Ndo Projects za Graduates? Matikiti Mengi Sana Dar es Salaam yanapatikana kwa Sh.300/=

Troll JF

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2015
Posts
7,804
Reaction score
12,237
Wakuu nimeshangaa bei ya Matikiti Jana nilivyopita Sokoni na Kununua Tikiti kubwa kwa Tsh. 300/= tofauti na Maneno Mengi ya Kwenye Keyboard yanayosimuliwa na watu wengi ambao wamezaliwa Dar es Salaam ambako hakuna Shamba.

Tukitaka kutoka tufanye Kilimo kwa timing Ikiwemo Mazao ambayo unaweza kuhifadhi hata kama hauna Mteja Matikiti nyanya, Nanasi na Mbogamboga ni Vigumu sana kuyahifadhi.

Supply > Demand = Low Price
 
Una shauri nini mkuu maana hata wewe ni mtanzania mwenzetu saidia kuwashauri graduates nini wafanye kujikwamua maana maisha ya baada ya chuo sote tunayajua
 
Una shauri nini mkuu maana hata wewe ni mtanzania mwenzetu saidia kuwashauri graduates nini wafanye kujikwamua maana maisha ya baada ya chuo sote tunayajua
Wafanye agricultural consultation kabla ya kuingia field na kuanza kujitutumua kwa kutumia maandiko ya inspiration ambayo mara nyingi hayana/hayaweki bayana changamoto watakazo kutananazo field.

Pili waende sokoni wafanye uchunguzi ni kipindi gani kuna mahitaji makubwa ya kile atakachokizalisha ili kuepuka hasara.
 
Kwa sasa maeneo ya pwana mvua zinanyesha,na matikiti yanapenda Maji,hivyo tegemea kuyaona ya kutosha sokoni,mda mzuri wa kulima tikiti Ni kuanzia mwezi wa saba!!
 
Kwa sasa maeneo ya pwana mvua zinanyesha,na matikiti yanapenda Maji,hivyo tegemea kuyaona ya kutosha sokoni,mda mzuri wa kulima tikiti Ni kuanzia mwezi wa saba!!
Variety ipi hiyo inayopenda maji mkuu??!
 

Tikitimaji KUBWA kwa shilingi mia tatu (Tsh. 300/=)? Unaweza ukafafanua ni la ukubwa gani mkuu, like kilo ngapi? Na soko lipi ulikokuta bei hiyo?
 
Nimetoka kununua tikiti moja kwa 3500/- jioni hii.

Hiyo ya 300 wanauza wapi?
 
Nimetoka kununua tikiti moja kwa 3500/- jioni hii.

Hiyo ya 300 wanauza wapi?
Huyo muongo, matikiti ya size ndogo 2000, ya kati 3000-4000 na makubwa 5000-6000 tena nimenunua Leo.

Atuambie hiyo bei ni ya wapi?,
 
Huyu labda atakuwa Nangulukuru si Dar ambapo kipande cha tikiti ni sh 500-1000
 
Mwenye macho haambiwi tazama huu mmea unapingana na sheria za kiuchumi wenyewe when Supply > Demand = The higher the price
Na hata kinyume chake bado the higher the price.
Unahitaji ujasiri tu, na tena unastawi hata ndani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…