NBS waache kutumia jina la Rais kuhamasisha sensa. Wao pia wanajitosheleza!

NBS waache kutumia jina la Rais kuhamasisha sensa. Wao pia wanajitosheleza!

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Sijafurahishwa kabisa na huu ubunifu wa watu wa takwimu kutumia jina la Rais na viongozi wengine kuhamasisha sensa.

Mama Ana Makinda ni mtu mashuhuri, angeweza kutumia hata jina lake au maafisa wengine! Kutumia jina la Rais naona kama haijakaa sawa!
Kama iko sawa toa hoja, haya si malumbano ni mtazamo tu!

Screenshot_20220828-181748.jpg
 
Naamini ukibaki msomaji wa kawaida kama mimi hupungukiwi na kitu ,ona sasa tutataka kujua uwezo wako wa kufikiri na kiwango chako Cha Elimu.

Naomba nikujibu kwa uelewa wa wengi na utaniambia kama hujaridhika.

Kwanza tambua sensa ni Rais na Rais ni sensa, zoezi hili toka mwanzo msimamizi Mkuu ni Rais kwa Sababu taarifa za maswali ya sensa yatamsaidia Rais kutekeleza majukumu yake ipasavyo na ni Rais ndio anatakiwa kuwataka, kuwaomba na kuwasihi watu washiriki zoezi Hilo.

Hapo aangaliwi mtu maarufu kwa Sababu hata kingwendu ni maarufu kuliko Anna Makinda ,hapo kinachoangaliwa ni nani mwenye uhitaji wa taarifa za sensa kati ya Anna Makinda na Rais Samia?. Jibu ni Rais Samia, kama ndivyo basi ni yeye ndio kuwaomba watu taarifa hizo.

Mtazamo wangu
Yawezekana mtazamo wangu usiwe sahihi lakini una ukweli ndani yake, zoezi hili Upinzani wanaona kama ni moja ya siasa za CCM. Mtanzamo huo unafanya wapinzani wengi washindwe kushiriki zoezi hili muhimu kwa kujua au kutokujua.

Uhalisia
Uhalisia wa zoezi hili ni kwamba sensa ni mkakati wa maendeleo kwa watu hivyo Rais kuwa mstari wa mbele kukuhamasisha ni kwa nafasi aliyonayo katika maendeleo ya nchi yetu. Rais Kama mdau namba moja wa maendeleo ni lazima aone umuhimu wa kila mtu kushiriki
 
"NBS hakuna atakaewasikiliza, tena watu wataanza kunon'gona kuwa hii Kampuni ya Mabasi ya Tabora inawasumbulia nini..."
 
RAIS Samia , yeye mwenyewe tu Hana Ushawishi .

Yaan mikutanoni mwake watu wanaenda kumuona 'Rais '.


Wakati wa Rais Magufuli, Watu walienda kumuona 'Magufuli Rais wa TZ".


So far zoezi limebumaaaaa Licha ya mabilioni 600+
 
Sijafurahishwa kabisa na huu ubunifu wa watu wa takwimu kutumia jina la Rais na viongozi wengine kuhamasisha sensa.

Mama Ana Makinda ni mtu mashuhuri, angeweza kutumia hata jina lake au maafisa wengine! Kutumia jina la Rais haijakaa sawa!

View attachment 2337621
Sensa ya nchi yeyote ni mali ya RAIS wa nchi husika kama ilivyo bajeti ya nchi. NBS ni technical Experts tu wa Sensa. Refer to the Statistical Act!!!! Una swali lingine?
 
Naamini ukibaki msomaji wa kawaida kama mimi hupungukiwi na kitu ,ona sasa tutataka kujua uwezo wako wa kufikiri na kiwango chako Cha Elimu.

Naomba nikujibu kwa uelewa wa wengi na utaniambia kama hujaridhika.

Kwanza tambua sensa ni Rais na Rais ni sensa, zoezi hili toka mwanzo msimamizi Mkuu ni Rais kwa Sababu taarifa za maswali ya sensa yatamsaidia Rais kutekeleza majukumu yake ipasavyo na ni Rais ndio anatakiwa kuwataka, kuwaomba na kuwasihi watu washiriki zoezi Hilo.

Hapo aangaliwi mtu maarufu kwa Sababu hata kingwendu ni maarufu kuliko Anna Makinda ,hapo kinachoangaliwa ni nani mwenye uhitaji wa taarifa za sensa kati ya Anna Makinda na Rais Samia?. Jibu ni Rais Samia, kama ndivyo basi ni yeye ndio kuwaomba watu taarifa hizo.

Mtazamo wangu
Yawezekana mtazamo wangu usiwe sahihi lakini una ukweli ndani yake, zoezi hili Upinzani wanaona kama ni moja ya siasa za CCM. Mtanzamo huo unafanya wapinzani wengi washindwe kushiriki zoezi hili muhimu kwa kujua au kutokujua.

