Mfukize kwa majani ya kitunguusomu na mavi ya Tembo na na mavi ya punda siku hiyo anapozungumza lugha hiyo ya kiarabu kama kweli anayo mashetani wachafu watamkimbia hawata kuja tena kumletea matatizo wakati unamfukiza avae shuka nyeupe huku unamuombea kwa jina la Mwenyeezi mungu yamtoke hayo mapepo wanayomsumbuwa wakati unapomfukiza useme maneno haya ( Ewe pepo uliyekuwepo ndani ya taja jina lake (fulani bin fulani) ninakuondosha utoke ukimbilie baharini kwa jina la Mwenyeezi Mungu mmoja toka haraka) Sema mara 3 usikae mbele yake wakati unapomfukiza asije kukuvamia wewe kisha umfukize asubuhi na usiku kwa muda wa siku 3 yatamkimbia mwilini hayata rudi tena hayo mapepo yaliyomkumba.