Natatizwa na matumizi ya maneno Kundi na Kikundi.

Natatizwa na matumizi ya maneno Kundi na Kikundi.

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,703
Reaction score
1,724
Pamoja na sintofahamu ya maneno hayo ninayokutana nayo lakini hii sasa inapelekea kukosa umakini wa maneno hasa Kundi na Kikundi.
Kawaida kwenye vyombo vya habari hasa DW au BBC lugha ya Kiswahili husikia wakitamka Kundi la Taliban la huko Afghanistan.
Jana kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku Star TV nikasikia mtangazaji akisema Kikundi cha Taliban. Nikajiuliza hivi Taliban pamoja na kuchukua uongozi wa nchi ya Afghanistan bado ni Kikundi tu?
Labda mie sielewi tofauti ya maneno haya, naomba msaada.
 
Pamoja na sintofahamu ya maneno hayo ninayokutana nayo lakini hii sasa inapelekea kukosa umakini wa maneno hasa Kundi na Kikundi.
Kawaida kwenye vyombo vya habari hasa DW au BBC lugha ya Kiswahili husikia wakitamka Kundi la Taliban la huko Afghanistan.
Jana kwenye taarifa ya habari ya saa mbili usiku Star TV nikasikia mtangazaji akisema Kikundi cha Taliban. Nikajiuliza hivi Taliban pamoja na kuchukua uongozi wa nchi ya Afghanistan bado ni Kikundi tu?
Labda mie sielewi tofauti ya maneno haya, naomba msaada.


Kundi ni kubwa na kikundi ni kundi dogo, na hiyo inatumika kwa kulinganisha na kundi jingine.

Mfano unaweza sema; Chadema ni kundi kubwa la wanachama lakini CCM ni kikundi kidogo tu cha wanachama.

Ni mfano tu 🤣🤣
 
Kundi ni kubwa na kikundi ni kundi dogo, na hiyo inatumika kwa kulinganisha na kundi jingine.

Mfano unaweza sema; Chadema ni kundi kubwa la wanachama lakini CCM ni kikundi kidogo tu cha wanachama.

Ni mfano tu 🤣🤣
Yeah mkuu, hata mie nafahamu kuwa:-
1. Kundi ni kuwa na idadi kubwa ya watu/vitu na
2. Kikundi ni kuwa na idadi ndogo ya watu/vitu.
Nimeambiwa idadi ndogo huwa haizidi 50.
 
Yeah mkuu, hata mie nafahamu kuwa:-
1. Kundi ni kuwa na idadi kubwa ya watu/vitu na
2. Kikundi ni kuwa na idadi ndogo ya watu/vitu.
Nimeambiwa idadi ndogo huwa haizidi 50.


Idadi ndogo au kubwa inapatikana kwa kulinganisha (mlinganisho), yaani ni lazima kuwepo na idadi ya vitu tofauti katika sehemu tofauti ndipo unapoweza kusema idadi hii ni ndogo au kubwa kulingana na idadi ya vitu fulani katika eneo fulani.

Kwenye kikundi na kundi ni lazima pawepo na makundi mawili au zaidi tofauti ndipo unapoweza kusema hili ni kundi na hiki ni kikundi.
 
Idadi ndogo au kubwa inapatikana kwa kulinganisha (mlinganisho), yaani ni lazima kuwepo na idadi ya vitu tofauti katika sehemu tofauti ndipo unapoweza kusema idadi hii ni ndogo au kubwa kulingana na idadi ya vitu fulani katika eneo fulani.

Kwenye kikundi na kundi ni lazima pawepo na makundi mawili au zaidi tofauti ndipo unapoweza kusema hili ni kundi na hiki ni kikundi.
Nawasikia sasa hawa Star TV wakiitambua Taribani kama KUNDI na si Kikundi.
 
Nasi tulipokuwa katika usajili wa group la kusaidiana miaka 5 ilopita,

Tuliambiwa tumesajili "kikundi" maana tuko wanachama 35.

Tukaambiwa kundi ni idadi jumuishi ya watu wengi sana kama kuanzia 60, 80, 100 na kuendelea.

Jacobus
 
Back
Top Bottom