Ndugu wa Tanzania Mnakielewa chanzo cha Misukosuko ya Nchi? (Ali H. Mwinyi)

Bintimkonge asante kwa kufafanua, ni kweli kabisa Tanzania haikuwa nchi pekee iliyokuwa na uhaba wa bidhaa enzi zile. Hata wenzetu wa Zambia ambao walionekana kuwa na unaffuu (kama mnakumbuka zile sabuni muruwa za bafuni kutoka Zambia enzi hizo) walitamba kwa siku chache tu kabla ya 'new international economic order' kuwakumbatia! Naamini kabisa ni kosa kufikiri kwamba matatizo/mafanikio ya uchumi kwa nyakati fulani yanawiana na sera binafsi za kiongozi fulani. Nionavyo Nyerere angekuwa ni kiongozi wa awamu ya tatu, ukuzi uchumi ungaliweza kuwafaidi wengi zaidi kuliko ilivyokuwa.

Dhana nninayoilaani kwa nguvu zote ni hii ya umimi au uyeye katika maendeleo ya taifa. Inavunja nguvu za wale wanaopenda kujenga. Tukiamini kuwa sio rais na wala nani tuliyemchagua anaweza kubadili mwenendo wetu wa maendeleo, tunajiwekea uwigo mkubwa wa maendeleo. Sharti ni moja tu hao viongozi wawe kweli ni matunda ya demokrasia ili wasimamie yale tunayoyataka, sio wao wajisemee eti uwazi na ukweli wakati sisi tunaamini tofauti, au ari mpya maisha bora wakati hata hatung'amua tuko na ari gani. Naamini ni dhambi kupachika majina ya viongozi kwa miradi mbalimbali, mara eti ni Daraja la sijui Mkapa(wapi na wapi jamaini Mkapa hajaanza uwaziri, watu walikuwa wanajadili ujenzi huo), Sijui BWMkapa Towers badala ya Mafuta House hali mradi huo ulikuwepo tangu miaka ya 1970 ikawa imecheleweshwa na Kumekucha Auction Mart kama wapangaji, na mradi ukaanza kwa mikiki kabla ya 1995. Tusiwape sifa watu bila sababu
 

huyo kaisha eleke kunapotakia anaonge kwa kumtetea nyerere

ufisadi ulikuwepo toka kwa huyo jamaa pia mtoto hupatikana baada ya kutunga mimba halafu kuzaliwa na kuanza kukua

kwa sasa ufisadi ni mkuwa saana angalai mafisadi waliotajwa awamu hii wametokea awamu ipi?
 

HAyo maamuzu magumu mugumu yametusaidia nini?

Na nani alishgulikia? na faida yake

kujenga majumba na kuweka jina la mwezako ilikuwa ni uwoga wakati wa hujumu uchumi lakini kijana sasa hivi toka alipoachi madaraka nyerere nani atakaye kusumbua ukiweka jula lako ukijenga nyumba hata tatu
 
Binafsi mimi ninadhani kuwa pamoja na udhaifu wake wa kutokuwa madhubuti kiongozi, Mwinyi alijenga msingi mkubwa sana wa demokrasi kwa kutumia ile filosofi yake ya RUKSA. Ninachomlaumu zaidi ni pale alipotumia filosofi hiyo kukubali uanzishwaji wa mfumo wa vyama vingi vya siasa bila kujenga level ground kwa vyama hivyo; matokeo yake Tanzania imekuwa na vyama dhaifu hadi leo kwa vile chini ya mfumo uliokuwapo wa Chama Kushika Hatamu, CCM ilikuwa na raslimali nyingi sana za kitaifa tofauti na kwa majirani zetu wa Kenya, Zambia na Malawi ambako hawakuwa na hizo sera za Chama kushika Hatamu.
 


Sadakta Bwana Mkubwa, Hakukukuwa na viongozi waroho Sasa nani alitafuna vyama vya Ushirika? Nani alishusha uzalishaji wa mashamba makubwa? Nani aliviondowa Viwanda? Hivyo umasikini uliokuwepo katika MIAKA YA 1980 ULIKUWEPO WAKATI TUKIPATA UHURU?
Kuhusu hili la kurapa na uchaguzi wa bidhaa nahisi wewe ni Bwana mdogo hukuonana huo wakati. Kwa kweli kulikuwa hakuna uchaguzi si bidhaa muhimu si anasa zilizokuwepo wakati huo. Pengine ungewauliza wakubwa wako nini maduka ya RTC?
 


Alaa kumbe ni wale wa kiwaraka waraka. Bora usipoteze wakati wetu nenda kwenye uwanja wa dini ukamwage !
 
Kwani enzi hizo wangapi walikufa njaa? kutugeuza gulio la waarabu wachina na wazungu ndo solution. kufanywa gulio au ili la sasa la kuwaleta wazungu wachukue mali zetu si maamuzi yanayoitaji akili.Ni maamuzi ya kichovi ambayo yataturudisha tu kwenye utumwa.
 
Zhule wacha kujidanganya kwamba umegeuzwa gulio la waarabu na wachina. Ni wewe mwenyewe ndio umetaka kugeuzwa gulio. Nani anasaini mikataba mibovu kwa tamaa ya kupata commission? Na nani anawapa wahindi akina Patel na wenzake hizo tender ili wapate chao? Ni sisi wenyewe ngozi nyeusi watanzania wazawa. Hakuna mchina wala muhindi aliyekulazimisha usaini mikataba mibovu kwa njaa yako, au utoe tenda kwa tamaa ya kuwekewa kwenye account huko nje.

Amka ndugu amka jichunguze wewe kwanza kabla ya kulaumu wenzako.
 


wewe ndio mwongo. hao waliokuwa na tv walikuwa wanaangalia kituo gani na tv tanznaia zimeanza mwaka 1994? mmeshasahau maduka ya ushirika? ama kweli
 

Watu wakushukuru kwa soko huria ni Marehemu Sokoine(Waziri mkuu) na marehemu Kombe(Mkuu wa usalama wa Taifa)kwa wakati huo ambao walifanya kazi kkubwa sana kmshawishi Mwalimu Nyerere hadi akakubali Mwaka 1984 Mwinyi amekuta kazi hiyo imeisha fanywa mwaka 1985 alipochaguliwa kuwa Rais.
 

Inaelekea wewe ni kijana mdogo sana! mwaka 1974 kulkiuwa na njaa haijapata kutokea katika historia ya nchi yetu watu wengi walikufa kwa njaa mpaka tukaletewa mahindi ya njano kutoka marekani,zama hizo ulijulikana mahindi ya yanga!Unalijua hilo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…