafanuzi wa kina ili nianze kuchukua hatua Jumatatu ijayo kabla sijachelewa. Maana hali ni ngumu sana huku mitaani na inkera kwa kweli kusikia majibu ya kwamba wao PPF wanasubiri majibu na maelekezo toka serikalini. Sasa nimekuwa najiuliza, ina maana serikali haijui kuwa watu wana-suffer huku mitaani?
 
Mkuu, kabla hujachukua uamuzi wa kwenda court, nikuulize umefatilia vizuri benefits zinazotolewa na PPF na vigezo na masharti ya kupata mafao yako?,
PPF wana scheme 3, traditional, deposit administration na wote scheme, kila scheme ina vigezo vyake (soma uvijue wewe ulikuwa kwenye scheme gan),
Sasa kwenye mafao yanayotolewa na PPF kuna old age, survival benefits, maternity, gratuity, death, education na disability. Hawa jamaa hawana withdraw benefits kama walivyo NSSF na mifuko mingine, sasa kwa ishu yako ya kufukuzwa kazi kwenda kudai mafao yako itakubid hadi utimize miaka 55+ hapo ndo utaweza kudai mafao ambapo utapewa old age au gratuity inategemea na umechangia kwa muda gani.
Mim binafsi sikushauri uende court ila jaribu kupata mshauri mzuri mwenye uelewa na mifuko ya hifadhi ya jamaa especially PPF, huyo mhudumu alikuwa anakuletea bla bla nyingi ila ukweli ni huo PPF hawana fao la kujitoa ukiacha kazi subiri ufikie umri wa pension ambao ni miaka 55+

6GB
Nimemuelewa ndugu hapo juu. Tatizo si aina gani ya scheme, na walio wengi wanapoajiriwa hilo la scheme huwa hawapewi elimu. Mimi binafsi niliunganiishwa na PPF bila kujua ni scheme gani sijui nini nini huko. Tatizo linalokuja hapa kwa jinsi nilivyomuelewa na kwa jinsi ukweli ulivyo ni kwamba, PPF wamesitisha fao la kujitoa, ila hapo awali walikuwa wanatoa fao hilo. Na hata kwenye website yao, pale mbele kuna kipengele hicho cha 'withdrawal benefitis'......... Tatizo lingine ni kwamba, PPF wanatoa mafao kwa watu waliopunguzwa makazini (yaani waliopewa redundancy)....hapo awali pia ilikuwa hawatoi mafao kwa waliofukuzwa makazini. Mimi nimekuwa mfuatiliaji mzuri sana tangu nifukuzwe kazi. Sasa wanachokifanya kwa sasa PPF ni kutoa mafao kwa waliopewa redundancy kwa madai kuwa, waliopewa redundancy hawawezi tena kuchangia ndiyo maana wanapewa mafao yao. Sasa kama waliopewa redundancy na bado ni vijana wanapewa mafao yao kwa kigezo hicho cha kutokuweza kuendelea kuchangia, taabu au shida ni nini kwa huyu aliyefukuzwa kazi? Kwa nini asipewe mafao yake? Kumbuka, serikali kupitia mawaziri wake mara mbili wamesikika wakisema kuwa kuna maandalizi ya kuleta fao la kukosa ajira kwa watu waliofukuzwa kazi. Sasa kama kuna utaratibu huo wa kuleta fao la kukosa ajira, maana yake ni kwamba, kuna ulazima kwa mtu aliyepoteza ajira kupewa mafao yake. Sasa mtu kapoteza ajira, hakuna faol la kukosa ajira, ajira hazipatikani, hawezi kufanya biashara sasa mtu wa namna hii anazuiwaje kupewa mafao yake? Hii si fair kwa kweli. Binafsi naungana mkono na ndugu na nina imani kuna grounds za kufungua kesi kwa kweli.
 
