Ndio maisha yetu ya sasa

The redemeer

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2025
Posts
1,497
Reaction score
2,681
.

Ukiona mwanamme anamfungulia mlango wa gari mke wake..

Basi Jua huenda gari ni jipya ama mlango ni mbovu..

Sikuhizi mke hampigii simu mume wake akiwa kazini..

Labda awe anaulizia ile condom imefikaje kwenye suruali anayoifua..

Na mume hampigii mke simu mpaka awe anataka kumuelekeza hela ya kula kaiweka chini ya kabati..

Ukiona mke kamuita kimahaba mume wake, basi ujue ana deni la vikoba, ama luku tayari imekwisha..

Ndio Dunia yetu. Mke na mume ukiwaona nje wanapiga story usiku..

Basi ujue ndani wamepulizia dawa ya mbu, wanasubiri iishe nguvu wakalale.

Ukiona wanakaa sebreni pamoja basi ujue Kuna ugeni ama kesi ya mtoto wao.

Huwezi kuona wazazi wakibusiana. Lakini ndani Wana watoto sita..

Ndio familia zetu. Wazazi hawana bond zaidi ya watoto..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…