Nbc mnanihukumu kwa makosa yenu wenyewe

Nbc mnanihukumu kwa makosa yenu wenyewe

ngomicom

Senior Member
Joined
Jul 6, 2012
Posts
123
Reaction score
19
Wapendwa wana JF: Naamini nyote mnakumbuka utaratibu n amatangazo ya kuboresha taarifa za kibenki kwa wale wenye akaunti zao. Naomba kuwakumbusha tangazo la NBC, pamoja na maelezo mengine benki hii ilieleza kuwa wanaostahili kuboresha taarifa ni wale ambao waliofungua akaunti kabla ya Julai 2007.

Mimi ni mmoja wa wateja wa benki taja na nilifungua akaunti October 2007 katika tawi la Industrial area,
Cha ajabu tangu mwezi uliopita benki inagoma kunipatia huduma kwani kila niendapo ATM mashine naambiwa "No transaction permitted", baada ya kuingia kaunta kwa wahudumu wamenijulisha kuwa sikuboresha taarifa za kibenki na kwakuwa nilifungua tawi nikiwa shule nikafungua kama mwanachuo, inanipasa kwasasa kuboresha taarifa eti anuani zangu za sasa ni tofauti. Maswali ya kujiuliza ni mengi, mfano;
  • Mimi mteja wao ninakosa gani?
  • Kwanini tangazo lao halikueleza wanaotakiwa kuboresha kwa makundi yao?
  • Ninani atakaye lipa gharama hizi na usumbufu ninaoupata kwasasa?
  • kwanini kitengo chao cha mahusiano na jamii kisiwajibishwe kwa kuninyanyasa mtanzania
hukumu hii ninayopewa si halali yangu maana makosa na yao NBC
 
Pole sana just do what they need ,life goes on ,ni agizo toka bot
 
Lawama nyingi hazisaidi sana. Nina imani kabla ya hiyo message unayopata kwenye ATM ulishataarifiwa kuwa uboreshe akaunti yako hasa kama ulikuwa unatumia huduma za ndani ya benki. Mimi nafahamu kuwa walengwa wakuu walikuwa wale waliofungua akaunti 2007 kurudi nyuma. Lakini katika matangazo mengi ya BOT pamoja na commercial banks hayakubagua wateja, kila mmoja alipaswa kuboresha akaunti yake. Mimi nimefungua akaunti NBC 2011 na bado niliupdate details zangu sembuse wewe wa 2007. Nenda benki kapeleke documents wanazohitaji, itakusaidia sana kupata huduma za kibenki mapema kuliko kuja Jf kulalamika.
 
Back
Top Bottom