Uchaguzi 2020 Ndugu, jamaa na marafiki zangu wengi hawana ‘vichinjio’ (Kadi za mpiga kura)

Uchaguzi 2020 Ndugu, jamaa na marafiki zangu wengi hawana ‘vichinjio’ (Kadi za mpiga kura)

Snowden E

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2018
Posts
1,668
Reaction score
2,908
Baada ya suala la uchaguzi wa uraisi na wabunge kupamba moto. Nilianza kufanya utafiti kidogo kwa makundi tajwa kama wametimiza vigezo na masharti ya kushiriki kwenye zoezi la kuchagua viongozi.​

Nili tumia njia ya maswali, na nilifanikiwa kuuliza kwa watu 100.​

Swali lilikuwa moja tu.​
Niliuliza...​
1. Utapiga kura kuchagua kiongozi unayemtaka?​

Nilihitaji jibu la NDIYO AU HAPANA.​
Pia nilihitaji kujua kama jibu HAPANA, je.. kwanini iwe HAPANA?.​

Ila, kabla ya kuanza utafiti, nilitarajia kuwa wengi wa ndugu, jamaa na marafiki zangu, hawana ID za mpiga kura.​

Baada ya kuanza kuuliza swali, majibu yalikuwa hivi...​
80% Walisema HAPANA (hawata piga kura).​
15% Walisema NDIYO (watapiga kura).​
5% Walikataa kujibu.​

SABABU ZA WALIOSEMA HAPANA (WATU 80)
70% Walidai kuwa, hawakwenda kuhakiki kwenye daftari la mpiga kura.​
21% Walidai kuwa, kupiga kura ni kujisumbua na kupoteza muda. Yeyote atakaye chaguliwa ni sawa.​
9% Hawa kuwa na sababu maalumu.​
........... MWISHO..........​
ZINGATIA.​
Utafiti wangu haukujikita kwenye chama chochote cha siasa.​
 
Ayaaaa umeharibuuu. Ungewauliza na kama wangepiga wangewapigia chama gani. Ili tufurahi au tuanze kuwabadilisha upepo.
Mimi wife najuta anamiliki kichinjio. Maana analeta utani na chaguo lake hapo 28 October
 
Wengi waliokua wakisema kupiga kura ni kujisumbua ni wale waliochagua viongozi ambao kura zao hazikutosha kushika dola miaka iliyopita, na haohao ndio wasiokua na vichinjio leo japo wanaenda mikutanoni.

Tuvumiliane tusubiri October 28 kushuhudia matokeo tuu
 
Hilo la kupiga kura ni kujisumbua limekuwa jibu la wengi, wengine vichinjio wanavyo ila wao wanadai kadi zao hutumia ktk shughuli zingine sambamba na namba za nida!
 
Wengi waliokua wakisema kupiga kura ni kujisumbua ni wale waliochagua viongozi ambao kura zao hazikutosha kushika dola miaka iliyopita, na haohao ndio wasiokua na vichinjio leo japo wanaenda mikutanoni.

Tuvumiliane tusubiri October 28 kushuhudia matokeo tuu
Ni wale waliopigia kura viongozi waliopo madarakani na wanaona hakuna wanachofanya kubadili maisha yao
 
Kwa hiyo unataka kuwaambia watanzania takwimu za watu milioni ishirini na tisa waliohakikiwa kuwa ndo wakiojiandikisha hazipo? Mkiwa mnatoa hoja angalia mamlaka husika zishasema nini . Ukiambiwa wewe ni ,chochezi utakataa?
 
Back
Top Bottom