NBC: This is not fair!

Exim, Barclays and Stanbic. Atleast mnajitahidi.

Hawa wahindi sijui ndo afadhari wangekuwa wanamatawi mengi TZ wange komba wateja wote maana card ile unatumia tu kwa kuchukulia kwenye ATM ukienda kwa teller huna haja ya kuonyesha card wewe unachukua tu mpunga.
 
for that case benki zote zilizo angalau na matawi hata mikoani ziko hivyo, I mean NBC, CRDB na NMB. sasa ukifunga ya NBC where do you go?

Damn!!!!!!!!!
It looks to me that the only alternative remaining is to make use of M-Pesa as so far it have been very OK with me.

Pole sana though.
 
Zamani niliifunga account yangu Benki ya Posta kwa sababu ukitaka kuweka au kuchukua pesa yako kule uombe ED kabisa kazini, maana siku nzima itapotea kwa kwenda kuweka au kuchukua 10,000/= Tena mahali pengine hata kama balance yako ni milioni 10 watakwambia mwisho kuchukua ni 10,000/= ati hawana hela ya kutosha. Nikaishiana nao kwa kuniudhi walipokaa na kitabu changu miezi 8 eti wanapiga hesabu ya faida waniingizie kwenye kitabu. Nilipofuatilia nikakuta mtu mmoja makao yao makuu kakiweka kitabu changu kwenye draw yake akidai bado anakifanyia kazin(Baada ya miezi 8).

Nikaona NBC bora. Lakini nao wakaaza kuboa taratibu na hatimaye mb** wao ni mkukwa zaidi. unaenda na kadi yako counter yenye picha yako kabisa na saini kwa nyuma. Kwyenye system wanaiona balance yako. Wanakusainisha nyuma na mbele kwenye karatasi zao za kuchukulia pesa, lakini bado wanataka upitie ATM kuuliza salio ambako wanakata 75/=, Ukikosea ukarudia tena unakatwa tena. Ukichukua pesa wanakata 500/= ukichukuwa mara mbili kukamilisha 600,000/= wanakata 1000/= wanakuuliza unataka huduma nyingine? ukikubali ukasema labda niulize swali wanakata. Hawaweki faida (Interest) kwenye pesa yako, kila mwisho wa mwezi wanakata tena ati ni ledger maintenance fee. Wizi---wizi---wizi!

Halafu counter zaweza kuwapo 6, lakini utakuta kuna mhudumu 1 au wawili tu, quee ni ndeeeeefu lakini hawajali, unakuta wanapiga story ndani na wengine wanajipitishapitisha wakikata viuno kwenye vyumba kutoka chumba kimoja hadi kingine, halafu wanaingia kwa vyumba vya wahudumu walioko counter na kuanza kuwasemesha story na kupeleka kazi za ndugu zao za kuwawekea na au kuwachukulia pesa ati hawawezi kupanga mstari. Sasa NBC wanataka kufanana na Benki ya Posta.

NMB nao ndio SACCOS hasa! Wao wanakata viuno kwenye makorido wakijipitishapitisha wakati wateja wamejaa hata wanashindwa kupumua bali wanapumuliana. Kama una wivu na mkeo na umekwenda naye utakufa kihoro kwa namna wanavyombana kwenye msitari. Hata konokono anayo speed kubwa wanavyofanya kazi. ATM wameanza kuweka na hawakati pesa, lakini zinaweza kuwapo 2 ukakuta ama mbovu zote au moja tu inafanya kazi, watu hujaa mno, maana chini ya laki tano ati lazima uende ATM. Halafu Kadi zao kumbe zinaexpire bwana. yaani weacha tu.

Sio hapo tu lakini, ukienda Muhimbili hospitali kwa mfano, ati wanataka mambo mapya ya kisasa, computerised services kila kitu. Nguvu ya savor ni kaduchu na wao wanataka mambo makubwa. Mteja mmoja kumwandikisha alipe akamwone daktari ni nusu saa au zaidi, wanadai mtandao uko slow leo. Unaweza kuamua kupona hapohapo kabla ya kumwona huyo daktari wao. Hata akikuona daktari, anakwambia kalipie vitu hivyo.... unakwenda kukaa tena kwenye mstari weeeeee! Kwa nini tunaanza system ambazo hatuziwezi?

Na nyie BoT mko wapi wezi wa mabenki wanatamba tu nanyi mmelala? Au nako tupeleke EWURA?
 
Bora ungeenda na hiyo statement ukapewa pesa!! uliza kinachfuata baada ya kwenda na hiyo statement kama hapo benki hufahamiki......

Ha ha haaa! Yashawahi kunikuta haya nikasubiri kwa two hours wanasubiri fax kutoka mlimani Branchi, nikawasemea Mbovu sana ikabidi wanipe tu maana nilitishia kufunga account yangu siku hiyo hiyo
 
Pumb* zao hela yako na wakunyanyase wao kwenda zao
 
Kerooooooooooo
Mimi sometimes najiuliza hivi watanzania wanaofanya kazi benki, haswa hawa ma bank teller wamesoma wapi?? Kila siku nikipanga kwenda benki najiandaa kabisa kuudhiwa. I have never been at ease with these guys.

