Ndoa ni mfano wa computer

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
Kama Computer Vile!




Ndoa ni mfano wa computer.
Kwani computer hukupa kile kimewekwa tu, huwezi kutumia program ya MS Word kama haijawekwa, huwezi kupata internet kama haijawa connect na internet.
Ndivyo ndoa zilivyo
Ukiweka takataka utapata takataka.
Ukiwekeza katika mke kujisikia vizuri na utavuna mume anayejisikia vizuri.
Usipowekeza upendo ndani ya ndoa hauwezi kupokea upendo.
No water in, no water out period!
Hakuna kuwekeza mawasiliano mazuri usitegemee kuwa na mawasiliano mazuri
Ukiilea vizuri ndoa yako itakuwa oasis katikati ya jangwa, na usipowekeza katika kuilea itakuwa jangwa la sahara.
Mke akiweza heshima kwa mume wake, atavuna upendo kutoka kwa mume wake.
Mume akiwekeza upendo kwa mke wake; atavuna heshima kutoka kwa mke wake.
Mume akiwekeza kuwa karibu na mke, kuwa waza kwa mke, atavuna tendo la ndoa linaloridhisha.
“Marriage is the art of two incompatible people learning to live compatibly
 
Ni Zawadi!



Tendo la ndoa ni zawadi (God-given) Binadamu tumepewa katika ndoa.
Hii ina maana kwamba shetani hawezi kutoa chochote zaidi ya kuharibu maana.
Tendo la ndoa ni ubunifu wa Mungu mwenyewe kwa ajili ya mke na mume kuwa mwili mmoja.
Wimbo ulio bora 4: 1-16
Mungu aliumba tendo la ndoa (sex) ili kuwaunganisha mke na mume kiroho na kimwili.
Kutoka kwa mmoja Adamu wakaumbwa wawili (Adam na Eva) na hawa wawili hawakamiliki hadi wawe mmoja tena kupitia tendo la ndoa katika ndoa.
Mwanzo 2:23-24
Mungu aliumba tendo la ndoa lenye mipaka kamili.
Mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa ni uhalibifu na kuna matokeo mabaya kiroho na kimwili.
Mathayo 19:5 -6
Katika tendo la ndoa, wanandoa huweza kunufaika na kuwa kitu kimoja (Mwanzo 2:24), kufarijiana (Mwanzo 24:67), kuijaza dunia (Mwanzo 1:28) pia kwa kujilinda na majaribu ya dunia (1Wakorintho 7:2, 5)
 

Hii nimeipenda imakaa vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…