Naomba nianze nukuu mbili za waziri mkuu mstaafu EL alizotoa bungeni wakati akichangia repoti ya iliyokuwa kamati teule chini ya uenyekiti wa mtunzi wa kitabu cha "Pepo ya Mabwege" ndg. H. Mwakyembe.
"Mheshimiwa Dk. Mwakyembe ni Mwanasheria, tena Daktari alikuwa anafundisha Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni "Natural Justice". Mheshimiwa Spika, wewe ni Mwanasheria unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani, wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja kati ya watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja"
Nukuu ya pili ni hii
"Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa makini sana jambo hili nikajiuliza hivi kulikoni mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo kulikoni?"
Mwenyekiti wa kamati teule wakati anahitimisha hoja yake alisema kuwa hawakumuhoji kwa vile walijua kutokana na wadhifa wake anaweza kuharibu ushahidi.
Swali ni je natural justice ni haki ya mtuhumiwa yeyote au inategemea na status yake ili hali no one is above the law?
"Mheshimiwa Dk. Mwakyembe ni Mwanasheria, tena Daktari alikuwa anafundisha Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni "Natural Justice". Mheshimiwa Spika, wewe ni Mwanasheria unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani, wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja kati ya watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja"
Nukuu ya pili ni hii
"Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa makini sana jambo hili nikajiuliza hivi kulikoni mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo kulikoni?"
Mwenyekiti wa kamati teule wakati anahitimisha hoja yake alisema kuwa hawakumuhoji kwa vile walijua kutokana na wadhifa wake anaweza kuharibu ushahidi.
Swali ni je natural justice ni haki ya mtuhumiwa yeyote au inategemea na status yake ili hali no one is above the law?