warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,218
- 18,440
HABARI kubwa ya mjini hivi sasa , hasa
kwenye mitandao ya kijamii ni juu ya madai
mazito ya kuvunjika kwa ndoa ya selebriti
wawili Bongo, staa wa muziki wa Kizazi
Kipya, Judith Wambura Lady Jaydee au
Jide na mtangazaji maarufu wa Radio
Times FM , Gardner G . Habash , iliyofungwa
Mei 14, 2005, Ijumaa linamaliza utata .
KABLA
Kabla ya Gardner kufunguka , habari zilidai
kwamba wawili hao walikuwa kwenye gogoro
zito ambapo Gardner aliamua kuondoka
katika nyumba waliyokuwa wakiishi pamoja
iliyopo Kimara - Temboni , Dar .
Ilidaiwa kwamba baada ya kuondoka
nyumbani eti Gardner alikwenda kukaa kwa
mmoja wa ndugu zake .
Habari hizo za kwenye mitandao ambazo
hazitaji chanzo cha kuvunjika kwa ndoa hiyo ,
zilidai watu wa karibu na familia hiyo
walisema hiyo siyo mara ya kwanza kwa
wawili hao kutengana , lakini mzozo wa safari
hii unaweza ukawa wa moja kwa moja .
ACHA BWANA
Ilidaiwa kwamba ni kutokana na kutemana
huko, ndiyo maana Jide msanii anayetajwa
kuwa ni miongoni mwa wenye mafanikio
kimaisha Bongo, hakwenda Kituo cha Polisi
Oysterbay, Dar kumwangalia mumewe
ambaye aliwekwa korokoroni kufuatia kitendo
chao cha kuwakimbia askari wa usalama
barabarani akiwa na Ephraim Kibonde hivi
karibuni .
MAFUMBO?
Ilisemekana kuwa hisia za kuachana huko
zinachochewa pia na baadhi ya maandiko
ambayo mwanamuziki huyo wa Kibao cha
Yahaya , amekuwa akiyaweka katika akaunti
zake za mitandao katika siku za hivi
karibuni .
Ilielezwa kwamba katika akaunti yake ya
Mtandao wa Istagram, Jide aliweka picha
yake akiwa amesimama nje ya gari lake
kisha akasindikiza kwa kuandika hivi :
Walking away from troubles, maneno
ambayo kwa tafsiri isiyo rasmi yanamaanisha
kujiondoa kwenye matatizo .
BINTI MACHOZI?
Ilidaiwa kuwa kabla ya hapo , katika mitandao
inaandikwa kuwa Jide pia aliweka picha yake
akionekana kuwa na huzuni huku Binti
Machozi akilengwalengwa na machozi na
kusindikizia na maneno akiuliza : Sijui
nisemaje ?
GARDNER ANASEMAJE?
Mtu wa kwanza kupigiwa simu alikuwa ni
Gardner ambaye aliipokea na kabla
hajaelezwa chochote , alisema alikuwa katika
sehemu ambayo asingeweza kuzungumza ,
hivyo angempigia mwandishi wetu baada ya
robo saa.
JIDE VIPI?
Baada ya kukata simu, mwandishi wetu
alimwendea hewani Jide na baada ya kuita
kwa muda , simu yake ilipokelewa na Gardner
akasema: Mpigie baada ya robo saa.
DAKIKA 20 BAADAYE, GARDNER AFUNGUKA
Dakika ishirini baadaye , Gardner alimtumia
ujumbe mfupi wa simu mwandishi wetu na
kumweleza kuwa alikuwa Kituo cha Polisi
Oysterbay, Kinondoni jijini Dar ambako aliitwa
kwa ajili ya soo lao la kuwakimbia trafiki.
Baada ya kubadilishana maneno kadhaa,
baadaye aliamua kupiga na mazungumzo kati
yake na Ijumaa yalikuwa kama ifuatavyo ;
Ijumaa : Ebwana hivi hizi habari kwenye
mitandao juu ya kuvunjika kwa ndoa yako na
Jide zimekaaje ?
Gardner: Hamna kitu bwana, watu
wanaunganisha tu vitu sijui kwa sababu gani.
Ijumaa : Sasa kama ni hivyo kwa nini Jide
hakuja kukuona siku ile ulipolala polisi ?
Gadner : Unaona sasa , wao wanajua hivyo ,
lakini siyo kweli , Jide alikuja usiku sana kwa
sababu alikuwa anawaogopa mapaparazi .
Unajua Jide yeye huwa hapendi hayo mambo .
Alikuja usiku sana, lakini hata hivyo polisi
nao walimgombea sana kumpiga picha.
Ijumaa : Wanasema Jide kuna maneno
amepost kwenye akaunti zake mitandaoni
zinazoonyesha kuchoshwa na wewe ,
unasemaje?
Gardner: Si ndiyo kama hivyo nimekuambia ,
watu wanaungaunga tu vitu ambavyo
hawavijui na sisi hata hatujui malengo yao.
Wakati ule uliponipigia simu mara ya kwanza
nilikuwa naye kwenye gari ananipeleka pale
polisi , lakini akapaki mbali kwa sababu
hiyohiyo niliyokuambia kuogopa mapaparazi
na si unakumbuka hata ulipompigia kwenye
namba yake nilipokea mimi ?
Ijumaa : Kwani upo naye hapo sasa hivi
nimsalimie?
Gardner: Hapana tumeachana mimi niko
kwenye usafiri mwingine naelekea kazini na
yeye yupo kwenye misele mingine .
Ijumaa : Haya kaka basi poa .
