Kuna mambo mengi sana yanayochangia ndoa nyini siku hizi kuto dumu, kwanza ni watu kutokuwa na hofu ya Mungu, unajua hofu ya Mungu ndani ya Moyo wako itakuzuia kufanya mambo mengi ambayo hayana maana.
Lakini pia jambo lingine ni tamaa, watu tumekuwa na tamaa ya kutaka kuishi maisha ambayo yako nje ya uwezo wetu, mtu huna uwezo wa kununua lakini unatamani kumiliki ndege, kwa hiyo watu wanaingia katika ndoa wakiwa na matazamio makubwa sana mwisho wa siku yanawashinda wanaanza ubabaishaji.
Kukosekana kwa uvumilivu, watu tumekwa si wavumilivu tena na kujifanya wajuaji jambo ambalo linaleta ushindani ndani ya ndoa na matokeo yake badala ya kusonga mbele mnaanza kushindana. Watu watumie muda kufahamiana vema kabla hawajaamua kuingia ndani ya ndoa, ndoa si mchezo wa kuigiza.
Mwisho kabisa ili niwaachie watu wengine nao nafasi ya kuchangia nadhani suala la watu kutokuonyesha uhalisia wa maisha yao toka mwanzo wa uhusiano nalo ni tatizo, be yourself kama unataka kufanikiwa katika mambo yako.
Mwombe Mungu akupe Mke mwema ama Mume mwema utaishi katika ndoa kwa amani na upendo.