Elections 2010 NEC sasa yagoma kuwalipa mawakala

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Kinyume na makubaliano kati ya vyama vya siasa na NEC katika dakika za lala salama kuelekea uchaguzi NEC wamegoma kuwalipa mawakala na kuwatupia zigo hilo vyama husika.

Leo kiongozi mmoja wa NCCR MAGEUZI alionekana Channel Ten jioni hii akilia na NEC kwa kukiuka makubaliano yake na vyama vya siasa.

Zimekuwepo shutuma nyingi dhidi ya NEC kuyachakachua matokeo na kuwanufaisha CCM na hili ni jipu jingine ambalo laweza kupasuka wakati wowote ule.

Mawakala wa vyama vya siasa ndiyo inasadikiwa ni karata turufu ya kumwokoa JK na CCM kutoka kwenye kibanio cha kudhalilishwa vibaya na Chadema kwenye chaguzi hii.

Hivyo kutowalipa mawakala yawezekana kabisa kuwa ni njama ya kuwaweka mawakala hao katika hali ya tafurani ambayo endapo vyama vyao vikishindwa kuwalipa CCM ikawalipa na hivyo kuzua utata wa wanawajibika kwa nani na hivyo kuufanya uchaguzi huu kutokuwa wa huru na wa haki.

Pamoja na Mwenyekiti wa NEC kuahidi chaguzi hii kuwa ya huru na haki yapo matendo mengi ya NEC yanayoashiria kuwa nia hii siyo ya dhati na kutoka moyoni.

Zimekuwepo kauli za kutofautiana kati ya NEC na wasimamizi wa chaguzi majimboni na hili NEC imeshindwa kuwakemea wasimamizi hao au hata kutoa mwongozo unaoeleweka hususani kwenye eneo la wapigakura kuwa mita 100 kutoka vituo vya kuhesabia kura kuhakikisha haki inatendeka........Msimamizi wa Tarime amedai wapigakura wajiendee majumbani na watajulishwa matokeo jambo ambalo Naibu Mwenyekiti wa NEC tayari alikwisha kutoa mwongozo tofauti kabla ya hapo alipouulizwa swali na mgombea ubunge wa jimbo la Bukoba mjini Bw. Rwakatare..........NEC walisema ni ruhksa kwa wapigakura kuwa mita 100 kutoka vituo vya kupiga kura............
 
Ni njama tu ili kupunguza nguvu ya CHADEMA. Wanajua CCM imejikusanyia fedha nyingi za kiufisadi na wanaweza kuwalipa mawakala na kuwaonga walalahoi. Kwani hujui NEC ndo CCM?
 
this was not unexpected... lots of money involved by a corrupt system to finish off vichwa ngumu

lets wait for 2015, inshallah
 
Ni njama tu ili kupunguza nguvu ya CHADEMA. Wanajua CCM imejikusanyia fedha nyingi za kiufisadi na wanaweza kuwalipa mawakala na kuwaonga walalahoi. Kwani hujui NEC ndo CCM?
si chadema pekee hata kafu zanzibar na bara, tusisahau kafu ni chama muhimu sana

CCM is very smart, bilioni 70 kwa miraji, vijisenti kwa uchaguzi na mawakala

LOL
 
hatuhitaji watulipe, kama wanataka wawalipe mawakala wa CCM, sisi tutajilipa wenyewe, KURA NI ZETU MALIPO YA NINI? TUTALINDA KURA ZETU KWA GHARAMA ZETU.
 
Ndiyo maana tunasema tena, na nimeshauri ktk thread nyingine kuhusu mawakala kutokulipwa. Majibu ni haya.
MOJA: TUME ISHITAKIWE KWA UMOJA WA ULAYA- EU, NA WAFADHILI AMBAO NDIO WALISHATOA FEDHA ZA UCHAGUZI NA PIA WASHITAKIWE MAHAKAMANI.

PILI, VYAMA VIANDAE MAANDAMANO YA AMANI HARAKA, WAWASILISHE UKIUKWAJI HUU KWA UMOJA WA ULAYA, UBALOZI WA MAREKANI WAUJUE UNAFIKI NA UOZO HUU NA PIA KESI MAHAKAMANI.

TUME KWA MBINU HII YA UOVU, INAISAIDIA CCM ISHINDE KWA WIZI NA KUHONGA MAWAKALA.
 
Dr alisema jana ulinzi wa kura ni kazi yetu achana na mawakala
 
hatuhitaji watulipe, kama wanataka wawalipe mawakala wa CCM, sisi tutajilipa wenyewe, KURA NI ZETU MALIPO YA NINI? TUTALINDA KURA ZETU KWA GHARAMA ZETU.
wewe unaongea hivyo kwasababu haupo kwenye ground.. tumezoea

bila pesa kura zinaibiwa... hebu niambie wewe ni wakala wa wapi?? au ndio walewale mavuvuzela??

You have posted something that shows you are not on teh ground

bila pesa za wakala kura huna

njaa kali
 
do you trust EU??? unadhani hao richmond, tanzania one, GGM etc wanapata wapi sapoti

wake up buddy
 

ACID njaa ya watu haipo kwenye uwakala, njaa ya watu ipo kwenye mabadiliko, na hili km huliamini subiri uchaguzi upite. chaguzi ndogo za Tarime pamoja na nguvu kubwa ya CCM bado walishindwa, KUMBUKA TARIME YA JUZI NDO TANZANIA YA LEO.
 
do you trust EU??? unadhani hao richmond, tanzania one, GGM etc wanapata wapi sapoti

wake up buddy

Guys, the concept behind this ni kuwa, the matter is made kwown to the whole world rather than assuming that here is no impact that can be made. Something is greater than nothing. these people need to be fully exposed.
 
Jamani jambo hili ni la msingi sana hasa maeneo ya vijijini. Unajua Tshs 10,000 kwa watu wa vijijini ni sawa la milioni kwa watu wengine. Nafikiri hoja hii ya NEC kutowalipa mawakala ni njia muhafaka ya kuutengenezea ushinsi CCM. Nina uhakika mawakala wengi wa vijijini kama watashindwa kulipwa ni rahisi sana kushawishiwa kuchakachua matokeo. Kuna haja ya kuliangalia suala hili kwa kina
 
Jamani hela ya mawakala ni muhimu sana. Hilo ni tengo la CCM. wapinzani wakomae na NEC. hela ipatikane else sijui kama kuna means zingine za kupata hizo hela.
 
Kinachowatia hofu NEC ni hii hali anayokumbana nayo bosi wao. lazima walinde mkate wao atii.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…