sAFARI NJEMA ILA UJUE INAEMEKANA HAKUNA KIUMBE ALIYEWAHI KUFIKA MWEZINI
GONGA
HAPA NA
HAPA PIA
hAPA
UNAKWENDA NA CHOMBO GANI HUKO IKIWA WANAODAI KUWA WALIKWENDA HUKO MWAKA 1969, LEO WANADAI HAWANA TEKNOLOJIA YA KUWAPELEKA HUKO? KWA TAARIFA gonga
HAPA and
here
Lumbe nakushukuru kwa mapenzi yako kwangu.Umeeona mbali.Hawa jamaa huenda wamekusudia wakanitoe kafara huko mwezini,ndio maana nimepangiwa niwe wa mwanzo kushuka.
Lakini sikio la kufa halisikii dawa.Mimi safari ya mwezini bado ninaayoo!!.Nataka niwe wa mwanzo kufa huko.Isipokuwa sasa nitakuwa na tahadhari na hawa jamaa.Kwanza nitabaki kwenye space station kwa muda kuuchungulia mwezi.
Pale space station (ISI) si neno kwa sababu mara nyingi huwa tunakwenda.Sasa hivi wenzangu sita wako huko.Juzi rafiki yangu alikuwa anakwenda kuwapelekea matunda na maji,almanusra asababishe ajali kama ile ya Bp kule Lousiana.
BBC News - Russian cargo ship 'under control' official says
Ngoja nikuhadithie maisha yetu kule ISI:Moja ya matatizo tunayokumbana nayo ni kula,tunayo dining room lakini ni kama ada tu kwani sahani na vikombe wala havikai juu ya meza,huwa vinaelea.Kutokana na
weightlessnes chakula kama uji ukiumimina ili uutie mdomoni unaruka na kuenea mpaka kwenye dari.Tuna sehemu maalum ya kulala lakini ni kwa ajili ya kukaa pembeni tu inapokuwa huko kwenye zamu kwa sababu hakuna usiku.
Kwa vile space station imo kuizunguka dunia muda wote basi jua huchomoza kila baada ya dakika 90.Ndio maana tukilala tunakaa mbali na dirisha ili mwangaza wa jua usitukere.Kitanda kimoja tunaweza kulala wawili,mmoja juu na mwengine kwa chini uvunguni na wala hadondoki sakafuni.
Angalia huyu dada ambaye huja kutuamsha kila mara tukibadilishana zamu.
YouTube - Kawabata Makoto: Morning On The Moon