Nawatetea Tigo kuhusu 'Jaza Ujazwe'

DCI Comrade One

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2012
Posts
557
Reaction score
718
Wakuu Naomba niwatetee kampuni ya tiGO.

Leo hii Watanzania wanapiga kelele kuhusu "Jaza ujazwe". Lakini Watanzania wamesahau kuwa uchokozi waliuanzisha wenyewe.

Uchokozi huo waliuanzisha kwa kuharibu maana ya "tiGO". Sina haja ya kufafanua, ila kila Mtanzania anajua neno "tiGO" linatumikaje huku mtaani.

Ila ukigoogle maana ya tiGO kwa lugha ya huko kampuni ilikotokea maana yake ni "Wewe". Bila shaka walilenga kumaanisha tiGO ni kampuni inayokujali wewe.

Na wacha Mungu wanaotumia Kiingereza wakaichakachua "TIGO" kuwa ni "Trust In God Only". Ambayo imekaa vizuri.

Ila sie Waswahili bwana .... sijui akili zetu zikoje mpaka tukaipa "tiGO" ile maana yetu ileeeeee!

Sasa tiGO nao wametuletea Uswahili tunaanza kulialia.

Acheni longolongo bwana.
 
Hongera kwa "KUJAZWA" mkuu baada ya kuwa "tigolized".
 
Watanzania wanapenda kushupalia vitu vepesi-vepesi.

Aliyebuni hili tangazo anapewa promo ya bure mpaka bungeni, pesa inaingia tu na makampuni kinzani yamefungwa yameshindwa kucopy kwasababu watajikuta wao ndiyo wameishia kutukana.
 
hahahaha promotion hiii
 
Jaza ujazwe kwa mpigo? hakika TiGO wamedhamiria kuwaridhisha wateja wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…