Elections 2010 Ndg. Jamal Abdallah TAMIMU wa Muhambwe: Elimu Darasa la Saba. Ni Rushwa?

Mwanaukweli

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2007
Posts
4,786
Reaction score
1,715
Huyu sijui TAKUKURU wamemkosaje? Alikuwa anatoa rushwa waziwazi.

Shughuli zake hazieleweki vizuri na kuna malalamiko mengi dhidi yake toka kwa wananchi juu ya Ujambazi.

Hivi Millenium hii ya pili bado viongozi wasio na Elimu wala maadili wana nafasi???

CCM safisheni aibu kama hizi!! Wapiga kura tunaona na tutaamua
 
Kwa kigezo cha Elimu nimeona wapo wengi wenye Elimu ya msingi akiwemo LAMECK wa ROrya tena kuna wadau wanasema jamaa aliishia la 4 tu akiingia kwenye mishe mishe zake!! ccm imechafuka haswa hakuna msafi ndani ndo mana wameamua kufunika kombe.....
 
Kwenye elimu yupo pia Jah People kule Njombe na yeye siku zote amekuwa akijisifu ni darasa la saba tena lile la juu. Lakini kwenye Ujambazi nadhani unahitajika uthibitisho ni tuhuma nzito saana hizo!
 
KWA WALIOPO CHADEMA..........MUULIZENI WAZIRI WA ZAMANI ALIYESHINDWA NA HUYU BWANA ATAWAAMBIA YOTE(kuhusu ujambazi na utekaji akishirikiana na wakimbizi).........! ILA HAITAKUWA GIA YA KUMSHINDA KWANI CCM HUKU HAINA MPINZANI......!
 
nadhani kwa elimu ya msingi RUKWA wameongooza ...sina tatizo nao anyway ingawa kwa karne hii?????anyway anyway
nadhani kwenye hii list kuna wauza madawa ya kulevya (madai sina uthibitisho), mafisadii, walaghai, wazinzi (wanaoambukiza watu VVU kwa makusudi -madai tu sina uthibitisho) na waporaji...yote haya ni sawa tu au ujambazi ni extreme case???
mix with yours
 
hongereni kwa kumtoa selelii.... pia hoja yenu ya uraia imewasaidia sana, well done
 
Nchi imeangamizwa na wasomi, nikianzia na Dr Balali, Dr Andrew,Chenge, Dr Kikwete, Prof Kapuya, Dr Kamala, Dr Nchimbi wale wanasheria wa IMMA nadhani wananchi wanajaribu turufu na wale wasio na elimu! Tanzania bila elimu inawezekana. Nimewapenda hawa kuwa kweli kuliko yule Chitalilo, Dr Mzindakaya, Dr Nagu, Dr Mathayo David
 
Kuna mmoja yule wa Mbeya Vijijini elimu yake wameandika" ANAJIENDELEZA" sijui ndio kisomo chenye manufaa? Chadema wakijipanga vizuri lakini wasiwe OVERCONFIDENT wanaweza kulitwaa hili jimbo.
 
hongereni kwa kumtoa selelii.... pia hoja yenu ya uraia imewasaidia sana, well done

Vibaraka wa mafisadi mnajitokeza mmoja mmoja bila kujijua!! Mmefulia ile mbaya; njaa itawaua!!
 

Kwa hiyo itakombolewa na wa darasa la saba?
 
KWA WALIOPO CHADEMA..........MUULIZENI WAZIRI WA ZAMANI ALIYESHINDWA NA HUYU BWANA ATAWAAMBIA YOTE(kuhusu ujambazi na utekaji akishirikiana na wakimbizi).........! ILA HAITAKUWA GIA YA KUMSHINDA KWANI CCM HUKU HAINA MPINZANI......!

Kwa maana hiyo maadili na elimu si hoja, hongo ndio kigezo cha kiongozi mzuri!

Jamani hapa CCM imeporomoka kabisa, yaani walau wangeweka minimum level Elimu ya Sekondari.

Tutapiga kampeni kali za kuhakikisha huyu Jamal wa Std. 7 hatuwakilishi bungeni.
 
Kwa hiyo itakombolewa na wa darasa la saba?

Mkuu hujanisoma wasomi wetu wanasiasa hawana tofauti na darasa la saba waliowengi! Richmond haikusainiwa na Ngumbalu, Deep green hawakuwa darasa la nne! Mikataba ya kilevi ya madini ni wasomi wetu! wala rushwa na drugs dealers ni wasomi
common hebu waacheni hao wakweli wa elimu ndogo wafanye mambo afterall ubunge hausomewi
 

Mkuu nimekupata

Nadhani hata hivyo ni muhimu hata kujali maadili yao kama wana sifa mbaya au utajiri usiojulikana umepatikanaje. Au ndo tunauza nchi hivyo? Well labda mie sioni mbali.
 
kati ya waliogombea jimboni MUHAMBWE ni yupi ambaye angekuwa right candidate ukiacha suala la rushwa( TOA USHABIKI)
 
HOJA ZA CHaDEMA ZINAFUTWA......JF BWANA!.....maana nimezuiwa!
 

Kigezo cha elimu inaweza isiwe kikwazo kwa huyu bwana lakini biashara zake zinatia mashaka. Ni mfadhili wa siku nying wa CCM pale Kibondo nakumbuka wakati wa kampeni za mwaka 2000, CCM waliandaa chakula cha mchana nyumbani kwa huyu jamaa na Mkapa akashauriwa kutokula mahali hapo kutokana na huyu jamaa kuhusishwa na kashfa ya DC kumbaka mzungu nyumbania kwake mwaka mmoja kabla.
 
Naona hii story ya RaiaMwema la wiki hii inamhusu huyu bwana:



SOURCE: RaiaMwema Toleo 147
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…