Sir Good
JF-Expert Member
- Aug 19, 2013
- 1,031
- 412
Heshima kwenu wakuu! Kutokana na ugumu wa maisha niliamua kujinyima nikahifadhi visent vyangu kwenye kibubu lengo lengo nifikishe japo 2ml ili ninunue pikipik na niifanye bodaboda niepukane na adha ya kutumwa.
Bahati mbaya kabla lengo halijatimia, kibarua kikaota nyasi. Kuchungulia kibubu nikajikuta nina million moja na laki moja pesa ambayo siwezi pata pikipiki mpya.
Nikamweleza rafiki yangu mmoja akaniambia kuna kampuni mpya ya kihindi ambayo inauza na pia inakopesha pikipiki aina ya Hero hivyo kama nahitaji naweza kwenda huko.
Nikaenda, kufika mapokezi nikaeleza shida yangu, yule jamaa akaniambia ni kweli kampuni ilikuwa inakopesha ila wamesitisha kutokana na ukorofi wa watu kutopeleka pesa kwa wakati hivyo kazi hiyo ya kukopesha wameikabidhi kampuni nyingine.
Akaniuliza niwapigie simu? ila wao kama kampuni wanauza pikipiki shilingi million moja na laki saba na hamsini ila kwa mkopo kupitia hiyo kampuni waliyoikabidhi nitalipa shilling million mbili na laki mbili, nikamjibu sawa wapigie.
Baada ya maongezi ya muda mfupi yule jamaa akasema "fresh nipe laki saba nikuandikie risit" nikampa, akanikabidhi risit ya kampuni inayoagiza na kuuza pikipiki hapa Tanzania na namba ya simu ya mhusika wa hiyo kampuni inayokopesha hizo pikipik, akampigia tena simu nami pia nikampigia na akaniahidi ndani ya wiki moja nitakuwa tayari nimepata pikipik.
Kweli bwana ilipofika siku jamaa akanipigia simu ili niende nikachukue, nikaenda kampuni ipo barabara ya Nyerere inatizamana kiwanda cha viatu. Kufika pale nikakutana na watu wengine, nakumbuka zilitoka kama pikipik saba hivi.
Nikampa laki 3 akaniandikia risiti. Nimepiga kazi Mungu amenijaalia nimemaliza deni kama miezi 3 hivi iliyopita baada ya kumaliza deni akaniambia nimpatie tin number ili anifanyie mpango wa kadi itayoendana na jina langu kwani hapo mwanzo alinipa kopi yenye jina LA kampuni.
Alinihaidi baada ya mud a mfupi ningeipata kadi lkn sasa miezi inakatika bado sijaipata, nimekuwa nampigia simu kaniongopea weee mpka sasa hana cha kuongopa hivyo ukimpigia simu hapokei, ukibadilisha namba anapokea ukijitamblisha anakupiga sound tu.
Nashindwa hata kubadili namba sababu sina kadi orijino, kuna mtu alitaka kuinunua kwa pesa nzuri tu lakini linapokuja swala la kadi ametoka nduki.
Mbaya zaidi nasikia pikipiki zote zilizotoka kwa njia mkopo zinakamatwa na kampuni inayoziagiza, sasa sijui tatizo liko wapi, mi nimeamua kuifungia ndani tu. Ni hayo tu wakuu ila mnisamehe kwa kuwachosha na maelezo marefu.
Bahati mbaya kabla lengo halijatimia, kibarua kikaota nyasi. Kuchungulia kibubu nikajikuta nina million moja na laki moja pesa ambayo siwezi pata pikipiki mpya.
Nikamweleza rafiki yangu mmoja akaniambia kuna kampuni mpya ya kihindi ambayo inauza na pia inakopesha pikipiki aina ya Hero hivyo kama nahitaji naweza kwenda huko.
Nikaenda, kufika mapokezi nikaeleza shida yangu, yule jamaa akaniambia ni kweli kampuni ilikuwa inakopesha ila wamesitisha kutokana na ukorofi wa watu kutopeleka pesa kwa wakati hivyo kazi hiyo ya kukopesha wameikabidhi kampuni nyingine.
Akaniuliza niwapigie simu? ila wao kama kampuni wanauza pikipiki shilingi million moja na laki saba na hamsini ila kwa mkopo kupitia hiyo kampuni waliyoikabidhi nitalipa shilling million mbili na laki mbili, nikamjibu sawa wapigie.
Baada ya maongezi ya muda mfupi yule jamaa akasema "fresh nipe laki saba nikuandikie risit" nikampa, akanikabidhi risit ya kampuni inayoagiza na kuuza pikipiki hapa Tanzania na namba ya simu ya mhusika wa hiyo kampuni inayokopesha hizo pikipik, akampigia tena simu nami pia nikampigia na akaniahidi ndani ya wiki moja nitakuwa tayari nimepata pikipik.
Kweli bwana ilipofika siku jamaa akanipigia simu ili niende nikachukue, nikaenda kampuni ipo barabara ya Nyerere inatizamana kiwanda cha viatu. Kufika pale nikakutana na watu wengine, nakumbuka zilitoka kama pikipik saba hivi.
Nikampa laki 3 akaniandikia risiti. Nimepiga kazi Mungu amenijaalia nimemaliza deni kama miezi 3 hivi iliyopita baada ya kumaliza deni akaniambia nimpatie tin number ili anifanyie mpango wa kadi itayoendana na jina langu kwani hapo mwanzo alinipa kopi yenye jina LA kampuni.
Alinihaidi baada ya mud a mfupi ningeipata kadi lkn sasa miezi inakatika bado sijaipata, nimekuwa nampigia simu kaniongopea weee mpka sasa hana cha kuongopa hivyo ukimpigia simu hapokei, ukibadilisha namba anapokea ukijitamblisha anakupiga sound tu.
Nashindwa hata kubadili namba sababu sina kadi orijino, kuna mtu alitaka kuinunua kwa pesa nzuri tu lakini linapokuja swala la kadi ametoka nduki.
Mbaya zaidi nasikia pikipiki zote zilizotoka kwa njia mkopo zinakamatwa na kampuni inayoziagiza, sasa sijui tatizo liko wapi, mi nimeamua kuifungia ndani tu. Ni hayo tu wakuu ila mnisamehe kwa kuwachosha na maelezo marefu.