Ndoa ina miezi 2 mume kinyesi kinamtoka bila habari

Ndoa ina miezi 2 mume kinyesi kinamtoka bila habari

toplemon

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2017
Posts
4,612
Reaction score
4,721
MUME WANGU KINYESI KINAMTOKA KILA SAA NA NDOA INA MIEZI MIWILI

Naomba unisiadie Kaka maana sijui nafanya nini[emoji24][emoji174], niko kwenye ndoa ina miezi miwili sasa. Mume wangu kabla ya kuoana tulikaa kwenye Mahusiano kwa miezi 3 tu, alikuja kanisani kutafuta mchumba ndiyo akaelekezwa kwangu.

Aliniambia moja kwa moja anataka kunioa na hataki kunichezea, familia yake naifahamu na kila mtu anamjua, ni ana kazi nzuri na kipato chake kiko vizuri. Sikuona shida basi maandalizi yakaanza na tukafunga ndoa.

Siku ya kwanza tuko chumani alikua ni mtu wa aibu sana, akawa kama hataki kuvua nguo mbele yangu, niliona kama vile kaokoka sana labda ndiyo mara yetu ya kwanza nikaamua kumpotezea. Aliingia chooni akavulia nguo huko, ila nilishangaa kumuona anafua nguo zake za ndani usiku huohuo.

Ingawa nilishangaa lakini sikumuuliza chochote. Alirudi kitandani na tulifanya mapenzi vizuri tu na mimi niliridhika tena sana. Sio mwanaume wangu wa kwanza hivyo nilijua tofauti na alikua vizuri ziadi hata ya ma-X wangu.

Kila kitu kilikua vizuri kwakua tulikua tunashinda ndani sikuona chochote. Baada ya siku tatu tulirudi nyumbani, ila tukiwa nyumbani kuna kitu nilishtuka, kulikua na Pedi nyingi sana kwake maboX kama mawili tena yale makubwa.

Nilimuuliza za nini, ankaniambia ni rafiki yake alikuja akasahau anaziuza lakini atamtumia. Basi nikakaa kimya, lakini kaka asubuhi akivaa nguo kwenda kazini anakua kama anajificha nisimuone, anavalia chooni na akirudia ataingia chooni moja kwa moja kuvua kishaa atatoka na vitu kwenda kutupa, sikutaka kuuliza kwani ndoa ilikua bado changa.

Lakini nilishtuka nikaanza kuchunguza, mwanzo sikuona kitu, mwisho nikafuatilia ile mifuko ambayo kila akitoka kazini anaingia chooni na kwenda kuitupa, kuangalia Kaka niligundua kuwa mume wangu anavaa pedi, anaidumbukiza matakoni kwa nyuma ili nguo zake za ndani zisichafuke.

Niliangalia ile mifuko ambayo anaichanganya kwenye mifuko ya taka nikaja kujua kuwa ina mavi. Nilishuka lakini sikumuuliza, katika kumchunguza kuna siku anavua nguo chooni naona mavi yanadondoka wakati hata hajamalizia kuvua.

Aliponiona alishtuka lakini hakuongea kitu, ila baada ya hapo sijui ndiyo kashindwa kujizuia kwani sasa hivi ni yanatoka bila yeye hata kujijua. Akiwa nyumbani anaweza kuwa kakaa kwenye kochi unasikia harufu ukiangalia ni mavi yanatoka. Nikitaka kumuuliza ananikwepa, haniambii chochote anakua mkali.

Kaka naomba unisaidie sijui nafanya nini maana ndoa bado changa ndiyo kwanza tuna miezi 2, mwanaume hataki kuongea na sasa hivi ni kama hajali.

Akienda kazini ni atajifunga funga huko nyuma ili kujizuia ila akirudi hatahajali anakua huru nashindwa nifanye nini kaka na hii hali sijui mume wangu ana matatizo gani?
 
