Nataka Nianze Biashara ya Kupaka Rangi Kucha za kina Dada Chuoni kwetu

wamidosho

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2015
Posts
456
Reaction score
424
Heshima kwenu wakuu!!

Mimi ni mwanafunzi jinsia ya kiume wa chuo kikuu kimojawapo kinachopatikana katika mkoa wa Morogoro,Nategemea kuingia mwaka wa tatu mwaka huu hapo October.

Kutokana na fursa zinazonizunguka hapa chuoni kwetu nimeona hii Biashara ya kuwapaka Rangi wanachuo wenzangu especially kina Dada.Nimeona kama fursa kwangu ya kujiajiri,kuniongezea kipato huku nasoma na pia njia ya kujiandalia mazingira pale nitakapo hitimu masomo yangu.

Njia niliyofikiria ya kuwafikia haraka wateja wangu ni kuwatembelea kwenye hostel zao kila chumba.Pia muda sahihi niliona utafaa ili nisijichanganye na masomo yangu nitakuwa nautumia pale ambapo nitakuwa sina kipindi darasani wakati huo na siku za weekend.Najua changamoto lazima zitakuwepo ila nishajiandaa kisaikolojia kukabiliana nazo.

Mana hili wazo nilikuwa nalo tokea naingia mwaka wa pili ila nilijikatisha TAMAA😰 mwenyewe Kwa kuhofia Watu watanionaje,ila Kwa sasa nimedhamilia Kwa moyo wangu kuianza Biashara hii pindi chuo kikifungua.

Wakuu nachohitaji kutoka kwenu naomba mwenye mawazo,ushauri juu ya Biashara hii pia mwenye kujua vifaa muhimu kama uv light na vingine vingine vitakavyotumia kwenye Kazi ya kupaka rangi kucha pia aina za Rangi zinazotumika na bei zake.

Kwasasa Kwa kuanza nimeanza kufanya research baadhi Kwa kuangalia Google,YouTube tutorial zao,pia nahitaji mchango wenu Wana JF wenzangu juu ya swala hili ili kunisaidia mdogo wenu.

ASANTENI NA MUNGU AWABARIKI🙏🙏
 
Fanya na kusuka raster utapiga ela balaa!
 
Nunua na bidhaa nyingine za urembo wanazopenda halafu wakopeshe ili wakulipe boom linapotoka! Wasipokulipa unaenda kuwashtaki kwa Warden au Waziri wa mikopo wa chuo.
 
Nunua na bidhaa nyingine za urembo wanazopenda halafu wakopeshe ili wakulipe boom linapotoka! Wasipokulipa unaenda kuwashtaki kwa Warden au Waziri wa mikopo wa chuo.


Sawa mkuu asante
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] umenishawishi mkuu, na mm ntaanza ila mtaani, sema jomba nipe direction, mtaji apa mtaani kuna mtu ua naona ana wateja balaa.


mtaji ni kama sh.ngapi na mm ni mwanachuo ka wewe ila naingia mwaka wa 2 sema chuo chetu kina watu wachache sana, apa dar es salaam
 
daah, utawala sana, tena watoto wa chuo wanakuaga wakali kinoma
usisahau ndom tu mkuu
 
hivi ukiwa na wazo alafu ukalifanyia kazi nn kitapungua ? mbona mpaka ulilete huku ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…