Gardner: Poa kaka , mchana mwema .
kwenye mitandao ya kijamii ni juu ya madai
mazito ya kuvunjika kwa ndoa ya selebriti
wawili Bongo, staa wa muziki wa Kizazi
Kipya, Judith Wambura Lady Jaydee au
Jide na mtangazaji maarufu wa Radio
Times FM , Gardner G . Habash , iliyofungwa
Mei 14, 2005, Ijumaa linamaliza utata .
KABLA
Kabla ya Gardner kufunguka , habari zilidai
kwamba wawili hao walikuwa kwenye gogoro
zito ambapo Gardner aliamua kuondoka
katika nyumba waliyokuwa wakiishi pamoja
iliyopo Kimara - Temboni , Dar .
Ilidaiwa kwamba baada ya kuondoka
nyumbani eti Gardner alikwenda kukaa kwa
mmoja wa ndugu zake .
Habari hizo za kwenye mitandao ambazo
hazitaji chanzo cha kuvunjika kwa ndoa hiyo ,
zilidai watu wa karibu na familia hiyo
walisema hiyo siyo mara ya kwanza kwa
wawili hao kutengana , lakini mzozo wa safari
hii unaweza ukawa wa moja kwa moja .
ACHA BWANA
Ilidaiwa kwamba ni kutokana na kutemana
huko, ndiyo maana Jide msanii anayetajwa
kuwa ni miongoni mwa wenye mafanikio
kimaisha Bongo, hakwenda Kituo cha Polisi
Oysterbay, Dar kumwangalia mumewe
ambaye aliwekwa korokoroni kufuatia kitendo
chao cha kuwakimbia askari wa usalama
barabarani akiwa na Ephraim Kibonde hivi
karibuni .
MAFUMBO?
Ilisemekana kuwa hisia za kuachana huko
zinachochewa pia na baadhi ya maandiko
ambayo mwanamuziki huyo wa Kibao cha
Yahaya , amekuwa akiyaweka katika akaunti
zake za mitandao katika siku za hivi
karibuni .
Ilielezwa kwamba katika akaunti yake ya
Mtandao wa Istagram, Jide aliweka picha
yake akiwa amesimama nje ya gari lake
kisha akasindikiza kwa kuandika hivi :
Walking away from troubles, maneno
ambayo kwa tafsiri isiyo rasmi yanamaanisha
kujiondoa kwenye matatizo .
BINTI MACHOZI?
Ilidaiwa kuwa kabla ya hapo , katika mitandao
inaandikwa kuwa Jide pia aliweka picha yake
akionekana kuwa na huzuni huku Binti
Machozi akilengwalengwa na machozi na
kusindikizia na maneno akiuliza : Sijui
nisemaje ?
GARDNER ANASEMAJE?
Mtu wa kwanza kupigiwa simu alikuwa ni
Gardner ambaye aliipokea na kabla
hajaelezwa chochote , alisema alikuwa katika
sehemu ambayo asingeweza kuzungumza ,
hivyo angempigia mwandishi wetu baada ya
robo saa.
JIDE VIPI?
Baada ya kukata simu, mwandishi wetu
alimwendea hewani Jide na baada ya kuita
kwa muda , simu yake ilipokelewa na Gardner
akasema: Mpigie baada ya robo saa.
DAKIKA 20 BAADAYE, GARDNER AFUNGUKA
Dakika ishirini baadaye , Gardner alimtumia
ujumbe mfupi wa simu mwandishi wetu na
kumweleza kuwa alikuwa Kituo cha Polisi
Oysterbay, Kinondoni jijini Dar ambako aliitwa
kwa ajili ya soo lao la kuwakimbia trafiki.
Baada ya kubadilishana maneno kadhaa,
baadaye aliamua kupiga na mazungumzo kati
yake na Ijumaa yalikuwa kama ifuatavyo ;
Ijumaa : Ebwana hivi hizi habari kwenye
mitandao juu ya kuvunjika kwa ndoa yako na
Jide zimekaaje ?
Gardner: Hamna kitu bwana, watu
wanaunganisha tu vitu sijui kwa sababu gani.
Ijumaa : Sasa kama ni hivyo kwa nini Jide
hakuja kukuona siku ile ulipolala polisi ?
Gadner : Unaona sasa , wao wanajua hivyo ,
lakini siyo kweli , Jide alikuja usiku sana kwa
sababu alikuwa anawaogopa mapaparazi .
Unajua Jide yeye huwa hapendi hayo mambo .
Alikuja usiku sana, lakini hata hivyo polisi
nao walimgombea sana kumpiga picha.
Ijumaa : Wanasema Jide kuna maneno
amepost kwenye akaunti zake mitandaoni
zinazoonyesha kuchoshwa na wewe ,
unasemaje?
Gardner: Si ndiyo kama hivyo nimekuambia ,
watu wanaungaunga tu vitu ambavyo
hawavijui na sisi hata hatujui malengo yao.
Wakati ule uliponipigia simu mara ya kwanza
nilikuwa naye kwenye gari ananipeleka pale
polisi , lakini akapaki mbali kwa sababu
hiyohiyo niliyokuambia kuogopa mapaparazi
na si unakumbuka hata ulipompigia kwenye
namba yake nilipokea mimi ?
Ijumaa : Kwani upo naye hapo sasa hivi
nimsalimie?
Gardner: Hapana tumeachana mimi niko
kwenye usafiri mwingine naelekea kazini na
yeye yupo kwenye misele mingine .
Ijumaa : Haya kaka basi poa .
Gardner: Poa kaka , mchana mwema .