Natengeneza magari na vifaa vya kisasa kabisa DSM

NI MTAZAMO TU

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2014
Posts
1,203
Reaction score
999
Nimerudi toka ughaibuni ,vijana wanaita mbele ambako nilikuwa nisoma machenical egr miaka 4 na nimefanya kazi zaidi ya miaka 6 kutafuta uzoefu..

Nimekuja kwaajili ya kuendeleza Taifa letu, karibuni tushirikiane kutatua matizo ya magari yatu kwa pamoja..

Nipigie kwa mamba hii 0715784787 hapa Dsm haswa magari madogo sollon car..
 
Tutakaribia mkuu ila ungevitaja hvyo vifaa na kuweka picha na ufanyaji kazi weke tusije tukakimbia tulipo kumbe ndo yale yale
Pili unatakiwa useme ofic ilipo sio namba za cmu au unafanyia gari lilipo?
 
Nasikia kuna kitu kinaitwa throtle cleaning, hiyo inatakiwa ifanyike kila baada ya muda gani na kwa kigari kama toyota passo inaweza kwenda sh ngapi hivi
 
Kuweka tangazo hapa jukwaani ni bure kabisa...

Ajabu ni kwamba waweka matangazo huwa wanabania kuweka maelezo ya kutosha utadhani "keyboards" zao zinatumia wino...

Hivi unadhani watu wana muda wa kukutafuta kwa simu ikiwa mtu mwenye kutafuta wateja hutoi maelezo muhimu kama aina ya magari uwezayo kutengeneza, mahali ofisi zako zilipo, muda unaofungua na kufunga ofisi yako n.k
 
Poleni sana kwa maelezo yasio jitosheleza, lakini najibu maswali ya wadau wote.

1.sina ofisi ila ukiniita nakuja ulipo na vifaa vyangu.

2.vifaa sio tatizo tatizo ni uwezo wa fundi kufanya hizo service za magari wadau.

Na magari ambayo ninatengeza ni aina zote sollon Gar.

4.Ambaye atakuwa serious na kazi naomba tufanye kazi wadau.

Asante kwa ushirikiano wenu wakuu..
 
Mkuu, Jitahidi kufungua garage ndio italipa vizuri.

Ukiwa na muda karibu kwenye hii thread kutoa mchango wako kuhusu kozi za engineering:https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...ich-engineering-field-has-the-best-scope.html
 
we umesoma tena umesomea mbele unashindwa kuwa hata na website ndogo tu? walau hata facebook?
 

ndugu kuwa serious kidogo. kuna kazi unaweza kuja kufanya nyumbani kwa mteja na kuna kazi huwezi kufanya nyumbani kwa mteja??? sababu kuna kazi ni chafu zinahitaji garage,utamwaga oil na kusababisha parking yangu kuwa garage.

kuna kazi zinahitaji gari iinuliwe juu ndio zifanyika kwa urahisii sasa nyumbani kwangu utatumia nini jeki?? fungua garage kaka.
 
Asante sana wakuu, ila mwanzo mgumu mkumbuke,maana tatizo kubwa eneo ndio pasua kichwa hapa DSM.
 
Ni kweli, touch screen zimeleta majanga ktk uandishi makini. Lakini pale kila bandiko linapokuwa na makosa haya linapunguza credibility
TUJARIBU KU EDIT POSTS ZETU KABLA YA KUZITUMA
 

tafuta eneo uweke garage, sivyo kazi bado!
umesema umesoma chuo gani vile?
 

naona bado hajaamua kufanya kazi. kama mtaji utata na anajiamini atafute wadau wafanye makubaliano atapata sehem ya kazi na vifaa!
 
Nashukuru sana kwa ushauri wenu juu ya Garage wakubwa
 
Nissan Xtrail yangu inasumbua ktk kubadili gia.Unatibu gari kabila hiyo?
 
Mkuu mooza asante kwa kunipigia na tukimaliza kazi yako naomba uwajulishe wana JF mafanikio ya kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…