Ndoa zetu na umiliki wa mali...kizungumkuti kingine!!


Asante Michelle kwa mchango wako. Sina hakika lakini nadhani sheria ya ndoa haiwatambui watoto kama warithi wa mali ya ndoa endapo hakuna wosia. Kwa hiyo kuandika majina ya watoto siyo suluhisho. Bado napendekeza kwanza tujitahidi kuelewa nini kinahusika kama mali za ndoa kwa mujibu wa sheria. Pili tujadiliane na wenzetu. Hakuna njia ya mkato!

Pia nawaonea huruma wanaume wanaojidai kuficha. Endapo Mke akitoa ushahidi kuwa hizo mali zilipatikana kwenye ndoa hata kama ziko sayari nyingine zitapigwa panga 50% by 50%. Kwa hiyo wanawake wajitahidi kufuatialia na kupata nyalaka za mali ambazo waume zao wanajidai kuficha. Hiyo ndiyo dawa yao watu wa namna hiyo!!
 
<p>
[/COLOR]</p>
<p>&nbsp;</p>
<p><font color="black">itakuwa safi hiyo ...lol,</font>
</p>
<p>&nbsp;</p>
mi nna aibu aisee,sitadhubutu kuchukua.ntamrithisha mama yake.upendo haujitangulizi.
 
Kwa Roman Catholic, kanisani pia wanatoa huduma ya kutunza wosia. Umewahi kufuatilia hiyo alternative?

ASANTE NILIKUWA SILIJUI HILI,
itabidi nifuatilie, ikiwezekana nikaondoe RITA manake ghalama zinaanza kunishinda,
na ukizingatia hata sijui nitakufa lini,
je nikifa na miaka 100...lol
si itabidi niwe nalipia miaka yote hiyo ,,,lol.
 
kaka wewe umeshaandika? na ulianzaje kumshirikisha mama DC?

Mimi nimeandika very simple.

1. Mali zetu tulizonazo sasa (list imewekwa) na zile tutazopata baada ya kuandika wosai huu zitamilikuwa na Mama DC na atazitumia kuwaendeleza watoto wetu hadi wawe watu wazima. Baada ya hapo ataamua kuwapa kila mtoto chake kutegemea na utashi wake (ni mama yao, kwa hilo na-asume hawezi kuwazika)!!
2. Mama DC atawatunza wazazi wangu na wake kwa kuendelea kuwapa msaada kama tunavyofanya sasa ila kutegemeana na uwezo utakaokuwepo. Kama hilo litaonekana kuwa gumu basi awapatie &#8804;10% ya mali zetu za ndoa.
3. Relatives ambao tunawasaidia ataendelea kuwasaidia kutegemeana na uwezo wa familia.

Nilimweleza tu mama DC kwa maneno kuwa nitaandika wosia ila hajui kama nimeshaandika tayari. Pia haya mambo nayasema kila siku kwake na kwa tu wengine. Sitaki hata siku moja ndugu zangu waje kumnyanyasa. Ila sasa kuna mambo ya biashara na hayo ndo nataka tuandike mkataba wa umiliki by shares ili yasihesabiwe kwenye mali za ndoa. Umenipata?


Mwisho!
 
Acha woga THE FINEST...lol,
kwanini wakuharakishe ikiwa warithi wanakuwa hawajui,
ulichokiandika humo ndani...
labda waambiwe na shahidi au mwanasheria wako,
Acha bana chukua hatua...lol
Aha aha nnunu nimejenga hoteli mbili moja Zanzibar nyingine Bagamoyo kwahiyo wanataka niwarithishe mapema ndio maana nimestuka
 

sasa hapo kaka ina maana bila kumshirikisha yeye mie niandike mwenyewe na zake je? c bado tatizo litakuwa pale pale?....
 




Dark city hii issue iko so delicate hasa kwa familia zetu za kiswahili, hata muwe morden kiasi gani hizi underlying factors zinashindwa kabisa kurahisishwa na kuwekwa wazi. Nilipoona hii thread cha msingi imebidi nimfuate Huby kazini kumwambia wazo langu la kuweka mambo sawa kuhusu mali zetu... Nimewasha moto, anadai "What! Ar you planning to kill me?" Hajawahi niambia maneno makali kama hayo. Na huyo ni msomi ..... yaani kazi ipo
 
<p></p>
<p>&nbsp;</p>
mi nna aibu aisee,sitadhubutu kuchukua.ntamrithisha mama yake.upendo haujitangulizi.

utakuwa umetenda wema mkubwa sana,
na ni nadra kutolewa na watu na hasa wa karne ,
hii tuliojaa tamaa za mali hata tusizopata kwa jasho letu.

