Obuntu
JF-Expert Member
- Feb 6, 2008
- 510
- 34
Napenda nichukue nafasi hii kuwatakia Sikukuu njema wafanyakazi wote wa majumbani. Pia natumia fursa hii kuwashukuru kwa kazi kubwa wanazofanya majumba, kwa maana bila wao familia zetu nyingi zingekuwa mashakani.
Najua siku ya kesho mtakuwa na kazi nyingi sana hasa hasa zinazohusiana na kupika na usafi wa nyumba kwa ujumla. Jaribu kutumia wakati huo kuongea na ma-boss wenu kama kuna kitu kinawatatiza maana ma-boss wote kesho watakuwa nyumbani na watakuwa wanafuraha sana, ukizingatia pia mapochi yao yatakuwa na maela ya kutosha.
Pia nawaombeni ma-boss kuwanunulia zawadi hawa wasaidizi wetu maana wao ndiyo wanaijua vizuri nyumba kuliko hata sisi! Wapeni shukrani kwa kuwalelea watoto na usaidizi mwingineo.
Asanteni Sana na Mungu awabariki..
Najua siku ya kesho mtakuwa na kazi nyingi sana hasa hasa zinazohusiana na kupika na usafi wa nyumba kwa ujumla. Jaribu kutumia wakati huo kuongea na ma-boss wenu kama kuna kitu kinawatatiza maana ma-boss wote kesho watakuwa nyumbani na watakuwa wanafuraha sana, ukizingatia pia mapochi yao yatakuwa na maela ya kutosha.
Pia nawaombeni ma-boss kuwanunulia zawadi hawa wasaidizi wetu maana wao ndiyo wanaijua vizuri nyumba kuliko hata sisi! Wapeni shukrani kwa kuwalelea watoto na usaidizi mwingineo.
Asanteni Sana na Mungu awabariki..