Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,659
Wakuu, napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wale wote walioomba msaada wangu niwasaidie baada ya kuona bandiko langu kwenye jukwaa hili wiki mbili zilizopita.
Nawashukuruni sana na ninapenda kuwaambia kuwa msaada wangu ni wa ukweli na si kuungaunga, Nimesoma vizuri kabisa masuala ya kodi. Nina shahada ya Uzamili ya kodi na CPA(T). Pia kwa sasa nafanya mitihani ili niwe "Chartered Tax Advisor" na baadaye nitamalizia na shahada ya uzamili ya Natural Resources Taxation.
Ninao uwezo mkubwa wa kodi na ni mwandishi mzuri sana wa defenses na tax planning. Na sheria kodi ya Ongezeko la thamani naijua vizuri sana. Hii sheria tuliyonayo sasa na pia mswada wa kuwa sheria mpya ya VAT 2014 pia niko vizuri.
Masuala ya kodi ya kimataifa nayafahamu (ndiyo nyumbani pao maana nimesoma hukohuko kwa wataalamu kuliko wote duniani katika masuala ya kodi).
Ninayo mambo mengi mazuri ya kuweza kuiletea kitu kizuri nchi hii na wananchi wake.
Kama una tatizo la kikodi iwe ni mahakamani ama unataka mkopo benki ama unataka kuthamanisha mali zako lakini kipengele cha kodi kinakutatiza usisite kuniona. Masuala ya kodi yanagharimu sana kupata ufumbuzi lakini mimi ni mtanzania ninayeangalia hilo. Gharama si kama zile unazotozwa na makampuni ya ushauri wa kodi.
Uwezo wangu mwingine mkubwa ni kwamba Mimi naweza kusimama na wakili yeyote maarufu wa nchi hii mahakamani na katika suala la kodi atachemsha tu labda suala hilo la kodi niwe sijaanza nalo mimi toka mwanzo.
Karibuni sana na asanteni kwa kunisikiliza.
Nawashukuruni sana na ninapenda kuwaambia kuwa msaada wangu ni wa ukweli na si kuungaunga, Nimesoma vizuri kabisa masuala ya kodi. Nina shahada ya Uzamili ya kodi na CPA(T). Pia kwa sasa nafanya mitihani ili niwe "Chartered Tax Advisor" na baadaye nitamalizia na shahada ya uzamili ya Natural Resources Taxation.
Ninao uwezo mkubwa wa kodi na ni mwandishi mzuri sana wa defenses na tax planning. Na sheria kodi ya Ongezeko la thamani naijua vizuri sana. Hii sheria tuliyonayo sasa na pia mswada wa kuwa sheria mpya ya VAT 2014 pia niko vizuri.
Masuala ya kodi ya kimataifa nayafahamu (ndiyo nyumbani pao maana nimesoma hukohuko kwa wataalamu kuliko wote duniani katika masuala ya kodi).
Ninayo mambo mengi mazuri ya kuweza kuiletea kitu kizuri nchi hii na wananchi wake.
Kama una tatizo la kikodi iwe ni mahakamani ama unataka mkopo benki ama unataka kuthamanisha mali zako lakini kipengele cha kodi kinakutatiza usisite kuniona. Masuala ya kodi yanagharimu sana kupata ufumbuzi lakini mimi ni mtanzania ninayeangalia hilo. Gharama si kama zile unazotozwa na makampuni ya ushauri wa kodi.
Uwezo wangu mwingine mkubwa ni kwamba Mimi naweza kusimama na wakili yeyote maarufu wa nchi hii mahakamani na katika suala la kodi atachemsha tu labda suala hilo la kodi niwe sijaanza nalo mimi toka mwanzo.
Karibuni sana na asanteni kwa kunisikiliza.