Natamani sana kumjua zaidi Siti Binti Saad

Natamani sana kumjua zaidi Siti Binti Saad

Jembebutu

Member
Joined
Feb 14, 2017
Posts
88
Reaction score
225
Wanajukwaa,

Nimesikia machache sana na kuvutiwa na hadithi za nguli wa muziki wa Taarab hapa nyumbani Sinti binti Saad. Naomba kumjua zaidi miaka aliyovuma, muziki wake, haiba na mengine mengi.
 
Nakushauri mkuu menda youtube tafta historia yake wameweka kwa simulizi ya sauti saafi sana
 
Kwa ufupi Alizaliwa Fumbwe zanzibar,kipaji chake kilijidhihirisha pale alipokuwa anatembeza vyungu mitaani ambapo alikuwa anaimba kwa sauti nzuri sana na yenye pitch kubwa ya kike alipokuwa ananadi bidhaa zake baadae alisajiliwa Columbia Records(ambayo hivi karibuni ilisimamia kazi za wanamuziki kama Adele, Mariah Carey, celine Dion) ambapo alirekodi album yake ya kwanza kwa lugha ya kiswahili na kuwa msanii wa kwanza wa kike kuimba kwa lugha hiyo badala ya kiarabu kama ilivyozoeleka alitamba na nyimbo kama wewe paka,njia ugurusumbwe,uchungu wa mwana, nilikwenda matembezi pamoja na muhogo wa Jang'ombe na nyingine nyingi.
 
Shaaban Robert aliandika kitabu ‘Wasifu wa Siti binti Sadi’ ndipo taarifa zake zinapopatikana kwa uhakika.

Nimewahi kusikia yule aliyekuwa mmiliki wa kikundi cha East African Melody ambaye pia alikuwa mtunzi na muimbaji mzuri (sasa hivi marehemu) ni mjukuu wake.
 
1629402499534.png

Siti binti Saad
 
Jembebutu Shaaban Robert aliandika kitabu kumhusu. kinaitwa Wasifu wa Siti binti Saad. Unaweza kukisoma bure ndani ya maktaba app. pitia huu uzi, kwenye post no 16 kuna link ya app ya playstore. install ujisomee hicho na vingine vingi bure, karibu.
 
Back
Top Bottom