KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 8,589
- 16,936
Watu saba wamejeruhiwa nchini Korea Kusini, wanne kati yao vibaya, baada ya ndege ya kivita kudondosha mabomu manane kwa bahati mbaya katika eneo la makazi ya raia wakati wa mazoezi ya kijeshi.
Tukio hilo lililohusisha ndege ya Jeshi la Anga ya KF-16 lilitokea katika jiji la Pocheon, karibu na mpaka na Korea Kaskazini.
Ni bomu moja pekee ndilo linaloaminika kulipuka.
Kikosi cha kutegua mabomu kinafanya kazi ya kuondoa kwa usalama mabomu mengine saba ambayo hayajalipuka.
Serikali ya Pocheon imeiambia BBC wakazi wanaoishi karibu na eneo hilo wamehamishwa.
Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya ndani, watu wawili walipata majeraha ya shingo na mabega.
Jeshi la anga la Korea Kusini limesema linachunguza tukio hilo na kuomba radhi kwa uharibifu huo na kuongeza kuwa itatoa fidia kwa walioathirika.
Jengo moja la kanisa na nyumba pia ziliharibiwa kutokana na tukio hilo. Picha zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari vya ndani zinaonyesha dirisha lililovunjika la jengo na paa la kanisa lililoharibika.
Wizara ya ulinzi imesema mafunzo hayo ya Alhamisi yalihusisha mazoezi ya pamoja na vikosi vya Marekani.
Tukio hilo lililohusisha ndege ya Jeshi la Anga ya KF-16 lilitokea katika jiji la Pocheon, karibu na mpaka na Korea Kaskazini.
Ni bomu moja pekee ndilo linaloaminika kulipuka.
Kikosi cha kutegua mabomu kinafanya kazi ya kuondoa kwa usalama mabomu mengine saba ambayo hayajalipuka.
Serikali ya Pocheon imeiambia BBC wakazi wanaoishi karibu na eneo hilo wamehamishwa.
Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya ndani, watu wawili walipata majeraha ya shingo na mabega.
Jeshi la anga la Korea Kusini limesema linachunguza tukio hilo na kuomba radhi kwa uharibifu huo na kuongeza kuwa itatoa fidia kwa walioathirika.
Jengo moja la kanisa na nyumba pia ziliharibiwa kutokana na tukio hilo. Picha zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari vya ndani zinaonyesha dirisha lililovunjika la jengo na paa la kanisa lililoharibika.
Wizara ya ulinzi imesema mafunzo hayo ya Alhamisi yalihusisha mazoezi ya pamoja na vikosi vya Marekani.