Natamani kumiliki biashara yangu

bribrii

Senior Member
Joined
Jan 25, 2014
Posts
110
Reaction score
21
mimi ni msichana,ni mwanafunzi katika chuo kikuu fulana hapa nchini mwaka wa kwanza napenda kumiliki biashara yangu mwenyewe .lakini tatizo pesa,sina mtaji wa kuniwezesha.kutimiza lengo langu .msaada wa kimawazo tafadhari mnisaidie niweze kutimiza malengo yangu.
 
Wewe unahisi ukiwa na kiasi gani ndio utaanza biashara? Pia ni biashara gani unayopanga kufanya.

Je uwa unapenda kufanya nini?

Nijibu hayo niendelee
 
Pamoja na majibu utakayompa money stunna. Nakushauri anza kujibana mapema angalau kwa kuweka akiba boom lako unalopata, kanyoe nywele zote kichwani ili kupunguza gharama za kusuka, vipedo usinunue, chips mayai pungua.....ninaimani baadaya ya miaka yako chuoni utakuwa umepata kianzio.
 
Soma kwanza kama ulivyoamua.Biashara itafuata.
Maana bado mdogo sana na ukizingatia ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza.

Na mbaya zaidi umejitambulisha msichana,wapo watu watataka wakupe pesa na yao yawe.Maisha ya chuo tunayajua yalivyo.

Pili inabidi uweke wazo lako hapa la Biashara gani unayotaka kumiliki ili watu wakupe mpango kazi wa muda mrefu kisha hapo mbele utaamua.
Maaa kila mtu anawazo la biashara na liktokea Tangazo la mtu anasema anatoa mtaji bila masharti Nchi nzima itahamia kwake.
 
Fikiria ni biashara gani utafanya.Kama utahitaji kufungua kampuni au formal business unitafute nikusaidie ili uweze kutimiza ndoto yako.Mimi ni mtaalam wa mambo hayo haswa kwenye kuandaa documents kama Memorandum & Articles of Association,Business Plan etc.Nitakuhudumia probono kwa vile wewe ni mwanachuo.Hongera kwa kufikiria kuwa mjasiria mali.Ni bora kujiajiri ukimaliza chuo badala ya kuhangaika ukitafuta jobu ambazo kupata ni ngumu
 
Uza viwalo vikali first grade, visendoz na vipodozi hapo chuoni we uwe mcheshi tu utatoka mno.

Au chora wasichana wenzio kucha hapo mkono mmoja buku.

Mtaji kuanzia wa nguo ni elfu 30 hadi 50 sidhani kama utakosa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…