Ndugu yangu amepata msongo wa mawazo (depression)

Aje nimfundishe kunywa pombe na kununua vichwa ambiance
 
Sawa mkuu hali yake imebadilika ghafla tangu juzi hata simu hapokei ( hajitambui )
Sawa mkuu hali yake imebadilika ghafla tangu juzi hata simu hapokei ( hajitambui )
Aisee pole yake,Atakaa sawa, depression ni tatizo la akili,
Hapo ni mazoea tu ndiyo yanamsumbua kwa sasa,
USHAURI:Akae na watu wake wa karibu pia kipindi hiki,km wazazi,marafiki nk,itamsahaulisha
Simu atakuja kuacha kutumia bila hata kuambiwa,hapo kuna vitu kama WhatsApp anafanyiwa na ex wake,so ndio inavyokuwaga,
kwa vitu kama simu dawa ni mazoezi,ataacha,kama anashughuli ya kufanya,aweke bidii,atasahau tu
kawaida Depression huwa inaweza chukua hata miaka2 kuisha,kama,inategemea na kitu kinachokupa unyonge huo,
mfano mmekaa kwenye mahusiano say miaka 15 au 20,alafu inatokea kitu kama hicho,hapo ndio inakuwaga ngumu kufuta memory,
Au umejenga nyumba yako kwa miaka 10,alafu unakuja ambiwa bomoa nyumba,inapita treni,pata picha msongo wake wa mawzo,
Ndugu yenu,kaeni nae karibu kipindi hiki,mpeni hata moral support,AFTER ALL,Wanawake wengi siku hizi.
 
Mkuu pole sana. Nakufariji kwanza na usijali hiyo hali itakaa sawa wenyewe kwa mdogo wako huyo mimi nishapitia huko.
 
Ni kweli mkuu mimi ilikuwa zaidi ya mwanamke,uchumi(sina kazi),familia nilipambana sana mwenyewe vilevi kwa wingi na mambo mengi ya ajabu ajabu ilifikia kipindi kila kukicha ni afadhali ya jana sikumbuki ilikuwaje ghafla nikaanza maombi ASANTE YESU na hali yangu ilibadilika sana ndani ya miezi 8
Namshukuru Mungu kwakweli amenipigania sana
 
Nimewahi kupatwa na tatizo hili, time is the best healer!
 
Aisee nilipitia pia hali hiyo...
 
DEPRESSION INAWEZA PELEKEA SUICIDAL...

Kati ya matatizo hatari ya akili, Depression ni mojawapo... Anahitaji kuangaliwa kwa ukaribu mno ili asije akafanya vitu vya ajabu vyenye madhara kwake na hata kwa familia yake.

Kama hali itazidi kuwa mbaya zaidi, ni bora mumpeleke hospital akapate matibabu... Ziko dawa zinafahamika kama ANTI DEPRESSANTS ambazo ni maalumu kwa watu wenye depression.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hujakosea, alinitesa sana dada mmoja alitokea tabora sintosahau ila alinifunza na kunipa ujasiri kwa wanawake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…