Uhalisia
Uhalisia wa zoezi hili ni kwamba sensa ni mkakati wa maendeleo kwa watu hivyo Rais kuwa mstari wa mbele kukuhamasisha ni kwa nafasi aliyonayo katika maendeleo ya nchi yetu. Rais Kama mdau namba moja wa maendeleo ni lazima aone umuhimu wa kila mtu kushiriki
Huyu mama Lanlady anaboa sasa. Kila siku ni kuleta haya mambo yasiyo na miguu wala mikono. Mwambie Sensa ni part of the Tanzania Population Policy. Hivyo coordinator wake (Enzi hizo ilikuwa ni Planning Commission) sasa ni Ofisi ya Waziri Mkuu. Ndiyo maana Maratibu ni Waziri Mkuu. Huyu mama haelewi kitu badala ya kuuliza anaanzisha hoja. NBS wantoa utaalam tu katika maseuala ya sensa. Sensa ni mali ya Mkuu wa nchi
 
Mtoa mada yuko sahihi. Wengine mnaotetea upuuzi huu hamna akili. Utaratibu wa sensa upo kila baada ya miaka 10, siyo hisani, ubunifu au fadhila za Rais wa wakati huo. Acheni ujinga.

Haya mambo ya kumpa kila sifa Rais kama mitaji myepesi ya kisiasa yamewalemaza Watanzania halafu tunashangaa kwa nini tupo hapa na tunashindwa kutoka tulipo.
 
Kilichokukasirisha nini wakati wenye majina yao wameafiki yatumiwe? We ungesema hata unakasirishwa na makarani wa sensa wanaohesabu watu nusunusu na kuondoka kwa ahadi watarudi kesho na hawarudi so kusababisha serikali kutofikia malengo yake ningekuelewa.
 
Sensa ya nchi yeyote ni mali ya RAIS wa nchi husika kama ilivyo bajeti ya nchi. NBS ni technical Experts tu wa Sensa. Refer to the Statistical Act!!!! Una swali lingine?
Kwani sensa hii ndiyo ya kwanza kwenye hii nchi?

Kwahiyo kwa kutumia jina la rais ndio watu watahamasika zaidi?

Hayo ni matumizi mabaya ya fedha za umma hata kama hazijatoka moja kwa moja mfukoni kwa kila mwananchi.

Hapo kuna fungu limewekwa kwa kutuma hizo msg za kuhamasisha. Ilihali tayari wananchi wana taarifa za kutoka vyanzo vingine!
Huyu mama Lanlady anaboa sasa. Kila siku ni kuleta haya mambo yasiyo na miguu wala mikono. Mwambie Sensa ni part of the Tanzania Population Policy. Hivyo coordinator wake (Enzi hizo ilikuwa ni Planning Commission) sasa ni Ofisi ya Waziri Mkuu. Ndiyo maana Maratibu ni Waziri Mkuu. Huyu mama haelewi kitu badala ya kuuliza anaanzisha hoja. NBS wantoa utaalam tu katika maseuala ya sensa. Sensa ni mali ya Mkuu wa nchi
Ukiuchukia ukweli ni vigumu kukubaliana na wanaouzungumza.

Hii sensa imekuwa na mbwembwe nyingi na wakati hali za maisha ni ngumu. Bidhaa bei ghali. Wanshindwa kutengeneza mifumo mizuri ya ukusanyaji kodi, wanakata watu tozo kila mahali ili kutuma tuma ujumbe wa sensa!
Kama ulivyokuwa bored na threads za Lanlady , ndivyo nami pia nimekuwa bored na hizo msg za sensa!
 
Naamini ukibaki msomaji wa kawaida kama mimi hupungukiwi na kitu ,ona sasa tutataka kujua uwezo wako wa kufikiri na kiwango chako Cha Elimu.

Naomba nikujibu kwa uelewa wa wengi na utaniambia kama hujaridhika.

Kwanza tambua sensa ni Rais na Rais ni sensa, zoezi hili toka mwanzo msimamizi Mkuu ni Rais kwa Sababu taarifa za maswali ya sensa yatamsaidia Rais kutekeleza majukumu yake ipasavyo na ni Rais ndio anatakiwa kuwataka, kuwaomba na kuwasihi watu washiriki zoezi Hilo
kwa matazamo wako huo, nachelea kusema unahitaji elimu zaidi ya masuala ya kisiasa na kijamii. Sensa sio siasa. Haihitaji mbwembwe nyingi!

Kama angeweza kufanya hayo yote kulikuwa na haja gani ya kuwepo na tume inayoshughulikia masuala ya sensa?
Lakini pia kumbuka hakuna aliyekataa kuwepo kwa hamasa, swali ni kwanini waendelee kutumia jina la rais kwa kutuma msg iihali tayari alishazungumza kupitia vyombo vya habari, vipeperushi, mabango nk?


Na ndio maana (kwa mujibu wa malalamiko ya baadhi ya wahanga) hadi tume nyingine (tume ya uchaguzi) huamuliwa namna ya kufanya kwa sababu tu iko chini ya rais!

Na ujue tu kwamba kwenye nchi hii hakuna kisochokuwa chini ya rais!
Maamuzi yote (hata kama yataamuriwa na watu wengine) lazima yaendane na matakwa yake!

#Kodi na tozo zaidi ya mara moja kwa kipato hicho hicho, ni wizi!
 
Back
Top Bottom