Ndoto yangu, Mtiririko wa hawa maraisi umekosewa ndio maana tunaisoma namba!

Kasimba G

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2011
Posts
3,428
Reaction score
2,612
Wasalaam wana Jambi!

Katika tafakuri yangu nimepata "kajindoto" kua kama taifa timing yetu imekua ndivyosivyo! Yaani mtiririko wa maRaisi ungekua JKN-JPM-BWM-AHM-JMK ingalu hizi hoja za uchwara zisingekuwepo.

Sasa JMK alikua raisi aliyeelewa kua yupo kwenye nyakati za dot com! kilakitu kiko wazi hata ukijificha chumbani au kwenye pango! Ni zama za utandawazi ambapo freedom mean everything! Ndio maana pamoja na kusoma mitandaoni haikumsumbua kwakua alielewa majira na nyakati.

Rafiki yangu mmoja alileta utani ati JMK alikua ameachia critisisms kwa sababu alikua shabiki wa yanga toka pwani! Ati mashabiki wa yanga toka bara ngumi mkononi!!!!! ukimuambia shabiki wa yanga wa bara kesho mechi ya watani nitakuoa!!!! Oups utashangaa pangaaaa!

Mtiririko ulitakiwa uwe kama kajindoto kangu Nchi yetu ingekua imekaa vizuri, kwasasa naona kama tutakwamishana tuu! Maana na utandawazi huu ambapo sekta isiyo rasmi inatiririka dunia nzima lakini hapa kwetu imebatizwa eti inaitwa upigaji.

Ati waliojiajiri na kujikimu wanaitwa wanaoishi kwa ujanja ujanja, wafanyabiashara wanaitwa wahujumu, wafanyakazi wanaitwa wezi, nk.

Watanzania tutanyoka tuu!
 
Anae ona Magu hayupo sahihi huyo hatutakii mema Watanzania,
Uhuru nao unamipaka yake,
Ilifikia hata watu wali idharau serikali na kuongea maneno yakila aina,

Wacha heshima iwepo hapa hata mwaka bado
 
ingekuwa njema kama mtu fulani asingepata zali la kuitwa prezidaa
 
Maisha ya binadamu yanabadirika kufuatana na Mazingira. Well let's say Mazingira ni vitu/ hali inayotuzunguka. So binadamu hata bila kumwambia na kumshurutisha ataishi ili aendane na Mazingira. Once you fight against your environment UTAKUFA. Unatakiwa uendane na Mazingira yako. Kipindi hiki ni cha utandawazi, ukitaka tuishi kwa kufuata kauli ya Mtu mmoja, ama bila kufuata misingi tuliokubaliana, TUTAKUFA. Isitoshe hata hayo makubaliano ni lazima yaendane na Mazingira ya sasa. Mfano katiba ndiyo inatoa misingi ya mahusiano yetu, lazima iendane na Mazingira ya sasa. Bahati mbaya zoezi la Jaji Warioba lilizimwa. Tukaleta Katiba pendekezwa. Je inakidhi lengo; kuendana na Mazingira ya sasa? Attn of Pasco, tujiulize, utawala huu kwanza tunafuata tuliyokubaliana!!? Pili, hata yale tulokubaliana tunayafuata!!? Tatu, tunayoyafanya leo, je hatupingani na Mazingira ya sasa!!!?
 
Mda mwingine tutumie akili japo kidogo.
Mara ngapi tumelalamika juu ya ufisadi nchi hii,je unapendelea serikali kupoteza pesa kwa watumishi hewa,unataka watu wasilipe kodi?
Tumechoka maisha ya kuonekana nchi ni ya wazungu,wa asia na waafrika wachache.
We kama maisha magumu usilazimishe achana nayo shughulika na mambo mengine sio lazima.
 
kwani hapo tatizo nini si JPM angeshamaliza mizizi ya ufisadi hukoo nyuma?
 
Anae ona Magu hayupo sahihi huyo hatutakii mema Watanzania,
Uhuru nao unamipaka yake,
Ilifikia hata watu wali idharau serikali na kuongea maneno yakila aina,

Wacha heshima iwepo hapa hata mwaka bado
mipaka si enzi hizi za utandawazi! enzi za mwalimu sawa ndio maana nimependekeza JPM angemfuatia JKN
 
Mkuu huo mpangilio wako uka sahihi kabisa.Kuna kipindi nchi inasonga mbele na mabadiliko yanaonekana alafu kunakuja kipindi cha giza totoro,maisha magumu tuanrudi nyuma miongo kadhaa.Ukiangalia hiyo orodha unaweza ukatambua kwa sababu gani.Kwanza ni kwa sababu ya background ya maisha ya kiongozi na geograpihcal position anapotoka (kijijini vs mjini),kipato cha kati,maskini au tajiri.Kingine ni roho mbaya au roho nzuri.Kingine kinachosumbua ni uelewa na uzoefu wa masuala ya duniani (diplomatic background) ambayo inawafanya wawe na exposure ya masuala mbalimbali.Kuna watu mpaka leo hii wanaamini kuna wapiga madili wanaookota hela kirahisi.Mwenye fedha anaonekana adui kwao,mnyonyaji,mwizi,fisadi n.k.Hawajui kwamba hiyo ni tuzo/reward ya jitihada zao katika kazi.Kuwa na fedha au kutokua na fedha ndio utofautisha mzembe na mtendaji kazi/anayetegemea akili na mwenye akili za utegemezi.
 
uko sahihi mkuu that is my point!
 
Umesababisha nimemkumbuka edward moringe sokoine roho yake ipumzike pema peponi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…