Nataka niwe mke wa pili

Wife kanikuta nafuatilia hii thread kanuna uyoo dyuu
 
Itaje kwa jina hiyo degree yako.
 
Siamini kama soko lako limeshuka kiasi hiki khaa? Kweli jpm katunhonyoa manyoya wengi aisee
 
Kila lakheri my dia.. ukishaingia ndoani uje utupe mrejesho!! Maana uke wenza mtihani kweli.
 
wakristo mnaruhusiwa mitala kwani?
 
Ni mme yeyote au unataka wa kiwango chako cha education ?wenzio wa aina yako husema hata huyo awe wa aina gani mfupi:Mfanya biashara ,Muajiriwa nk?wewe unata mme huyo awe na uwezo gani?Kielimu/Kazi?
 
Tatizo ushaanza na neno kulishwa, ukumbuke humuoi aje umlishe tuu,. Na kwa kigezo hicho kwa anaejua kuwaoa hao imekua ni kujipalilia makaa. Watakuigizia mpaka basi
Ndio nakwambia sasa, wapo vijana wengi tu wa form 4 wamewaoa na ndoa zao zipo vizuri tu. Wasiwasi wako tu wa kuwaogopa; pichu hainaga degree kaka.
 
Wewe utakuwa huna hamu ya kufanya tendo. Huo umri unapata mwenza wako ambaye hajaoa, kwanini unataka uwe wa pili??? Au mahubiri yamekuingia sana kwamba umeamua kujishusha ili Mungu akuinue?
1. Umetoa ujauzito mara ngapi?
2. Umekuwa na boyfrinds wangapi?
3. Umetumia kitanzi/dawa za kuzuia mimba mara ngapi?
4. Je una matatizo mengine yeyote ya kiafya ama mengineyo?


5. Sifa za mtu anayetaka/anayelazimika kuwa mke wa pili wa mtu ni;
a) Yule ambaye ana umri kuanzia 30 na kuendelea
b) Ambaye mwenzi wake amefariki dunia
c) Dada ambaye bahati nzuri/mbaya hakupata mtu wa kumuoa Ktk umri wake wa kuchipua
d) Ni yule ambaye anapenda kuwa hivyo kwa ridhaa yake mwenyewe
e) Na mengine ya kifamilia
f) Ni vile wanaume wenye sifa za kuoa wanapokuwa wachache na hawapatikani

Sasa wewe kwanini unataka ndoa ya namna hiyo?... Ueleze Umma wa Watanzania

Na sifa za umtakaye uziseme hapa ukiorodhesha zote kwa mapana yake.
 
hongera kwa kujitambua
 
Tayari wameanza kumuelewa Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema.... Wamehangaika sana bt wanarudi pale pale Na ndio ukweli huo wanaume wanahitaji mke zaidi ya mmoja kutokana na ratio Mola aliyoiweka mwenyew... Alilijua hili mapema ila wanadam sisi tunajifanya wajuaji
 
Heee jamani kulikoni tena, hadi mtu kiwa tayari kuwa mke wa pili…mmmmhhh

Wenye mmeowa kazi kwenu hapo
 
mtu anaanzaje kufikiria kuwa mke wa pili kama amepata wake mwenyewe? ukiona hivyo ujue kakosa wake mwenyewe na anatamani apate hata wa mtu hiyo inaitwa tutabanana hapahapa.
Binadamu hatufanani hata kidogo aisee, kuna vitu watu huwa wanavitaka ukiambiwa unaweza kushangaa ila ndo hivyo.
 
Ni marufuku kukata tamaa ,we una 27 unatamani uwe mke wa Pili? Tumia maarifa uliyopata kuutafuta Uso wa Mungu atakupa mwenza wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…