Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 593
- 1,376
"Lengo la ziara yetu ni kutazama tena, kuhuisha mwamko ndani ya chama chetu na ndio maana kazi ya kwanza tumefanya katika eneo hili (Mpanda/Katavi) ni kwenda kwenye shina namba tano (5) ili tukajiridhishe ni kweli wanafanya vikao? Ni kweli wanaandika mihtasari ya vikao vyao?
"Nataka niseme kwa uhakika kabisa kwamba tumeshuhudia kwamba ni kweli wanafanya na tumefurahi sana, msingi wa chama chetu ni mashina, na unakuwa msingi kwa sababu ndio kituo cha kwanza cha kuandaa na kulea wanachama wa chama cha Mapinduzi (CCM).
"Chama cha Mapinduzi (CCM) kina mashina laki 2 na elfu 46 na kila shina likiwa na viongozi watano (5), Mwenyekiti wa shina na wajumbe wake, lengo letu sasa ni kujuwa je kila shina kinafanya kazi sawasawa, kila tawi lunafanya kazi sawasawa, kila kata inafanya kazi sawasawa, maana mnaweza kuiongoza serikali vizuri kama ninyi wenyewe mnafanya kazi zenu vizuri, hatuwezi kuwa na ujasiri wa kuikosoa serikali tunayoiongoza au serikali za mitaa tunazoziongoza kama sisi wenyewe tuna mapengo kila kona hatutimizi wajibu wetu, ndio maana tumechukua hatua ya kijitazama kwanza sisi wenyewe kama kweli tunatimiza wetu halafu tuwe sasa na ujasiri wa kuikosoa serikali".
Dkt. Nchimbi amezungumza hayo wakati alipokutana na viongozi wa ngazi mbalimbali wa CCM mkoani Katavi jana, Jumamosi Aprili 13.2024.
"Nataka niseme kwa uhakika kabisa kwamba tumeshuhudia kwamba ni kweli wanafanya na tumefurahi sana, msingi wa chama chetu ni mashina, na unakuwa msingi kwa sababu ndio kituo cha kwanza cha kuandaa na kulea wanachama wa chama cha Mapinduzi (CCM).
"Chama cha Mapinduzi (CCM) kina mashina laki 2 na elfu 46 na kila shina likiwa na viongozi watano (5), Mwenyekiti wa shina na wajumbe wake, lengo letu sasa ni kujuwa je kila shina kinafanya kazi sawasawa, kila tawi lunafanya kazi sawasawa, kila kata inafanya kazi sawasawa, maana mnaweza kuiongoza serikali vizuri kama ninyi wenyewe mnafanya kazi zenu vizuri, hatuwezi kuwa na ujasiri wa kuikosoa serikali tunayoiongoza au serikali za mitaa tunazoziongoza kama sisi wenyewe tuna mapengo kila kona hatutimizi wajibu wetu, ndio maana tumechukua hatua ya kijitazama kwanza sisi wenyewe kama kweli tunatimiza wetu halafu tuwe sasa na ujasiri wa kuikosoa serikali".
Dkt. Nchimbi amezungumza hayo wakati alipokutana na viongozi wa ngazi mbalimbali wa CCM mkoani Katavi jana, Jumamosi Aprili 13.2024.