Hii issue ni vyema sana kama ikafika bungeni na akapatikane mbunge anaejitambua ili aiwasilishe vizuri (wasiwe wale wa kila kitu ndiyooo). Ni muda sasa tangu mifuko hii ikumbwe na hali ya sintofahamu
 
Hii issue ni vyema sana kama ikafika bungeni na akapatikana mbunge anaejitambu ili aiwasilishe vizuri (wasiwe wale wa kila kitu ndiyooo). Ni muda sasa tangu mifuko hii ikumbwe na hali ya sintofahamu

Wabunge wamekazania makinikia, wamekazania kuchambana tu. Kwa hili hata tusiwategemee wanasiasa, nimeshaona hawana dhamira ya kweli. Wao hawahusiki na hili ila ingekuwa wanahusika ungeona zamani wameshapiga kelele. Ni mmoja tu ambaye ana nia ya dhati juu ya hili naye ni Tundu Lissu. Lissu na wenzake wa Tanganyika Law Society walisikika wakisema hili suala wanalipeleka mahakamani. Sasa kwa mtu kama Lissu kusema hili suala linaenda mahakamani maana yake ana uhakika na matokeo yake. Binafsi nina tatizo au ni mhanga na hawa PPF, nachukua hatua kuanzia wiki ijayo.
 
Kumbuka, serikali kupitia mawaziri wake mara mbili wamesikika wakisema kuwa kuna maandalizi ya kuleta fao la kukosa ajira kwa watu waliofukuzwa kazi. Sasa kama kuna utaratibu huo wa kuleta fao la kukosa ajira, maana yake ni kwamba, kuna ulazima kwa mtu aliyepoteza ajira kupewa mafao yake. Sasa mtu kapoteza ajira, hakuna faol la kukosa ajira, ajira hazipatikani, hawezi kufanya biashara sasa mtu wa namna hii anazuiwaje kupewa mafao yake?

Samahani naomba nichangie ninachokifahamu kidogo kuhusu hifadhi ya jamii, samahani kama ntakuwa nakukwaza.
Mifuko ya hifadhi ya jamii mafao yake huwa wanafata muongozo kutoka ILO, kuna recommendations za ILO ukipata muda soma (102. Social Security (Minimum Standards) Convention, 1952.) Hii inataka mifuko yote ya jamii kutoa mafao yasiyopungua 9, sasa kwa nchi kama Tanzania mifuko yote inaoperate below standards.
Sasa kwenye ishu ya fao la kujitoa, kwenye targets za social security fao la kujitoa halitakiwi sababu mtu ukishamtoa kwenye mfumo wa social security hatma yake uzeeni ni nin!?, instead inatakiwa umpe fao la kukosa ajira (unemployment benefit) ambalo ILO pia wakarecommend, utapewa unemployment benefit wakiamini kwamba ipo siku utapata ajira au utajiari hivyo utaendelea kuchangia mifuko ya jamii kuweka akiba yako uzeeni ili uje upate annuity (old age pension).
Lakini hata hao waliopewa redundancy kama wanapata mafao yao ya kujitoa basi mifuko haipo fair inabidi na waliofukuzwa wapewe pia. Hapo ndo nilikuwa sijui kwahyo kama ni hivyo mnaweza mkapeleka malalamiko yenu and am sure mtafanikiwa. Ila kiukweli hadi upewe hilo fao ni kwamba ithibitike hutoajiriwa tena, sijui kama ntakuwa nimeeleweka nashindwa niliweke vipi sawa
 
Samahani naomba nichangie ninachokifahamu kidogo kuhusu hifadhi ya jamii, samahani kama ntakuwa nakukwaza.
Mifuko ya hifadhi ya jamii mafao yake huwa wanafata muongozo kutoka ILO, kuna recommendations za ILO ukipata muda soma (102. Social Security (Minimum Standards) Convention, 1952.) Hii inataka mifuko yote ya jamii kutoa mafao yasiyopungua 9, sasa kwa nchi kama Tanzania mifuko yote inaoperate below standards.
Sasa kwenye ishu ya fao la kujitoa, kwenye targets za social security fao la kujitoa halitakiwi sababu mtu ukishamtoa kwenye mfumo wa social security hatma yake uzeeni ni nin!?, instead inatakiwa umpe fao la kukosa ajira (unemployment benefit) ambalo ILO pia wakarecommend, utapewa unemployment benefit wakiamini kwamba ipo siku utapata ajira au utajiari hivyo utaendelea kuchangia mifuko ya jamii kuweka akiba yako uzeeni ili uje upate annuity (old age pension).
Lakini hata hao waliopewa redundancy kama wanapata mafao yao ya kujitoa basi mifuko haipo fair inabidi na waliofukuzwa wapewe pia. Hapo ndo nilikuwa sijui kwahyo kama ni hivyo mnaweza mkapeleka malalamiko yenu and am sure mtafanikiwa. Ila kiukweli hadi upewe hilo fao ni kwamba ithibitike hutoajiriwa tena, sijui kama ntakuwa nimeeleweka nashindwa niliweke vipi sawa


