Mwanamke mmoja tu yenyewe lakini Ni Kama vile anataka kunishinda.tatizo kubwa lipo mfukoni Sina kitu Sina hela,Nina wallet tu nimeijaza makaratasi ukiifungua hakuna kitu.kwa mfano Sasa hivi hapa nilipo huwezi kuamini Nina 1200 tu ndo nayomiliki nadhani mmenielewa.nyakati nyingine ni kweli wanaume wenzangu mpo sahihi mnaposhauri kuwa na mwanamke mmoja Ni kujipalilia ma pressure kwa hiyo angalau uwe na wa pembeni mpango wa kando.tatizo nawaza nitampa Nini huyu wa pembeni maana kwa Hali ya Sasa ukisema tu uspend 30000 na demu ukaimaliza yote kuja kuipata 30000 nyingine Ni mtihani shekhe!tusio na pesa sijui tunaonekanaje mbele ya wadada na kwa inavyooenekana hela zitaanza kuonekana awamu ya pili ya Magufuli 2020 huko ndo Mambo yatakaa sawa.kwa kweli niwape pongezi wanaume wote wenye michepuko nyie ndo wanaume Bhana wanaume wa shoka mnaojiweza mnatuwakilisha vema.endeleeni kutusukumia siku na mademu zetu Ila msiwagonge Sana sisi huku roho zinauma.