Lakin sometimes kusema ni rahisi kuliko kutenda....lol
 
Mkuu DC topic nzuri

Nizungumzie tu kipengele kimoja cha uwazi katika mapato na matumizi...hivi ni kwa nini kwa wengine wanaona kuwa ni vigumu kuweka wazi kipato chako na matumizi yako kama kweli mpo na mnapendana kiukweli?

Kwenye mapenzi ya ukweli mali/pesa shouldnt be an issue kwa kweli....ni suala la kushare na kupanga mipango pamoja....hili litasaidia hata wakati wa mirathi nk., manake mwenzio anakuwa anajua mnamiliki nini na wapi, pesa kiasi gani zipo etc...
 
Imekaa uzuri hii
 
DC suala la wosia liache tu hivyo hivyo wengine wakijua tayari umeandika urithi wako tayari kuchukua maisha yako ili wachukue chao mapema kabisa





TF kuna option pia ya kuandika wosia bila hata ndugu kujua kua u have done that.
 
sasa hapo kaka ina maana bila kumshirikisha yeye mie niandike mwenyewe na zake je? c bado tatizo litakuwa pale pale?....

Nyamayao,

Nadhani kuna kitu bado hatuelewani. Kwanza uelewe kuwa mali za ndoa umiliki wake ni 50% kwa kila mwanandoa. Pili huwezi kuandika wosia wa mali za mwenzio. Andikia hiyo 50% yako. Je ukifa leo ungependa apewe nani?

Unaweza pia kushauri itolewe kwenye charity foundations. Why not?
 

POLE SANA, ILA NAHISI UMEFANYA HARAKA ...lol,
siyo issue ya kuambiana kazini hii, linahitaji muda,utulivu na mahali mwafaka,

PIA SIYO HUYO TU MWENYE MTAZAMO KAMA HUO WA RED BALI NI WENGI SANA,
WENYE MTAZAMO NA MSIMAMO KAMA HUO.
HAIJALISHI NI MSOMI AU HAJASOMA.

MTAKAPORUDI NYUMBANI ONGEENI KWA KIREFU NA KWA UTULIVU,
PIA UKIONA HAELEWI AU HAPENDI WALA USILIENDELEZE,
LISIJE LIKAWA NDIYO CHANZO CHA KUTOELEWANA KWENU.

LABDA KWA SIKU ZA BAADAYE UNAWEZA KUMKUMBUSHIA TENA.
 
<p>
kazi kweli kweli, so natakiwa niandike mpaka bra na underskirt?...bwana king'asti mie ctaki, hebu hao wanasheria bac mjitokeze mtutoe matongotongo jamani....
</p>
<p>&nbsp;</p>
hehehe,utakoma!manake kuna watu utadhani wachawi aisee.usisahau na kopo la kuogea.ila ni ngumu aisee,na dc anasema tena watoto hawakubaliki!wenzetu ulaya wanateua na guardian wa watoto (baba mkwe wangu alifanya hii,it was easy),manake ukitokea msiba watu wanagombea watoto manake wanajua watapata access ya kila kitu.wakimaliza kutumbua mali mtoto anageuzwa hgeli!
 


Just baseless fears!!
 
<p> </p>
<p>&nbsp;</p>
 




Nafikiri uwazi unakua affected na the type of person you are married to. For instance unakuta wife wako ni spender mno tena spender wa vitu ambavyo c productive, the more you gain the more ana spend. Mshahara ukipanda sidhani kama utakua na guts za kumwambia kua umepanda..
 
<p> </p>
<p>&nbsp;</p>
sasa yangu ni ipi na yake ni ipi?manake kila kitu kinakuwa kimechangiwa na wote,hata in kind tu.na nafasi ya mama ama baba wa nyumbani inakuwaje?coz nilidhani whatever kilichopo ni chetu sote.
 

safi sana dc,
umeweka ulinzi mzuri sana,
kwa mkeo,wazazi,watoto wako na wategemezi wako.
Safi sana sana.

Kuiga kila jambo siyo vizuri,ila kuiga jambo zuri siyo vibaya,
wana jf itakuwa vema kama hili la dc tutaiga na kulifanyia kazi kwa
vitendo. Wosia ni muhimu sana kuandaliwa mapema.
 





Asante, nami nimegundua hilo - saizi namvutia week nzima, leo jioni najipanga kufuta yoote kwa maandalizi moto moto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…