64GB, hili sula kiukweli haliko clear hata huko serikalini kwa hao wakubwa, nina amini mkuu wa nchi akilijua hili kwa ufasaha, kuna watu watafukuzwa kazi. Maana wanatengeneza mgogoro kati ya wananchi na raia, hii maana yake ni kwamba wapo raia wataichukia serikali wakiamini ndiyo inayosababisha PPF kuwa na kiburi hiki, kitu ambacho si kweli.

Hawa PPF kiukweli wana mizengwe, na ni kweli kuwa wanafanya ubaguzi. Mtu akifukuzwa kazini hawampi mafao yake, ila yule aliyepunguzwa kazini anapewa. Sasa mimi nilipata taabu sana hapa kuwaelewa. Kwamba, yule amepunguzwa mimi nimefukuzwa, kipi kinafanya mimi niliofukuzwa kiwaaminishe PPF kuwa nitapata tena kazi, na kipi kinafanya PPF waamini kuwa yule aliyepunguzwa kazini hatokuja kupata kazi au ajira milele ilihali umri wetu ni ule ule tena wengine ni wadogo hata kwa miaka mitano tofauti na mimi? Ukijiuliza maswali haya, na ukawa na RAM ya GB64 kama ya kwako, hakika utaenda mahakani. Kwa sababu hakuna mantiki hapa. Ndiyo maana na mimi nikasema kuwa, lzima niungane na Ndugu Bunny Wailer kwa hili, maana amenifumbua macho.
 
Samahani naomba nichangie ninachokifahamu kidogo kuhusu hifadhi ya jamii, samahani kama ntakuwa nakukwaza.
Mifuko ya hifadhi ya jamii mafao yake huwa wanafata muongozo kutoka ILO, kuna recommendations za ILO ukipata muda soma (102. Social Security (Minimum Standards) Convention, 1952.) Hii inataka mifuko yote ya jamii kutoa mafao yasiyopungua 9, sasa kwa nchi kama Tanzania mifuko yote inaoperate below standards.
Sasa kwenye ishu ya fao la kujitoa, kwenye targets za social security fao la kujitoa halitakiwi sababu mtu ukishamtoa kwenye mfumo wa social security hatma yake uzeeni ni nin!?, instead inatakiwa umpe fao la kukosa ajira (unemployment benefit) ambalo ILO pia wakarecommend, utapewa unemployment benefit wakiamini kwamba ipo siku utapata ajira au utajiari hivyo utaendelea kuchangia mifuko ya jamii kuweka akiba yako uzeeni ili uje upate annuity (old age pension).
Lakini hata hao waliopewa redundancy kama wanapata mafao yao ya kujitoa basi mifuko haipo fair inabidi na waliofukuzwa wapewe pia. Hapo ndo nilikuwa sijui kwahyo kama ni hivyo mnaweza mkapeleka malalamiko yenu and am sure mtafanikiwa. Ila kiukweli hadi upewe hilo fao ni kwamba ithibitike hutoajiriwa tena, sijui kama ntakuwa nimeeleweka nashindwa niliweke vipi sawa

64Gb.......ingekuwa kwamba waliofukuzwa na waliopunguzwa hawapewi, mimi nisingehangaika; ningejua ni suala la wote. Ila kilichonisukuma hasa baada ya kupata shauri wa kwenda kortini ni ule ubaguzi. Kwamba wanaopunguzwa wanapewa halafu waliofukuzwa akina mimi hatupewi. Hiyo ndiyo complaint yangu kuu, na hata huyo aliyenieleza na kushauri kuwa niende mahakamani, alisisitizia hilo la ubaguzi, kwamba hapo hakuna fairness bali ukiritimba tu. Sasa hadi naleta huu mjadala kwenu ni kutaka tu kupata muongozo wa namna gani nawasilisha hili shauri mahakamani. Sina hela ya kumlipa mwanasheria je, kwa mazingira haya inakuaje? Dragon amelifafanua hili japokuwa hajaliweka vizuri, hivyo kama anasoma commet yangu hii, naomba anipe ufafanuzi ulio wazi zaidi maana alioutoa umekaa kisheria sheria na si wote tunajua sheria. Kadhalika kwa aliye na ufahamu wa mambo ya sheria namuomba pia achangie ili kufanya njia nitakayopita isiwe na mabonde, na mashimo mengi.
 
