Naweza kusoma nini na chuo kipi kwa division four point 33

Nenda uganda ukazuge kama mwaka mmoja hivi, kuna vijana wa mjini pale kampala wanatengeneza vyeti vya makerere na wanakusaidia kuingiza jina lako kwenye database ya chuo, ni pesa yako tu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
hahahaha...endelea kusoma status za watu facebook ndo size yako kwa kuwa hata kuchunga ng'ombe huruhusiwi kwa sifa hizo
si mlikuwa mnacheza shuleni badala ya kusoma mnanyoa viduku,mnavaa mlegezo, mnashinda facebook
 
Pole sana mdogo pia hongera kuonyesha nia ya kutaka kuendelea na masomo.Kufeli mtihani wa NECTA sio kufeli maisha,kufanikiwa kimaisha sio lazima uwe na cheti safi kwani kuna njia nyingine nzuri tu zitakuwezesha kufika mbali kimaisha,mfano pata elimu ya ujasiriamali ambayo haitaji kuwa na cheti kizuri tu,baada ya hapo unaweza kujiajiri mwenyewe na kufika mbali kuliko hata waliopata div I-III,achana na wanaokuponda
 
hapa sio sehemu sahii pa kukusaidia kwa matatizo yako,maana wengi wanakuvunja moyo!usikate tamaa rudia tu mtihani mwakani utafahulu kama ukiweka nia.


kawia ufike
 
Mkuu kwa hiyo pass mark yako labda UDOM tu ndio patakufaa, mi sisemi mengi.
 
facebook facebuk fathebuk facebuki fesibook phesibook phesibuk faceboooook!!!!!!! : like
 
Na mimi nina ndugu yangu naye amepata ya 33,nikashauriwa labda arudie form 3 kwa private school,naombeni msaada nianzie wapi na ni shule gani zilizopo arusha,kilimanjaro,tanga na dar.
Msaada tafadhali

Hakuna wasiwasi mpeleke shule moja inaitwa St.Joseph iko maeneo ya ngarenalo kama zimo lazima afaulu.
 
Nimesoma komenti zote hapa me nasema kua umeshapewa za uso,jipange upya urudie,chuo utapata badae,tafuta Credit kwanza
 
ushauri Nenda SAINT JOHN'S UNIVERSITY OF TANZANIA kipo DODOMA utasoma cheti PROCUREMENT and SUPPLY
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…