MUME WANGU KINYESI KINAMTOKA KILA SAA NA NDOA INA MIEZI MIWILI

Naomba unisiadie Kaka maana sijui nafanya nini[emoji24][emoji174], niko kwenye ndoa ina miezi miwili sasa. Mume wangu kabla ya kuoana tulikaa kwenye Mahusiano kwa miezi 3 tu, alikuja kanisani kutafuta mchumba ndiyo akaelekezwa kwangu.

Aliniambia moja kwa moja anataka kunioa na hataki kunichezea, familia yake naifahamu na kila mtu anamjua, ni ana kazi nzuri na kipato chake kiko vizuri. Sikuona shida basi maandalizi yakaanza na tukafunga ndoa.

Siku ya kwanza tuko chumani alikua ni mtu wa aibu sana, akawa kama hataki kuvua nguo mbele yangu, niliona kama vile kaokoka sana labda ndiyo mara yetu ya kwanza nikaamua kumpotezea. Aliingia chooni akavulia nguo huko, ila nilishangaa kumuona anafua nguo zake za ndani usiku huohuo.

Ingawa nilishangaa lakini sikumuuliza chochote. Alirudi kitandani na tulifanya mapenzi vizuri tu na mimi niliridhika tena sana. Sio mwanaume wangu wa kwanza hivyo nilijua tofauti na alikua vizuri ziadi hata ya ma-X wangu.

Kila kitu kilikua vizuri kwakua tulikua tunashinda ndani sikuona chochote. Baada ya siku tatu tulirudi nyumbani, ila tukiwa nyumbani kuna kitu nilishtuka, kulikua na Pedi nyingi sana kwake maboX kama mawili tena yale makubwa.

Nilimuuliza za nini, ankaniambia ni rafiki yake alikuja akasahau anaziuza lakini atamtumia. Basi nikakaa kimya, lakini kaka asubuhi akivaa nguo kwenda kazini anakua kama anajificha nisimuone, anavalia chooni na akirudia ataingia chooni moja kwa moja kuvua kishaa atatoka na vitu kwenda kutupa, sikutaka kuuliza kwani ndoa ilikua bado changa.

Lakini nilishtuka nikaanza kuchunguza, mwanzo sikuona kitu, mwisho nikafuatilia ile mifuko ambayo kila akitoka kazini anaingia chooni na kwenda kuitupa, kuangalia Kaka niligundua kuwa mume wangu anavaa pedi, anaidumbukiza matakoni kwa nyuma ili nguo zake za ndani zisichafuke.

Niliangalia ile mifuko ambayo anaichanganya kwenye mifuko ya taka nikaja kujua kuwa ina mavi. Nilishuka lakini sikumuuliza, katika kumchunguza kuna siku anavua nguo chooni naona mavi yanadondoka wakati hata hajamalizia kuvua.

Aliponiona alishtuka lakini hakuongea kitu, ila baada ya hapo sijui ndiyo kashindwa kujizuia kwani sasa hivi ni yanatoka bila yeye hata kujijua. Akiwa nyumbani anaweza kuwa kakaa kwenye kochi unasikia harufu ukiangalia ni mavi yanatoka. Nikitaka kumuuliza ananikwepa, haniambii chochote anakua mkali.

Kaka naomba unisaidie sijui nafanya nini maana ndoa bado changa ndiyo kwanza tuna miezi 2, mwanaume hataki kuongea na sasa hivi ni kama hajali.

Akienda kazini ni atajifunga funga huko nyuma ili kujizuia ila akirudi hatahajali anakua huru nashindwa nifanye nini kaka na hii hali sijui mume wangu ana matatizo gani?
Nitaendelea kusoma utakavyo kuwa unajibiwa mwanzo mwisho.
Mie Sina any comments
 
Mmh! Kwa namna hii ni dhahiri kabisa kwamba mumeo alishapoteza nati zote zinazoshikilia tyre, pole sana haya maisha ni taabu sana sometimes 🤔🤔
 
Back
Top Bottom