Pole sana kaka.
Kufungua kesi ndio salama yako ila hela ndio shida tena...hauna ndugu ama rafiki ambaye ni mwanasheria ambaye anaweza kukusaidia angalau kipindi hiki
 
64Gb.......ingekuwa kwamba waliofukuzwa na waliopunguzwa hawapewi, mimi nisingehangaika; ningejua ni suala la wote. Ila kilichonisukuma hasa baada ya kupata shauri wa kwenda kortini ni ule ubaguzi. Kwamba wanaopunguzwa wanapewa halafu waliofukuzwa akina mimi hatupewi. Hiyo ndiyo complaint yangu kuu, na hata huyo aliyenieleza na kushauri kuwa niende mahakamani, alisisitizia hilo la ubaguzi, kwamba hapo hakuna fairness bali ukiritimba tu. Sasa hadi naleta huu mjadala kwenu ni kutaka tu kupata muongozo wa namna gani nawasilisha hili shauri mahakamani. Sina hela ya kumlipa mwanasheria je, kwa mazingira haya inakuaje? Dragon amelifafanua hili japokuwa hajaliweka vizuri, hivyo kama anasoma commet yangu hii, naomba anipe ufafanuzi ulio wazi zaidi maana alioutoa umekaa kisheria sheria na si wote tunajua sheria. Kadhalika kwa aliye na ufahamu wa mambo ya sheria namuomba pia achangie ili kufanya njia nitakayopita isiwe na mabonde, na mashimo mengi.
Pole sana mkuu, kama upo dar jaribu kwenda SSRA maana hawa pia wanamamlaka ya kutatua matatizo kati ya Member na scheme pia wapo kulinda na kutetea haki za mwanachama. Huko hutotumia pesa ila kama ukishindwa huko fanya utaratibu fikisha mahakamani haki itatendeka
 
Ulivyokuwa na ajira hukukumbuka kuweka akiba? Pole sana...

Hivi kama anadai ana milioni mbili na laki kadhaa, unadhani mtu huyu alikuwa na anapokea net salary kiasi gani? Haujui kwamba wafanyakazi walio wengi kinachopatikana huishia tumboni, kwenye kodi ya nyumba (kama hajajenga), usafiri? Haujui kuwa kuna watu hadi leo hii wanalipwa laki moja na nusu? Kwa mshahara wa laki moja na nusu na ukute labda anaishi Dar, unafikiri ata-save nini hapo? Tunapojibu tuangalie namna ya kumjibu mtu kulingana na wakati na mazingira ndugu. Si kila kitu ni mzaha kama ilivyo mizaha kwenye jina lako.
 
Hivi kama anadai ana milioni mbili na laki kadhaa, unadhani mtu huyu alikuwa na anapokea net salary kiasi gani? Haujui kwamba wafanyakazi walio wengi kinachopatikana huishia tumboni, kwenye kodi ya nyumba (kama hajajenga), usafiri? Haujui kuwa kuna watu hadi leo hii wanalipwa laki moja na nusu? Kwa mshahara wa laki moja na nusu na ukute labda anaishi Dar, unafikiri ata-save nini hapo? Tunapojibu tuangalie namna ya kumjibu mtu kulingana na wakati na mazingira ndugu. Si kila kitu ni mzaha kama ilivyo mizaha kwenye jina lako.
Kweli mkuu! Hata mie mkataba wangu uliwahi kusitishwa nikiwa na pesa isiyozidi buku hamsini mfukoni, na nilikuwa napokea mshahara mzuri tu. Haya mambo omba uyasikie kwa mwenzio. Kilichonichanganya zaidi kodi ilikuwa inaisha wiki chache baadaye!
Yani, there are days and moments in life I dont want to remember, this one was one of those... Tena usiombe uachishwe kazi huku ukiwa na mali kibao za kampuni kama gari, laptop, uniform, everybody will know...
 
Back
Top Bottom