Ama kweli, tunasahau mno upesi! Sera ya soko huria ilipitishwa 1984, Mh Alhaji Mwinyi alichaguliwa kuongoza nchi 1985! Uamuzi wa watanzania wa au kuwa na sera ya vyama vingi ama la ulipigiwa kura (referandum) na wengi wakataka wabaki na chama kimoja, Nyerere akalazimisha pamoja na haja ya kuheshimu demokrasia, nchi haikuwa na budi walau wakati ule kuupa uzito uamuzi wa wachache yaani kuchagua kuwa na sera ya vyama vingi. Ni pale Zanzibar tu ambako hatujui kilichojiri, hakuna sera yeyote iliyowekwa wazi pale, ni vurugu tu! Sasa wewe Bimkonge na wengine, mnawezaje kudhani Mwinyi ndiye aliyeboresha sera wakati unaona kabisa Nyerere akiwa ni kinara wa kuleta soko huru (1984) na sera ya vyama vingi(1991)?
Lakini yote tisa, sera na mfumo sio miliki ya mtu mmoja!!! Hata huko Marekani, hakuna kinachobadilika eti tu kwa kuwa yupo Obama, yale yale yanaendelea, ni harafu tu ya juu tunayoona kama kihalalisho cha kuwepo aliye katika madaraka....habari ndio hiooo