NBC ndiyo benki inayo kera kuliko zote kwani makosa wanayaona na hawataki kujirekebisha. NMB is a big plus. Ni benki ya makabwela and it is struggling to survive. NBC wee acha tu....Hilo la tellers zisizo na wahudumu ndiyo zao. Maswali ya kuudhi ndiyo usiseme. Kuhitaji ukae masaa matano wakituma Fax tawi lako ndiyo business model yao. Keeero!!

Sina uhakika kama naweza kumshauri mtu afungue account NBC. No way. Afadhali benki nyingine ZOOOTE kwani wana songa mble. There are improvements in almost every area. NBC ni kurudi nyuma. Mshahara wangu suingekuwa unapitia hii benki, ningesha hama siku nyingi. As for now, najiandaa kuudhiwa every time I go there. I force myself to be cheerful na kujidai hamnazo. I carry a lot of newspapers and/or a book kila wanachosema nakubali and then natoa all the money I need for a t least a month. Mchwiiiiiiiiii
 

benki za tanzania huduma zao mbovu.
Mimi nilikwenda tawi la kariakoo nmb kutaka kufungua akaunti wakanisumbua na urasimu kibao nikaacha kufungua nikaenda barclays ikawa rahisi bila urasimu kosa la barclays wanakata ela balaa! Mara service charge mara gharama ya kuendesha akaunti ,na ukichukua ela kwenye atm mara 3 kwa siku kosa wanakata maela kibao!
Halafu ajabu nyingine mabenki yote huduma ya safe keeping draft hawana ,hii ingekuwa rahisi kwa wafanyabiashara ku export gold, diamond na tanzanite kwa urahisi bila ya mnunuzi kutoka nje ya nchi kuja tanzania au muuzaji kusafiri nje ya tanzania , na serikali ingepata mapato mengi kwa njia ya kodi sababu biashara ingefanyika kwa haraka bila urasimu.
 
Ninafikiri NBC wana mgomo wa ndani kwa ndani huduma zao ni mbovu nchi nzima kwa nini?Mtu anaweza kuwa anadepost elfu kumi tu lakini atakaa kwa teller nusu saa.Watu mnasimama kwenye foleni miguu inataka kurudi ndani.Inadibi wajirekebishe
 
Mimi niliambiwa na Teller signature hai-Match! Watatafuta japo ka-sababu kadogo sana wakukwamishe! Nikaenda kwa manager wa tawi I got the money but I was pissed off! They treat their customers in a very suspicious and hostile way!
 
Hayo yote tisa, wanajitahidi kuweka ATM kibao barabarani lakini je ni ngapi zinafanya kazi? Kipi bora kuwa Na ATM kibao mbovu au chache nzima? Customer care mbooovu, ukiwa na shida ya statement ndo balaa zaidi we acha tu!
Hata hivyo wana nafuu kuliko benk nyingine za makabwela
Nafikiri uongozi mbovu ndo maana kuna kasoro hizo
 


Hizo tabia zao za kustorishana wakati limstari haliendi SIIPENDI.......yaani siipendi ile mbaya. Hawa watu hawatujali kabisa.....mara kapokea simu, mara mtu kaingia ndani anamsemesha au anamuingizia transaction zake, mara katoka sijui keshi imeisha, halafu hakwambii chochote anakuangalia kama vile uko pale kuomba msaada..........yaani wananiboa wananiboa ilembaya. Tena ukienda hizo tarehe za mshahara hizo.......pls nenda na oksijeni yako....vinginevyo utasafoketi live.

ukikuta ATM moja nzima hilo limstari lilivyorefu utadhani wamepanga foleni ya kupokea mchele wa bure kwa bakhresa siku ya sikukuu huwezi kukaa. Tena mikoani ndio worse. Pesa zako mwenyewe lakini mpaka uzipate.......ni kwa mateso makubwa sana.

BOT naona wanawasubiri majembe ili waanze kazi walizoamini na serikali kusimamia haya mabenki.
 
Out of the topic fastladi: Ni kweli kabisa nimeona kitabu chenye sura yako. maudhui yake unaweza usiyapende. Nimekiona leo pale posta mpya ukivuka jengo la wizara ya kilimo barabara gani ile sijui azikiwe? karibu na duka matata la viwalo.Au nimechelewa kukiona
 
Nadhani kuna gap kubwa sana kwa upande wa regulator ( BoT) especially katika kuchukua maoni ya sisi wateja wa mabenki maana ni shida sana we acha hao NBC kuna kibenki kidogo cha wahind hao ni wezi kwenye ATMs
BoT lazima waweke standards na sheria kali za kutulinda wateja pia
 

Kama uko dar, na unahitaji huduma kwa dar mara nying, fungua Stanbic au Twiga Bancorp, nimekuwa nao mda mrefu, they never failed me. NBC is worse!
 

Yalinikuta mimi jana tu, niliienda Sea Cliff branch kuchukua Sh 700,000? nimpe jamaa chapchap nirudi ofisini...eeebwana eeee....niliambiwa ATM mwisho 600,000 zaidi ya hapo wafax details zangu nilikofungulia account, wakipta jibu ndo wanipe hiyo 100,000! Nilichukia! acha aisee....wale jamaa hawafanya biashara wanatoa misaada nadhani...au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…