Naunga mkono wanaokataa kutoa ushirikiano kwa Ulinzi Shirikishi wachukuliwe hatua na wapelekwe Mahakamani

Naunga mkono wanaokataa kutoa ushirikiano kwa Ulinzi Shirikishi wachukuliwe hatua na wapelekwe Mahakamani

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Huku mtaani kwetu suala la ulinzi shirikishi ni kama limekuwa linachukuliwa poapoa hivi, kuna wengine wao wanajiona wapo salama labda kutokana na mazingira yao ya nyumba zao kuwa na geti au kuwa na walinzi.

Wengine wanaona ni ubahiri kutoa fedha kwa vijana au watu wanaofanya kazi ya kulinda mtaani usiku, ni wazi kuwa inawezekana haipo kisheria lakini hiyo haimaanishi kuwa siyo kazi nyepesi.

Mara kadhaa nimeona viongozi wetu wa Serikali za mtaa wanaanzisha kampeni hiyo ya kulinda lakini wale wanaojiona wajanja wanapotezea kutoa ushirikiano, hii siyo sawa.

Nimeona Serikali ya mtaa flani hivi Kijitonyama wanasema kuwa wale ambao hawatalipa fedha kama motisha kwa vijana wanaolinda watawapeleka Mahakamani, mimi binafsi naunga mkono hoja hiyo.

Haohao wanaogoma siku wakivamiwa au wakiibiwa ndio wanakuwa wa kwanza kutoa lawama kwa Polisi na Serikali, hivi wanadhani Serikali na Polisi zitakuwa na kazi ya kumlinda kila mtu muda wote?

Mambo mengine tujiongeze tu wenyewe tu tutumie akili za kuzaliwa, siyo kila kitu iwe sheria.

Pia soma: Kijitonyama: Wananchi wanaokataa kulipia ulinzi shirikishi kupelekwa Mahakamani
 
Nimeona Serikali ya mtaa flani hivi Kijitonyama wanasema kuwa wale ambao hawatalipa fedha kama motisha kwa vijana wanaolinda watawapeleka Mahakamani, mimi binafsi naunga mkono hoja hiyo.

Haohao wanaogoma siku wakivamiwa au wakiibiwa ndio wanakuwa wa kwanza kutoa lawama kwa Polisi na Serikali, hivi wanadhani Serikali na Polisi zitakuwa na kazi ya kumlinda kila mtu muda wote?
Kwahiyo na wao wakisema tutalipa kodi kwajinsi tutakavyo au tunapojiskia ndio usawa?
Kila mutu atimize wajibu wake,
Kuwashtaki wanaogoma juchangia ni udikteta na kuwaonea
 
Sista karibia ameahaibiwa karibia TV tatu hapo nyumbani na hakuna hata amewahi kuipata. Hao watu wanalinda wapi, Kuna uhakika gani kuwa kweli wanalinda au ni aina nyingine ya wizi
 
Halafu hao shirikishi wenyewe wengi ndio hao hao vibaka, kwa taarifa yako wanakamata hadi vibali vya ujenzi na mizigo barabarani kama tra vilee na ukibisha au kuhoji chochote unakula kichapo,

Hii ni kariakoo mtaa wa misheni kota. Labda na wewe uwe unaponea hapo hapo ila hawa ni wa kupigwa vita au waajiriwe kama polisi kamili
 
Kazi ya kumlinda Raia na mali zake ni kazi ya vyombo vya dola ambavyo viko chini ya serikali, habari ya sungusungu sijui mgambo wachangiwe na wananchi haohao wanaotoa tozo sio sawa mwananchi alipe kodi, uanzishwe mpango kazi wa kila mtaa au kitongoji wawekwe hao shirikishi ambao fungu lao watakua wanafuata kwa OCD au mkuu wa kituo cha karibu, hiyo pesa itoke mambo ya ndani kama posho ya walinzi wa usalama kutoka makundi ya kiraia au jeshi la akiba mgambo,
 
Halafu hao shirikishi wenyewe wengi ndio hao hao vibaka, kwa taarifa yako wanakamata hadi vibali vya ujenzi na mizigo barabarani kama tra vilee na ukibisha au kuhoji chochote unakula kichapo,
Hii ni kariakoo mtaa wa misheni kota,
Labda na wewe uwe unaponea hapo hapo ila hawa ni wa kupigwa vita au waajiriwe kama polisi kamili

Shirikishi wengi ndio wachora ramani kwa wezi, hata wewe ukikaa vibaya wanakuibia tu bila huruma, kwanza walevi, wezi, wavuta bange ndio haohao shirikishi, na sio sahihi mwananchi kuchangia majukumu yasiyo yake
 
Kazi ya kumlinda Raia na mali zake ni kazi ya vyombo vya dola ambavyo viko chini ya serikali, habari ya sungusungu sijui mgambo wachangiwe na wananchi haohao wanaotoa tozo sio sawa mwananchi alipe kodi, uanzishwe mpango kazi wa kila mtaa au kitongoji wawekwe hao shirikishi ambao fungu lao watakua wanafuata kwa OCD au mkuu wa kituo cha karibu, hiyo pesa itoke mambo ya ndani kama posho ya walinzi wa usalama kutoka makundi ya kiraia au jeshi la akiba mgambo,
Sahihi kabisa, yaani kodi na tozo wachukue halafu bado wafanyakazi wao tuwalipe sie mshahara? Huku ni kufeli kukubwa
 
Yaani nikatwe kodi Tsh500,000/= kwenye mshahara kila mwezi halafu nichangie Tsh2,000/= eti ya Sungusungu kwani hio pesa ya makato ya kodi inaenda wapi?
 
Yaani nikatwe kodi Tsh500,000/= kwenye mshahara kila mwezi halafu nichangie Tsh2,000/= eti ya Sungusungu kwani hio pesa ya makato ya kodi inaenda wapi?
😁😁 wadau hapa tutaanza calculation za kujua basic salary

Hiyo ngoma ni ya 2.5 hivi 😝
 
Hamjui kuanzisha jeshi au chombo kinachofanya kazi ya jeshi ni kosa tena la kikatiba huo ulinzi shirikishi ungewezeshwa na polisi wawachague wale ma informer wao wawape hizo kazi na tunao polisi wengi tu wanalewa usiku kwenye doria kwann wao wasiwe wanafanya patrol kama kazi yao inavyotaka
 
Kazi ya kumlinda Raia na mali zake ni kazi ya vyombo vya dola ambavyo viko chini ya serikali, habari ya sungusungu sijui mgambo wachangiwe na wananchi haohao wanaotoa tozo sio sawa mwananchi alipe kodi, uanzishwe mpango kazi wa kila mtaa au kitongoji wawekwe hao shirikishi ambao fungu lao watakua wanafuata kwa OCD au mkuu wa kituo cha karibu, hiyo pesa itoke mambo ya ndani kama posho ya walinzi wa usalama kutoka makundi ya kiraia au jeshi la akiba mgambo,
Pweinti!
 
Ili suala la ulinzi lifanikiwe
1. Nyumba kadhaa zitavamiwa
2. Balozi au kiongozi atalazimisha watu muamke kulinda.
3. Mkikataa analeta kikundi chake kilipwe (mara nyingi ni wezi na vibaka)
4. Usipolipa ndo unaibiwa Kila siku.

Mji wa Arusha umekuwa Mkubwa na Polisi hawatoshi.
 
Back
Top Bottom