Uchaguzi 2020 Nawaonea huruma madiwani na wabunge waliopitishwa kwa tiketi ya CCM

Uchaguzi 2020 Nawaonea huruma madiwani na wabunge waliopitishwa kwa tiketi ya CCM

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2010
Posts
4,290
Reaction score
2,468
Ukweli mchungu ni kuwa shamrashamra zikishapungua, mwenyekiti wao bila kificho atawaambia kupitia umma kuwa sasa ni wakati wa kulipa fadhila. Haiingii akilini uwang'oe Mdee, Mbowe, Lema, Mbilinyi, Bulaya, Heche, Matiko, Msigwa na usilipe fadhili (price to pay).

Jiandaeni kisaikolojia. Jiandaeni kutumika kama pampas ndani ya chama chenu hicho hicho. Jiandaeni kufungwa midomo. Jiandaeni na utumwa huru.

Najua wengi nafsi hazina kicheko japo kinywani vipo. Dr. Tulia kasema mwenyewe hawakustahili. Sio kauli ya kubeza tu. Wameona uhalisia na sasa wanashangaa

Ni kama Yuda aliyetamani kuvitema vipande vya fedha ikashindikana kwa kuwa ilibidi maandiko yatimie, ila ole wake ambaye maandiko yametimia kwa njia ya yeye.
 
I can see how you are grieving..poleni sana ndio siasa hiyoo mchezo wasayansi na kushambuliana golini kwa zamu wakati wa kampeni jukwaa mliliteka ila sasa ni vilio na malalamishi.

Jipangeni uchaguzi ujao.

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
 
Upinzani watajua hawajui
Yaani wewe unavyopuyanga humu jukwaani mat.ako wazi kila mahali kuandika ujinga najaribu kupata picture umri wako ni kiasi gani nakosa jibu but nimehisi wewe ni bank teller amma NMB au crdb una mkopo wa ist unaona maisha umeyapatia ila ipo siku inakuja utatamani uje kufuta japo herufi moja ya unayoaandika humu ushindwe.

Kinachofanywa ndani ya Taifa hili siyo cha kufurahia unakuja msoto mmoja hujawahi ona na huu hauchagui huyu ni ccm huyu hana chama wote cha mtemakuni mtakiona!
 
Pamoja na ccm kushinda kwa 120% na chadema kutokuwepo bungeni utashangaa bado wabunge na wana ccm hawataacha kuitaja chadema kama inawakwamisha Arusha isiwe kalifonyaaa
Mbunge ataanza kwa kukipongeza chama chake kwa dakika mbili, halafu watatumia dakika 1 kumpongeza mbunge wa CUF kutoka Mtwara vijijini na chama chake kwa kuendesha kampeni za kiistarabu, dakika 4 kuwabeza Mbowe na Lissu na chama chao na dakika moja kuomba apelekewe maendeleo kwenye jimbo lake kama hali inaruhusu.

Amandla...
 
Mkuu wa kitengo cha Propaganda wa CCM hakika anastahili tuzo,,amejua kuwabaragaza,,bashiru aliposema tuna watu wa kila aina hamkujua ana maana gani,kibajaj alipowaambia bungeni safar hii ageni kbsa bungeni maana hamtarud hamkumuelewa ila leo ndo jib mnapata
 
Mkuu wa kitengo cha Propaganda wa CCM hakika anastahili tuzo,,amejua kuwabaragaza,,bashiru aliposema tuna watu wa kila aina hamkujua ana maana gani,kibajaj alipowaambia bungeni safar hii ageni kbsa bungeni maana hamtarud hamkumuelewa ila leo ndo jib mnapata
Sawa, Sema viumbe wa kila aina. Nimekuelewa. Maana hata shetani yupo miongoni mwenu
 
I can see how you are grieving..poleni sana ndio siasa hiyoo mchezo wasayansi na kushambuliana golini kwa zamu wakati wa kampeni jukwaa mliliteka ila sasa ni vilio na malalamishi.

Jipangeni uchaguzi ujao.

Congratulations in advance President Magufuli
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
Huwa ninasema kila siku akili ya muafrika the best it can do ni kuvukia barabara, not logical and rational thinking... Imagine mtu anashangilia kupangiwa mtu wa kumtawala, imagine licha ya kuona jirani yake, ndugu yake na Mtanzania mwenzake abadhulumiwa haki yake, ameumizwa na wengine kuuawa but yeye ndiyo kwanza anakenua meno kwa furaha. Na hapo wala hatarajii kupata chochote wakati wenzake waliyofanya hayo wanategemea malipo au fadhila....
 
Pamoja na ccm kushinda kwa 120% na chadema kutokuwepo bungeni utashangaa bado wabunge na wana ccm hawataacha kuitaja chadema kama inawakwamisha Arusha isiwe kalifonyaaa
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Tena hili nakuhakikishia ndiyo itakuwa salamu ya kila mbunge huko mjengoni..... Mhe Spika nakushukuru wewe binafsi kurudi tena bungeni, pia namshukuru Mhe namba 1 kwa kumuwezesha mimi kuingia bungeni na pia natoa shukrani zangu za dhati kwa kuhakikisha kwamba CHADEMA na ACT, wamefutwa rasmi bungeni, kwa sababu tokea tupate uhuru hawa wapinzani wamekuwa wakikwamisha mipango mingi ya maendeleo ya nchi....
 
Sometimes mtu unaweza kutumia nguvu nyingi kukamilisha uovu ulioupanga ila ukishakamilisha, unaweza kukaa chini na kuanza kujuta na kujiulaumu.
Nimemtafakari tena mwanadamu nakosa majibu sahihi
 
Back
Top Bottom